Mimi nichukue fursa hii kuwapa pole , lakini niwe jasiri sana kusema ukweli kama ninyi waandishi hamtafanya editing ..
Kwanza kabisa niweke wazi kuwa jambo hili limesababishwa na chokochoko za udini ambazo muasisi wake ni serikali ya CCM na viongozi wake, aliyepiga bomu hapa leo sio jambazi wa kutaka mali bali ni mtu aliyeelewa na kufundishwa tofauti kwa nia mbaya kuhusu dini nyingine, haya maneno ya udini yalianzishwa na viongozi wa chama tawala lengo likiwa ni kuwagawa na kuwatawala raia lakini kwa sasa wamelikoroga, wamewachonganisha watu wa dini mbali mbali haswa waislamu na wakristo ambao ndio wengi ktk taifa hili bila kujua madhara ya mkakati huu kuwa utaligawa taifa.
Sasa basi kazi hiyo haya ndio mavuno yake kwani tukio hili lina sura zote za kiimani, na nilitake jeshi la polisi kufanya kazi ya kukamata haraka kama ambavyo walinikamata mimi nyumbani kwangu kwa mabomu na vitisho, poleni sana .
Haya ndio maneno aliongea Lema
Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums