Maoni Yangu na Kinachoendelea Kwa Sasa

Maoni Yangu na Kinachoendelea Kwa Sasa

Mkoba Jnr

Member
Joined
Feb 8, 2025
Posts
66
Reaction score
133
Nakiri kuwa mimi sishabikii Simba, maoni nayotoa hapa sio ya kiushabiki bali ni uhalisia wa hali ilivyokuwa uwanjani

1.Pengo la Ahoua nadhani mmeliona. Zile faulo zilizokuwa zinapigwa pale nje ya box ingekuwa yule jamaa nadahni Mashujaa wangekuwa wameisha tangu kipidi cha kwanza. Wakati mwingine wekeni ushabiki pembeni, jamaa ni professional wa mipira ya kutengwa.

2.Mpira wa Simba kwa ndani ya Ligi nashauri usioneshwe kwenye TV maana matanganzo haya yanafika mbali na kimsingi karibu mechi zote za Simba msimu huu zimetawaliwa na utata wa kubebwa na waamuzi.

3.Tuondoe ushabiki pembeni tunahitaji kuwa na mpria wa haki ili tufurahie burudani sote . Mtu akipigwa, apigwe kihalali na sio kubebwa bebwa tu.

4. Wapo watu wanahoja eti kwa kuwa timu pinzani zinazocheza na Simba zinahaidiwa pesa, basi wao wanamalizana na refa. Hii ni hoja ya kitoto sana, hivi ahadi ya goli la mama kwenye mechi za kimataifa unaweza fananisha na hongo/rushwa. Kwamba RS Berkane waseme kwa kuwa Simba wamehaidiwa pesa, basi sisi tudeal na marefa. Ladha ya mpria itatoka wapi kwa mtindo huu.

5. Imeibuka hoja kuwa timu ndogo zinaikamia Simba. Ipo hivi kwa sasa Simba ndio timu ambayo ipo juu kwa Tanzania, wachezaji wa timu ndogo wanapocheza na timu ndogo wenao, wafuatiliaji wa hizo mechi ni wachache hivyo wachezaji hawajulikani. Ila inapokuja kutokea wanacheza na Simba, wafuatiliaji ni wengi na achezaji wanataka waonekane ili wapate fursa kwingineko. Hii hali ilikuwepo hata kipindi Yanga wanafanya vizuri kimataifa ukamiaji ulikuwepo. Hao kina Awesu, Baka,Kagoma, Fei wote wameonekana kwenye mashindano yanayotazamwa na wengi.

6.Mwisho kama mpenzi wa Mpira tuuukatae na kuukemea huu uhuni wa marefa. Mpira ni burudani, tunataka tuburudike na sio kuleta janja janja tu. Hivi kwa mfano mechi inaanza refa anawapa Simba penati au Yanga penati bila hata watu kucheza mpira kuna burudani gani hapo inayopatikana? MSIJIZIME DATA KWA KUWA MATOKEO YAMEKUWA UPANDE WENU, KUNA SIKU YATAKUWA UPANDE WA WENGINE WATAWAAMBIA MBONA NA NYINYI ILIKUA HIVI NA MLIFURAHIA. SIO KILA SIKU BAHATI ITAKUWA UPANDE WENU TU. TUKEMEE HILI JAMBO.
 
Mlianza nyie kwa sasa tulieni dawa iwaingie..
..goli la mkono
..mpira ulitoka nje pacome akauingiza ikawa goli.
...simu za rushwa kwny mechi ya Tabora na bado mamlaka zilikaa kimya.
...mechi anazocheza yanga chini ya mwamvuli wa udhamini ni mechi nyepesi zile timu 8.......juzi kocha wa FG amefukuzwa kwa kusema ukweli kuwa wanapeana.

Kwahyo usitegemee tutajuta kwa hilo la jana hata siku moja kwa sbb hakuna kosa alilolifanya refa hata moja....
 
