kali KENYATTA
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 288
- 166
Mpaka sasa CHADEMA ina watia nia watano kwenye kinyang'anyiro cha kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwenye ushindani huu; namuona Tundu Lissu akishindana kwa ukaribu zaidi na Mwenyekiti wa chama ndungu Aikaeli Freeman Mbowe ukiachilia wagombea wengine watatu. Hii ni kwa sababu ya ushwawishi walionao ndani na nje ya chama chao.
Je, mchakato wa mwaka huu wa kumpata mpeperusha bendara ya CHADEMA unaharibiwa kwa Mwenyekiti kutia nia? Hasa ikizingatiwa kwamba wapenzi na wanachama wa CHADEMA walikuwa wameishafanya hitimisho juu ya uteuzi wa ndugu Tundu Lissu? Ambae kwa mtizamo na imani yao ndiye pekee anayeonekana anaweza kumkabili mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)?
La hasha, CHADEMA kama chama kinachojipambanua kuishi na kuienzi Demokrasia; kinapaswa kuwa mfano. Matendo yana kishindo kuliko maneno. Hivyo basi, CHADEMA inataka kuiambia jamii ya wapenda siasa zenye kufuata Demokrasia kwamba, kinaishi kwa matendo yale wanayoyahubiri. Hili ni jambo jema sana kama vyombo vinavyosimamia mchakato wa maamuzi vitatenda kazi yake kwa uwazi, bila upendeleo au msukumo wowote usiokua na dalili za kuienzi Demokrasia ndani ya CHADEMA . Historia itajengeka na heshima itatamalaki kwenye duru za siasa hizo. Vilevile, CHADEMA itakua inasahihisha makosa ya michakato kama hii ya huko nyuma. Kila mpenda Demokrasia ataimba mapambao ya ushindi kwamba DEMOKRASIA imeamua.
Kupata upinzani ndani ya mchakato wa CHADEMA kwa ndugu Tundu Lissu kuna faida nyingi. Mosi, kwa kawaida kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza. Pili, ushindi bila ushindani mgumu hauna hamasa. Watoto wa mjini wanasema, "atachukulia poa." Tatu, mchakato mgumu ndani ya CHADEMA unamuandaa mshindi vyema kwenda kukabiliana na hatua ya kushindana na CCM akiwa ameiva. Kwa mfano; wanamasumbwi hujiandaa sawa sawa na mpinzani atakayepambana nae. Hivyo basi, mchakato mgumu ndani ya CHADEMA ni maandalizi mazuri ya kumfanya mshindi awe ameiva kupambana na CCM.
Natambua hamu, matamanio na imani waliyonayo wale wanaosema Tundu Lissu apewe kijiti kwa kuwa anatosha. Hata hivyo, njia hii si sahihi sana. Inafanya uchaguzi kukosa hamasa. CCM mara nyingi wamefanya maajabu kwenye michakato yao ya kumsaka mgombea wa kiti cha Urais. Kwa mfano, hakuna aliyetegemea kwamba John Pombe Magufuli angelikua mgombea wa urais kupitia CCM mwaka 2015. Mchakato wao ndani ya chama uliitikisa nchi, macho yote yalihamia Dodoma. Kila mpenzi na mfuatiliaji wa siasa za Tanzania hakupenda kupitwa na tukio lolote. Hii ni nafasi nzuri ya CHADEMA kuboresha pale CCM wanapokosea, hasa pale wanapobaki makundi kinzani baada ya kuisha kwa mchakato wa ndani. Ni fursa kwa CHADEMA kuanzisha safari mpya ya matumaini na siasa zenye kulenga kujisahihisha na kuwa mfano wa kuigwa.
Mwisho, nawatakia CHADEMA mchakato mwema. Mchakato wenye uwazi, usiopendelea mtu kwa ubaguzi wowote ule, na wenye kuboresha umoja kuelekea uchaguzi wa mwaka 2020.
Je, mchakato wa mwaka huu wa kumpata mpeperusha bendara ya CHADEMA unaharibiwa kwa Mwenyekiti kutia nia? Hasa ikizingatiwa kwamba wapenzi na wanachama wa CHADEMA walikuwa wameishafanya hitimisho juu ya uteuzi wa ndugu Tundu Lissu? Ambae kwa mtizamo na imani yao ndiye pekee anayeonekana anaweza kumkabili mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)?
La hasha, CHADEMA kama chama kinachojipambanua kuishi na kuienzi Demokrasia; kinapaswa kuwa mfano. Matendo yana kishindo kuliko maneno. Hivyo basi, CHADEMA inataka kuiambia jamii ya wapenda siasa zenye kufuata Demokrasia kwamba, kinaishi kwa matendo yale wanayoyahubiri. Hili ni jambo jema sana kama vyombo vinavyosimamia mchakato wa maamuzi vitatenda kazi yake kwa uwazi, bila upendeleo au msukumo wowote usiokua na dalili za kuienzi Demokrasia ndani ya CHADEMA . Historia itajengeka na heshima itatamalaki kwenye duru za siasa hizo. Vilevile, CHADEMA itakua inasahihisha makosa ya michakato kama hii ya huko nyuma. Kila mpenda Demokrasia ataimba mapambao ya ushindi kwamba DEMOKRASIA imeamua.
Kupata upinzani ndani ya mchakato wa CHADEMA kwa ndugu Tundu Lissu kuna faida nyingi. Mosi, kwa kawaida kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza. Pili, ushindi bila ushindani mgumu hauna hamasa. Watoto wa mjini wanasema, "atachukulia poa." Tatu, mchakato mgumu ndani ya CHADEMA unamuandaa mshindi vyema kwenda kukabiliana na hatua ya kushindana na CCM akiwa ameiva. Kwa mfano; wanamasumbwi hujiandaa sawa sawa na mpinzani atakayepambana nae. Hivyo basi, mchakato mgumu ndani ya CHADEMA ni maandalizi mazuri ya kumfanya mshindi awe ameiva kupambana na CCM.
Natambua hamu, matamanio na imani waliyonayo wale wanaosema Tundu Lissu apewe kijiti kwa kuwa anatosha. Hata hivyo, njia hii si sahihi sana. Inafanya uchaguzi kukosa hamasa. CCM mara nyingi wamefanya maajabu kwenye michakato yao ya kumsaka mgombea wa kiti cha Urais. Kwa mfano, hakuna aliyetegemea kwamba John Pombe Magufuli angelikua mgombea wa urais kupitia CCM mwaka 2015. Mchakato wao ndani ya chama uliitikisa nchi, macho yote yalihamia Dodoma. Kila mpenzi na mfuatiliaji wa siasa za Tanzania hakupenda kupitwa na tukio lolote. Hii ni nafasi nzuri ya CHADEMA kuboresha pale CCM wanapokosea, hasa pale wanapobaki makundi kinzani baada ya kuisha kwa mchakato wa ndani. Ni fursa kwa CHADEMA kuanzisha safari mpya ya matumaini na siasa zenye kulenga kujisahihisha na kuwa mfano wa kuigwa.
Mwisho, nawatakia CHADEMA mchakato mwema. Mchakato wenye uwazi, usiopendelea mtu kwa ubaguzi wowote ule, na wenye kuboresha umoja kuelekea uchaguzi wa mwaka 2020.