Judgement
JF-Expert Member
- Nov 13, 2011
- 10,327
- 4,780
Nianze kwa kumtakia RIP, kwani hatunae katika uso wa ardhi.
Si mara moja au mbili, ni mara nyingi Baba yangu nikiwa tumekaa nae zama za uhai wake, alikua akiyarejelea maneno haya :-
(Nikimnukuu)
Baba > Mwanangu mimi Baba yako nimekua, na nimekutana na mengi.
Katika dunia hii mwanangu ukitaka ufanikiwe kimaisha , ishi na watu vizuri.
Na uweke taswira usoni kwako kua watu ndiyo mtaji wako, na wewe ni mtaji kwa watu wengine.
Hakikisha usibweteke na mali za ndugu zako na ukazitegemea, nenda juu chini umiliki za kwako.
Ishi na familia yako kwa mapenzi, lakini usisahau kua mkeo si ndugu yako.
Na katika dunia hii mwanangu unapokutana na watu (binadamu) ukawasikia mtu anakwambia
"Mimi sipendi wizi kwelikweli "
"Mimi sipendi uongo"
"Mimi sipendi uzinzi"
Basi mwanangu uwasikiapo watu wakijinadi kwa kauli hizo , waangalie kwa macho mawili , kwani hua wanakua ni kinyume na kauli zao.
Anaejinadi hapendi uzinzi basi ndiyo mzinzi nambari one !
Mwanangu wale wenye tabia na mienendo yao mema hua hawajinadi , huvaa silka ya tabia zao kimyakimya na jamii ndiyo huwatambua.
(mwisho wa kunukuu)
Binafsi yangu maneno haya ya Baba yote ninayaona ukweli wake.
Si mara moja au mbili, ni mara nyingi Baba yangu nikiwa tumekaa nae zama za uhai wake, alikua akiyarejelea maneno haya :-
(Nikimnukuu)
Baba > Mwanangu mimi Baba yako nimekua, na nimekutana na mengi.
Katika dunia hii mwanangu ukitaka ufanikiwe kimaisha , ishi na watu vizuri.
Na uweke taswira usoni kwako kua watu ndiyo mtaji wako, na wewe ni mtaji kwa watu wengine.
Hakikisha usibweteke na mali za ndugu zako na ukazitegemea, nenda juu chini umiliki za kwako.
Ishi na familia yako kwa mapenzi, lakini usisahau kua mkeo si ndugu yako.
Na katika dunia hii mwanangu unapokutana na watu (binadamu) ukawasikia mtu anakwambia
"Mimi sipendi wizi kwelikweli "
"Mimi sipendi uongo"
"Mimi sipendi uzinzi"
Basi mwanangu uwasikiapo watu wakijinadi kwa kauli hizo , waangalie kwa macho mawili , kwani hua wanakua ni kinyume na kauli zao.
Anaejinadi hapendi uzinzi basi ndiyo mzinzi nambari one !
Mwanangu wale wenye tabia na mienendo yao mema hua hawajinadi , huvaa silka ya tabia zao kimyakimya na jamii ndiyo huwatambua.
(mwisho wa kunukuu)
Binafsi yangu maneno haya ya Baba yote ninayaona ukweli wake.