Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kiko wapi sasa, niliposema kufukuzwa kwa amorim yalikua makosa makubwa ndio hivi sasa. itapendeza vipigo viendelee hivi hivi, tena mancity ajipigie hata 7 pale old Trafford. Ety kocha fletcher,ole na Carrick time will tell. Glazers na Ratcliffe ni wamiliki wapuuzi wanaongozwa na hisia bila kutumia akili.
 
Mlisema shida ni Sancho, mara Rashford, mara Onana, Amorin. Wote hao hawapo, mkasema Maino hachezeshwi, Maino kachezeshwa. shida ni nn? Bruno au?
 
Nimesema tena ...hii timu HAITOKAA ifanikiwe Hadi mambo kadhaa yafanyike nayo ni kuondoa utawala wa uingereza kwenye klabu hio , timu ipewe any UAE national citizen ready to take over ...
 
Nimesema tena ...hii timu HAITOKAA ifanikiwe Hadi mambo kadhaa yafanyike nayo ni kuondoa utawala wa uingereza kwenye klabu hio , timu ipewe any UAE national citizen ready to take over ...
 
Nlitoa sababu za kufukuzwa amorim nikaambiwa sijui mpira πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ na Bado. ..
 
Nlitoa sababu za kufukuzwa amorim nikaambiwa sijui mpira πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ na Bado. ..
Ingependeza kama ungewa tag waliokwambia hujui mpira ili wakuelezee wamiliki na puppet wao fletcher anaipeleka wapi timu kabla ole na Carrick hawajarudi 😁😁😁
 
Ingependeza kama ungewa tag waliokwambia hujui mpira ili wakuelezee wamiliki na puppet wao fletcher anaipeleka wapi timu kabla ole na Carrick hawajarudi 😁😁😁

Mkuu na Hawa sijui watawaambia hawajui mpira ..Hawa ni mashabiki wa huko wanaongea..anachokisema ndio nmekisema juzi kati
 
View attachment 3528811
Mkuu na Hawa sijui watawaambia hawajui mpira ..Hawa ni mashabiki wa huko wanaongea..anachokisema ndio nmekisema juzi kati
Mkuu ninawajua mashabiki wa kweli wanaozipenda timu zao tena sio kwa kuwangalia tu hata kupitia michanga yao. Lakini pia nawajua mashabiki wa mpira ambao ni very idiot. Hivyo watu wa hivi usiwe unajiangaisha nao.

Maana kila mshabiki wa man united anayejitambua vizuri kichwani ambaye dishi lake halijayumba na kuitaji kubadilisha housing ya dishi lake. Lazima atakua anajua kuwa kinachoisumbua united ni saratani(cancer) ambao ni wamiliki.

Sasa imeshafikia stage 2 inaelekea stage 3 ambapo itakua ngumu kutibika kama hawa wamiliki wasipo badilika. Yaana unafukuza kocha akiyekua anaijenga timu taratibu huku akiwa na injury prayers wengine wapo afcon bado wachezaji wengi wabovu wasiofit mfumo wake na ufinyu wa kikosi.

Huku akiwa haogopi kusema ukweli wa matatizo ya club. Alafu unarudisha makocha wa nyuma waliofukuzwa kama ole kwamba wamalizie msimu hivi hii ni akili kweli.
 
Huyu ndio mwenyewe sasa kwanza lazima wanae wapate namba πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 

Attachments

  • 20260112_010103.jpg
    262.3 KB · Views: 10
Ndio Fursa nzuri hii Kwa Mwanitesa United, Ni faida kubwa Kwa Man Utd kutolewa FA, sasa hapo wawekeze nguvu zote kwenye Ligi Epl wapambane waingie top4 na kucheza UEFA msimu ujao...
Mashabiki Liverpool na Arsenal wanaombea Man Utd waendelee kupoteana hivihivi hata miaka50πŸ€ͺπŸ˜‹πŸ€“
 
Kuna kipindi pale Arsenal tulikua tunataka Stan Kroenke aachie timu agewe mtu mwingine. Miongoni mwa watu walioitaka Arsenal alikua Dangote na mmiliki wa Spotify.

Kroenke akagoma kuuza. Dangote akarudi kukomaa na viwanda vyake na jamaa wa Spotify akaenda kupambana kuimiliki Barcelona.

Kipindi hicho ilikua Arsenal tunaweza kosa mchezaji kwakua anauzwa 45M au 50M. Arteta ilibidi afanye kazi na aliowakuta, wakina Mustafi, Guendouzi, Ceballos na Odegaard kwa mkopo, Sokratis, Bellerin aliyetoka majeruhi, Xhaka asiyejiamini, Cech n.k.

