Maonyesho ya viwanda ni kichekesho

Maonyesho ya viwanda ni kichekesho

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2015
Posts
1,533
Reaction score
3,837
Wakuu,

Jana nilienda sabasaba kuangalia maonyesho ya viwanda, orodha ya viwanda nilivyo vikuta kule:

1. TBC
2. University of Dar es Salaam
3. Waagiza solar kutoka nje ya nchi na kuuza nchini
4. Waagiza incubator na mashine kutoka china kuleta nchini
5. Wauzaji wa bidhaa za kilimo kutoka Kenya
6. Wanaonunua asali wanapack nyumbani na kuja kuuza, hii haina tofauti na vyerehani vinne.
7. Viwanda vya ukweli ni Bakhresa, Nyumbu, watengeneza viatu pamoja na watu wa food processing kama tomato (red gold) nk

Maonyesho haya yaonekane kama changamoto kwa taifa, haiwezekani importers nao waende kwenye maonyesho ya viwanda wakati wao wanaagiza tu na kuuza. Wakuu ukweli ni kwamba Tanzania ya Viwanda bado, hamna viwanda kabisa.

Serikali ipunguze sehemu ya bajeti yake inayotumika kununua wapinzani na hizo pesa wapewe mikopo watu wenye nia ya kuanzisha viwanda.
 
458352.jpg
 
Hapo ndio panatakiwa tuone yale maelfu ya Viwanda ambavyo Mwijage amesema vimeshafunguliwa ndani ya Tanzania kwenye awamu hii ya tano.
 
Viwanda haviji kwa matamko! Viwanda huletwa na uwepo wa soko la bidhaa zinazotakiwa,Elimu ya viwanda ,malighafi, ubunifu wa raia/technologia hali wezeshi kwa ajili ya viwanda nishati,miundombinu n.k Kwa watu wenye elimu za shule za kata Tutasubiri sana. Inatakiwa kwanza uwekezaji kwenye elimu ,kuwekeza katika kuagiza teknolojia zaidi badala ya kununua bidhaa zilizo tayari na ku-import human capital kutoka nchi kama china na india ingesaidia.Inashangaza sana ukiona watu wanaopewa uraia wengi wanakuwa housewives huwa nachekaga sana.
 
Kuna tatizo, hata kina bakheresa kwa bidhaa zote wanazo onyesha kwenye maonyesho lazima tuangalie swala la Rule of origine (hii huwa inasema asilimia ngapi ya kinachozalishwa kisemekane kimezalishwa tanzania) mfano lazima uzalishe bidhaa ambazo ina 60% ya malighafi kutoka hapa nchini, endapo bidhaa hizo itakuwa pungufu ya 60% basi ujue sio bidhaa za tanzania ni za nje ila imechanganywa tayari imepoteza sifa ya made in tanzania. mfano kemikali nyingi zinazotumika kutengenezea vinywaji kama zinatengenezwa nje na ina sukari wanayo changanyia ya kutoka viwandani kama bado sukari hiyo wanaagiza nje bado haija kidhi vigezo vya kusema tanzania ina kiwanda cha kuzalisha vinywaji maana local content ya kinywaji ni asilimia kubwa ni kutoka nje, hapa tunachanganya tu.
 
So far sijaona a framework in place kusupport uanzishwaji na uendelezwaji viwanda. Sana nasikia watu wanatema mikwala...... nilikuwa ninawaza kwenda kuchukuwa mkopo nitafakari kuanzisha kiwanda mara paaaappp nikasikia wenye nyumba wanataka kupangiwa wasichukuwe kodi zaidi ya mwezi mmoja nikaona hatari iliyo mbele yangu....nawexa kuja kupangiwa bei ya bidhaa ntazozalisha nikashindwa rejesha mkopo....saivi niko niko tu naendelea na maisha mengine...
 
Back
Top Bottom