Nakiri kuwa mimi sishabikii Simba, maoni nayotoa hapa sio ya kiushabiki bali ni uhalisia wa hali ilivyokuwa uwanjani

1.Pengo la Ahoua nadhani mmeliona. Zile faulo zilizokuwa zinapigwa pale nje ya box ingekuwa yule jamaa nadahni Mashujaa wangekuwa wameisha tangu kipidi cha kwanza. Wakati mwingine wekeni ushabiki pembeni, jamaa ni professional wa mipira ya kutengwa.

2.Mpira wa Simba kwa ndani ya Ligi nashauri usioneshwe kwenye TV maana matanganzo haya yanafika mbali na kimsingi karibu mechi zote za Simba msimu huu zimetawaliwa na utata wa kubebwa na waamuzi.

3.Tuondoe ushabiki pembeni tunahitaji kuwa na mpria wa haki ili tufurahie burudani sote . Mtu akipigwa, apigwe kihalali na sio kubebwa bebwa tu.

4. Wapo watu wanahoja eti kwa kuwa timu pinzani zinazocheza na Simba zinahaidiwa pesa, basi wao wanamalizana na refa. Hii ni hoja ya kitoto sana, hivi ahadi ya goli la mama kwenye mechi za kimataifa unaweza fananisha na hongo/rushwa. Kwamba RS Berkane waseme kwa kuwa Simba wamehaidiwa pesa, basi sisi tudeal na marefa. Ladha ya mpria itatoka wapi kwa mtindo huu.

5. Imeibuka hoja kuwa timu ndogo zinaikamia Simba. Ipo hivi kwa sasa Simba ndio timu ambayo ipo juu kwa Tanzania, wachezaji wa timu ndogo wanapocheza na timu ndogo wenao, wafuatiliaji wa hizo mechi ni wachache hivyo wachezaji hawajulikani. Ila inapokuja kutokea wanacheza na Simba, wafuatiliaji ni wengi na achezaji wanataka waonekane ili wapate fursa kwingineko. Hii hali ilikuwepo hata kipindi Yanga wanafanya vizuri kimataifa ukamiaji ulikuwepo. Hao kina Awesu, Baka,Kagoma, Fei wote wameonekana kwenye mashindano yanayotazamwa na wengi.

6.Mwisho kama mpenzi wa Mpira tuuukatae na kuukemea huu uhuni wa marefa. Mpira ni burudani, tunataka tuburudike na sio kuleta janja janja tu. Hivi kwa mfano mechi inaanza refa anawapa Simba penati au Yanga penati bila hata watu kucheza mpira kuna burudani gani hapo inayopatikana? MSIJIZIME DATA KWA KUWA MATOKEO YAMEKUWA UPANDE WENU, KUNA SIKU YATAKUWA UPANDE WA WENGINE WATAWAAMBIA MBONA NA NYINYI ILIKUA HIVI NA MLIFURAHIA. SIO KILA SIKU BAHATI ITAKUWA UPANDE WENU TU. TUKEMEE HILI JAMBO.
Iyo namba 2 unamaanisha mambo yafanyike gizani ili uchakachuaji ufanyike kwa siri?
 
Mlianza nyie kwa sasa tulieni dawa iwaingie..
..goli la mkono
..mpira ulitoka nje pacome akauingiza ikawa goli.
...simu za rushwa kwny mechi ya Tabora na bado mamlaka zilikaa kimya.
...mechi anazocheza yanga chini ya mwamvuli wa udhamini ni mechi nyepesi zile timu 8.......juzi kocha wa FG amefukuzwa kwa kusema ukweli kuwa wanapeana.

Kwahyo usitegemee tutajuta kwa hilo la jana hata siku moja kwa sbb hakuna kosa alilolifanya refa hata moja....
Na hapo umeacha mengi mnooo wanayofanya ndani na nje ya uwanja.

Anyway, Ubaya Ubwelaaaa!
 
