Mroojr
Member
- Nov 15, 2010
- 65
- 8
Kulingana na habari za awali tulizo nazo bus hilo la Bunda limefumaniwa kwenye kivuko cha treni na kugongwa.Mpaka sasa ni watu 4 wamethibitika kufa na tunaendelea kufuatilia habari zaidi juu ya tukio hilo ikiwemo sababu ya msingi ya kusababisha ajali hiyo.Tutaendelea kuwajuza zaidi chochote kitakachojiri ikiwemo kuwawekea picha tutakazojaaliwa kuzipata nzuri.
============
============
Habari nilizozipata hivi punde zinasema kuwa Kuna ajali imetokea ikilihusisha Basi la Bunda Express lililokuwa likitokea Dodoma kwenda Mwanza asubuhi hii limegongana na Treni Eneo la Manyoni mkoani Singida.
Kwa mujibu wa chanzo changu cha habari cha kuaminika ambacho kipo Eneo la tukio Bado hawajajua idadi ya majeruhi na waliokufa lakini inaonekana ajali ni mbaya na ameshuhudia tayari maiti moja.
Majeruhi Tayari wamepelekwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Manyoni
Picha nitaweka hivi punde na Update zaidi.