KINGA YA NYUMBA DHIDI UCHAWI ,
TAFADHALI,kama huna kinga ya mwili usifanye hiki hadi upate kinga ya mwili sababu ukiweka hii utailinda nyumba ila wale watu watakulinda wewe ,ukitoka tu nje ya nyumba tayari ,
Upate NDIMU ,7 na sindano 7 ,na nyembe 7,kisha unaweka sindano kuchoma NDIMU na wembe utakaa dizaini hiyo pichani ,
Ukimaliza nuiza ,kisha shimo wastani moja chimba ,mbele ya nyumba nyuma ya nyumba pembeni na ubavuni hakiki , nyumba inakua katikati kisha kila kishmo ,zika NDIMU na sindano na wembe mmoja viwe kama hivyo pichani ,
Ila hakiki unafanya hivyo haoni mtu , yeyote ,
Basi wachawi wote watajuta ,
Ni mara moja tu kufanya ,
Picha hii nimetoa kama mfano tu ,ila hapo ni shughuli ya alibadili kuna vitu vinaongezeka hapo kama chumvi ya mawe buni nk,kama unavyoona na mbuzi awe pembeni wakina juma Khamisi ndio wanajua hizo shughuli ,hapo ni pigo moja tu mtu anasahau kwao , alibadili sio mchezo ,
Hasa kama mambo ya urithi ,mashamba , nyumba ,gari ,ni kafara nzito ,unaweza dhuru ,kama ni shamba ,mkwezi aliyechukua nazi punda aliyebeba mzigo ,aliyenunua ,aliyezipeleka sokoni , muuzaji mpaka mnunuaji ,
Hivyo hapo ni mfano wa kupachika zile sindano na nyembe kwa NDIMU ,ila vingine hapo havihusiani kama chumvi na buni hiyo ,
View attachment 2112043