Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
- Thread starter
- #21
Mchambuzi,
Hoja zako ni nzito na tutazijadili kama ulivyozigawanya taratibu.
Kwa kuanzia, Wanajamvi naona kuna kutomuelewa Mchambuzi katika aya ya kwanza kabisa ya bandiko lake.
Naomba kwa hisani yake niweke sawa alichokusudia ili tujikite katika mada zaidi na si katika sintofahamu inayojitokeza.
Katika aya hiyo ya kwanza, Mchambuzi ameandika kuwa ujio wa Kinana na Mangula umeonekana kuleta tumaini miongoni mwa Watanzania. Mstari wa mwisho ameuliza kwanini Mangula na Kinana kama watu wawili waonekane kuwa na uwezo wa kupambana na tatizo la kijamii na wala siyo taasisi kubwa zinazotumia mabilioni ya fedha za walipa kodi?
Kwa maneno mengine,iweje Mangula na Kinana wawe zaidi ya taasisi kama TAKUKURU ? Kwanini watu wanaamini kuwa Mangula na Kinana wana ufunguo wa tatizo la kijamii kubwa kuliko watu wawili, kumi, mia au elfu?
Na wala hukumaanisha kuwa ujio wa wawili hao ndio tumaini la suluhu.
Katika ayaya pili, natofautiana na Mchambuzi hasa pale anaposema Mchambuzi, huko mbele katika mada yako umezungumzia kitu kinaitwa Political will. Ili kuwe na consensus ni lazima kuwe na political will.
Nadhani wapinzani kwa ujumla wao wamekuwa ''pro-consensus'' kwa bahati mbaya hawana right partner katika kutafuta suluhisho.
Taarifa zote za tatizo la rushwa zinatolewa na taasisi za serikali, vyama au kupitia wazalendo wa nchi hii wanaochukua risk kubwa sana. Taarifa zimetumika kuifikia serikali ili ichukue hatua kama sehemu ya political will, consensus and solution
Tuna mlolongo wa matukio na mengine ya karibuni tu. Badala ya chama husika chenye serikali kushirikiana na Wapinzani, imekuwa ni kinyume chake. Kwa muktadha huo, je political will ipo? na kama haipo consensus itatoka wapi? Na kwanini tuanze kuwahukumu waleta mashitaka sawa na washtakiwa?
Mimi sidhani kuwa baada ya wapinzani kukosa partner katika suala hili,wao kulieleza kwa umma hiyo ni political asset! Yes, down the road inaweza kuwa hivyo lakini kwa wakati tulio nao hiyo inabaki kuwa silaha yao pekee katika vita dhidi ya rushwa Japo kwa kuanzia tu. Sina maana ya kuwa ni suluhu ya tatizo lakini basi ni sehemu ya utambuzi wa tatizo.
Kwa vile upande mwingine umeshindwa ''ku-cross the isle'' basi hilo linabaki kuwa liability by default.
Natumaini hoja yako ni ya utaifa zaidi ya uchama nami nakubaliana nawe kabisa.
Sina nia ya kutoka nje ya mada, tuendelee na core issue
Nguruvi3,
Asante sana kwa kunisaidia kuliweka suala hili vizuri zaidi hasa kwa wachangiaji ambao wanaona hoja yangu imekaa kichama zaidi; Kuhusu suala la political will na political asset, kimsingi nakubaliana na wewe; tofauti yetu kama ipo pengine ni kwamba - kuna ishara kubwa kwamba vyama vyote vya siasa vinajaribu kutumia hoja husika kisiasa zaidi, jambo ambalo linaweza kuwa sawa tu, ili mradi mwisho wa siku, the political process inatumika kuleta mabadiliko husika - kwa vitendo, sio kila upande kujaribu ku - manipulate suala hili kwa manufaa yake; Niseme pia kwamba nadhani uchaguzi wa 1995, suala hili lilikuwa manipulated kwa kumweka mgombea urais safi huku root-cause ya rushwa na ufisadi ikibakia intact bila kuguswa; ni muhimu tusirudi kule kule; nitajadili hili la political will na political asset zaidi baadae; Asanta sana;