Simba wanaleta utaratibu wa hovyo sana kwenye mpira wa nchi hii. Wanasusia mechi kwa sababu za kitoto kabisa, asilimia kubwa ya mechi zao msimu huu zimekua na maamuzi tata.

Hizi mbinu zao zikaanza kutumika na timu zingine zenye msuli wa pesa mfano azam na singida, tusije tukaanza kutafuta mchawi.
 
Simba imeingia Fainali ngumu ya CAF Kwa jasho na damu kwa kuzitoa timu Mapapa,inawezaje kubebwa kwa timu vijidagaa?
Kwa hiyo mnataka wachezaji wa Simba wakiangushwa ndani ya penati box marefa wapete?kisa kuwaogopa nyinyi wanunua mechi?
Kuna vitu vingine vina ushahidi wa wazi kabisa kapombe ameangushwa ndani ya box na mchezaji wa mashujaa kagusa mpira kwa mkono ndani ya box,mashujaa wamepoteza zaidi ya dk ishirini sana refa aache TU?
Hayo yote yapo na yanaonekana Sasa mnabisha Nini?
 
Watazamaji waliokaa uwanjani upande wa Shabalala pale yule Shujaa alipogusa mpira kwa mkono wote walipiga kelele kuashiria kaugusa mpira kwa mkono.
Pia ukiangalia reaction ya Shabalala mwenyewe utaona alishainua mikono juu kuashiria kua Shujaa alikamata.
Mlitaka refa afanyeje?
 
Iondolewe huo udhamini wa kubebana then ndo tuje tuongee hapa, vinginevyo Simba abebe tu ubingwa hata kwa penati kila mechi.
 
Wewe sio shabiki wa Simba ni pandikizi la utopolo. Acha kujizima data. UHUNI ufanye na mashujaa , nyinyi wengine mtoe milio na kujizima data. Pumbafu.
 
Watazamaji waliokaa uwanjani upande wa Shabalala pale yule Shujaa alipogusa mpira kwa mkono wote walipiga kelele kuashiria kaugusa mpira kwa mkono.
Pia ukiangalia reaction ya Shabalala mwenyewe utaona alishainua mikono juu kuashiria kua Shujaa alikamata.
Mlitaka refa afanyeje?
Mimi sizungumzii hilo tukio. bali tathmini ya mchezo kwa ujuml wake. Ila kama unaona mpira ulichezwa kwa haki hakuna shida, tutakumbushana haya yatakapojirudia kwa matokeo kutokuwa upande wenu.
 
Wewe sio shabiki wa Simba ni pandikizi la utopolo. Acha kujizima data. UHUNI ufanye na mashujaa , nyinyi wengine mtoe milio na kujizima data. Pumbafu.
Huwezi kutoa maoni bila kutukana?Unahisi unajua kutukana kuliko wenzio?Tukana tena hilo lishazoeleka. Au una matatizo ya akili?
 
Umeanza na Ahoua kisha ukaanza kutiririka nyongo zako .
Nimewadokeza tu.
Katika timu yenu wachezaji hawa muombe siku zote wasiwe majeruhi la sivyo mtapata tabu uwanjani
Kibu
Camara
Mpanzu
Ahoua
Hamza

Hao wanapokuwepo uwanjani wote mna uhaika kwa kushinda. Akikosekana mmoja kazi mnayo
 
Namaanisha ni mpira ambao hauna uhalisia, kunewbwa sana so ni bora wasioneshe kabisa tusubiri matokeo tu
Yanga vs FG golikipa wa FG alitoka golini akaacha lango wazi akaufuata mpira kwenye kona karibu na kibendera, halafu akaurudisha kwenye 18 yake yeye akiwa kwenye kona, Aziz Ki akafunga kwa hiyo cross ya golikipa. Hiyo ndio ladha tunayotaka ionyeshwe kwenye TV

NB: Kocha wa FG aliyemkemea golikipa wake, yeye ndio amefukuzwa kazi
 
Back
Top Bottom