Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
Mkazi wa Mtaa wa Ndejengwa jijini Dodoma, Laurent David, amefariki dunia baada ya kugonga treni ya mzigo akiwa eneo la reli.
Inaelezwa aliaga nyumbani kwamba anaenda kufanya mazoezi.
Ajali hiyo imetokea leo, Jumamosi Desemba 30, 2023 saa 12 asubuhi kwenye Reli ya Kati. Laurent inaelezwa alikuwa amekaa juu ya reli akisikiliza muziki kwenye spika za masikioni, hivyo hakusikia honi za treni.
Athumani Sweya, aliyeshuhudia tukio hilo amesema aliiona treni ilipokuwa inapita na ilipiga honi lakini kijana huyo hakusikia.
Anasema alipotaka kumsukuma ili atoke relini treni tayari ilikuwa imeshafika na kuigonga.
David Zabron, baba mzazi wa Laurent, akizungumza akiwa eneo la tukio amesema kijana wake aliondoka nyumbani saa 11 alfajiri akisema anaenda kufanya mazoezi uwanjani.
Inaelezwa aliaga nyumbani kwamba anaenda kufanya mazoezi.
Ajali hiyo imetokea leo, Jumamosi Desemba 30, 2023 saa 12 asubuhi kwenye Reli ya Kati. Laurent inaelezwa alikuwa amekaa juu ya reli akisikiliza muziki kwenye spika za masikioni, hivyo hakusikia honi za treni.
Athumani Sweya, aliyeshuhudia tukio hilo amesema aliiona treni ilipokuwa inapita na ilipiga honi lakini kijana huyo hakusikia.
Anasema alipotaka kumsukuma ili atoke relini treni tayari ilikuwa imeshafika na kuigonga.
David Zabron, baba mzazi wa Laurent, akizungumza akiwa eneo la tukio amesema kijana wake aliondoka nyumbani saa 11 alfajiri akisema anaenda kufanya mazoezi uwanjani.