KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,223
- 56,875
Alipoona Kandili hajibu neno aliongeza, “Nitakuibia siri yetu wanawake. Sisi huwaweka wanaume wote katika mafungu matatu. Fungu la kwanza ni la wale wanaume ambao tunawapenda kwa dhati. Wanaume ambao tuko tayari kuishi nao kwa heri au shari.
Kundi la pili ni la wanaume wazuri wa sura ya umbo. Kundi hilo tunalipenda kwa ajili ya kujionyesha tu mbele ya wenzetu. Anapita kijana mzuri. Wenzako wote wanababaika. Wewe unajitapa: ‘Yule wangu.’ Kundi la tatu ni la akina Bon. Watu wabaya au wazee. Tunawafuata kwa ajili ya uzito wa mifuko yao. Wao …”
Haikuwa mara ya kwanza kwa Kandili kusikia falsafa biyo. Hivyo alimkatiza Maua kwa kufoka tena: “Kwa hiyo mimi niko katika kundi lipi kati ya hayo?”
“Wewe. Wewe umeziba mwanya kwa makundi yote,” alijibiwa. “Wewe ni wewe tu mpenzi. Niamini tafadhali.”...
nimecheka sana haswa hilo jibu la maua mpaka nimeamua ku share nanyi waungwana!..😂
kitabu ni "pesa zako zinanuka"
muandishi Ben Mtobwa.
Kundi la pili ni la wanaume wazuri wa sura ya umbo. Kundi hilo tunalipenda kwa ajili ya kujionyesha tu mbele ya wenzetu. Anapita kijana mzuri. Wenzako wote wanababaika. Wewe unajitapa: ‘Yule wangu.’ Kundi la tatu ni la akina Bon. Watu wabaya au wazee. Tunawafuata kwa ajili ya uzito wa mifuko yao. Wao …”
Haikuwa mara ya kwanza kwa Kandili kusikia falsafa biyo. Hivyo alimkatiza Maua kwa kufoka tena: “Kwa hiyo mimi niko katika kundi lipi kati ya hayo?”
“Wewe. Wewe umeziba mwanya kwa makundi yote,” alijibiwa. “Wewe ni wewe tu mpenzi. Niamini tafadhali.”...
nimecheka sana haswa hilo jibu la maua mpaka nimeamua ku share nanyi waungwana!..😂
kitabu ni "pesa zako zinanuka"
muandishi Ben Mtobwa.