tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 26,021
- 25,423
Sakata la mali za John Komba kupigwa mnada kufuatia deni la Tsh bilion 1.2 analodaiwa na benki ya CRDB limefikia tamati baada ya mfanyabiashara nguli na Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Bw Yusuf Manji, kununua shule zake pamoja na baadhi ya mali zake ambazo zilikuwa zipigwe mnada.
Komba alikuwa anakabiliwa na uwezekano wa shule na mali zake kupigwa mnada (na kufungwa jela) ili kufidia deni hilo alilokopa CRDB miaka 5 iliyopita.
Source: Mwananchi.
MAONI YANGU
Komba amshukuru sana Manji kwa kumuokoa kwenda jela na mali zake kupigwa mnada. Sipati picha kama Komba angefungwa jela kile kitambi chake angekificha wapi. Lazima kingenywea kama puto lililotoboka. Hivi alidhani kuendesha shule ni lelemama au ni sawa na kuimba kwaya na kusimamia bendi? Chezea mikopo wewe!
Komba alikuwa anakabiliwa na uwezekano wa shule na mali zake kupigwa mnada (na kufungwa jela) ili kufidia deni hilo alilokopa CRDB miaka 5 iliyopita.
Source: Mwananchi.
MAONI YANGU
Komba amshukuru sana Manji kwa kumuokoa kwenda jela na mali zake kupigwa mnada. Sipati picha kama Komba angefungwa jela kile kitambi chake angekificha wapi. Lazima kingenywea kama puto lililotoboka. Hivi alidhani kuendesha shule ni lelemama au ni sawa na kuimba kwaya na kusimamia bendi? Chezea mikopo wewe!