Manispaa ya Temeke yakosa utu , yaanza kuwadhalilisha wafanyabiashara waliochelewesha malipo bila kujali janga la corona

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,650
218,105
Pamoja na serikali ya Tanzania kutambua ugumu wa mzunguko wa biashara nchini humo kutokana na janga la Corona , na kupitia BOT imetoa maelekezo kwa benki zote kutoa nafuu ya marejesho ya madeni ya mikopo kwa wateja wake , ambapo baadhi ya benki nchini Tanzania ikiwemo Exim bank , ambayo imetoa likizo ya malipo kwa wateja wake wanaodaiwa kwa miezi mitatu kuanzia June hadi Septemba .

Lakini leo Maduka yanayozunguka stendi ya mabasi ya kusini kwenye eneo la Tandika yamefungwa na mmiliki wa jengo ambaye ni Manispaa ya Temeke , amewafungia milango wafanyabiashara ambao ni wapangaji wake kwa kuchelewa kulipa kodi kwa miezi miwili na wengine miezi mitatu , bila kujali ugumu wa biashara zao kutokana na corona , zipo pia taarifa za Manispaa hiyo kuanza kuwasaka waliochelewesha malipo ya kuhuisha leseni zao na ambao bado hawakupata leseni za biashara .

Si lengo langu kutetea wafanyabiashara wasiolipa bali ninaishangaa Manispaa kwa timing ya kichovu ya jambo lenyewe kutokana na hali halisi , wenzako wanatoa nafuu wewe unawakomesha watu wako ! haikuwa sahihi kwa sasa kuanza kuwahangaisha wajasiriamali kutokana na mambo yalivyo , Hali ni ngumu mno , na hasa kwa maeneo ya DSM ambayo baadhi ya wakazi wamekimbia na wengine wanakataa kurudi tena kwa sasa ili kujiokoa na corona .
 
Walipe pesa ya kodi maana wako msitari wa mbele kuisifia serikali kwa mbwembwe kua haijafungia biashara zao tangu corona ianze hadi muda huu wanafanya biashara kwa uhuru kabisa.
 
Pamoja na serikali ya Tanzania kutambua ugumu wa mzunguko wa biashara nchini humo kutokana na janga la Corona , na kupitia BOT imetoa maelekezo kwa benki zote kutoa nafuu ya marejesho ya madeni ya mikopo kwa wateja wake , ambapo baadhi ya benki nchini Tanzania ikiwemo Exim bank , ambayo imetoa likizo ya malipo kwa wateja wake wanaodaiwa kwa miezi mitatu kuanzia June hadi Septemba .

Lakini leo Maduka yanayozunguka stendi ya mabasi ya kusini kwenye eneo la Tandika yamefungwa na mmiliki wa jengo ambaye ni Manispaa ya Temeke , amewafungia milango wafanyabiashara ambao ni wapangaji wake kwa kuchelewa kulipa kodi kwa miezi miwili na wengine miezi mitatu , bila kujali ugumu wa biashara zao kutokana na corona , zipo pia taarifa za Manispaa hiyo kuanza kuwasaka waliochelewesha malipo ya kuhuisha leseni zao na ambao bado hawakupata leseni za biashara .

Si lengo langu kutetea wafanyabiashara wasiolipa bali ninaishangaa Manispaa kwa timing ya kichovu ya jambo lenyewe kutokana na hali halisi , wenzako wanatoa nafuu wewe unawakomesha watu wako ! haikuwa sahihi kwa sasa kuanza kuwahangaisha wajasiriamali kutokana na mambo yalivyo , Hali ni ngumu mno , na hasa kwa maeneo ya DSM ambayo baadhi ya wakazi wamekimbia na wengine wanakataa kurudi tena kwa sasa ili kujiokoa na corona .
Ndani ya ccm kuna watu na mizimu
 
Back
Top Bottom