Kroenke akawa anagoma kutumia pesa akidai kwamba anataka timu ijiendeshe, itumie inachozalisha. Mashabiki tukaona anaongea upuuzi kwakua katika timu yake nyingine anayoimiliki ilikua haijiendeshi kwa mode hii. Kwanini akomae Arsenal tu ndiyo ijiendeshe hivyo?

Mashabiki wakaanza riots.

Tuje kwa United, wana wamiliki ambao ikatokea mchezaji anaongozwa na pesa na siyo ile kutaka kucheza timu fulani pesa hua inatoka. Kwa uzoefu wangu na observation mchezaji ambaye alifocus na pesa aliletwa United bila shida, Pogba, Martial, Fernandes, Amad, Mbeumo, Cunha, Sesko, Dorgu, Onana, Ugarte, Casemiro, Mazraoui, De Ligt, Sancho, Yoro, Heaven, Martinez, Malacia, Van De Beek, Antony, Chido n.k.

Hao ni wachezaji ambao kocha alipoint na wakaletwa. Ronaldo alirudi siyo kwa mapenzi ya kocha ila alirudi baada ya mashabiki wenyewe kuentertain hilo swala online.

Mtu anasema bora aje mmiliki mwarabu, ndiyo atafanya nini cha tofauti kwa anachotakiwa kufanya mmiliki? Kwani Newcastle mnajua inamilikiwa na nani? Wanaspend kama wapumbavu ila wako wapi? Mnahisi mmiliki atasababisha timu ikabe? Atasababisha wachezaji wageane pasi kwa wakati?

Chelsea walimleta Tuchel na alipofika tu alisema anachotaka. Akacheza back three akaondoka na CL, akiwa na wachezaji ambao Lampard alisema hawa na ubingwa ni maji na mafuta.

Amorim amefika United anacheza back three, mtu wa Hayloto Mbulu anasema huyu kocha hajui kitu back three bila wachezaji wa kufit mfumo itakutesa. Na yeye akapita na hilo gap. Kwakua it doesn't matter mchezaji kama una LB huyo ni LWB una RB huyo ni RWB so huwezi sema huna wachezaji wa kufit mfumo.

Mashabiki wa United hawajui mpira, hayo ni maneno ya Pogba, unashuhudia hayo kwa wanavyomhukumu kocha na wamiliki. Peronally kocha mtengeneza nidhamu namhofia kwakua once ukicheza na timu ipo disciplined wewe kuondoka na matokeo haiwezi kua easy.

Na Amorim alikua anafanya hili kwa bidii, sasa kwakua hamjui mpira mnahisi shida ni Amorim, kaondoka. Shida ni mmiliki? How? Mnasema kocha hapewi full authority? Ipi? Ronaldo aliwekwa benchi na kocha hakuhojiwa, a club legend. Bench. Na kocha hakuhojiwa.

Kocha analilia wachezaji aliowatumia Uholanzi, kaletewa. Kisha hawatumii na hajaulizwa. Unanunua starters wa Bayern, PSG na Atalanta na hauwatumii na haulizwi. Wewe mkazi wa Kinyanambo C unataka mmiliki afanye nini sasa?

Umelilia Amorim afukuzwe ili ucheze back four kafukuzwa umecheza back four na umenyooshwa unataka mmiliki aondoke. Kwa ishu ipi sasa?

Safari bado ndefu hadi mjue mlimhitaji Amorim na mlitakiwa mumpe muda awanyooshe hao viazi ambao kaka zao hawaamini kua wanatakiwa kukaa bench wajue kupambana.

Ndugu yangu, ze dudu, anakuambia anaona nafasi pale juu. Kimahesabu Wolves pia anaweza kumaliza ndani ya top four. Arsenal tulihitaji ushindi dhidi ya Brighton ili kuingia international games tukasuluhu. Hatukwenda.

Tulihitaji points 3 kwenye mechi zaidi ya nne ili kwenda CL au Europa na hatukwenda. So mahesabu yasikutie majaribuni ukajipa matarajio makubwa.

Muwe mnatumia akili
 
Sawa mwenye akili ya kumpa timu Fletcher. Halafu usifananishe Newcastle hii na upumbavu. Umeisema timu Bora Newcastle eti unaiuliza Iko wapi ...mbona huisemi na kuulizia Manchester city ..au na wao wnaaburuza mkia ? Haya wenye akili pangeni timu ya kucheza mechi ijayo na Manchester city ...
 
Si umeona ulivyokua miyeyusho umeshindwa kuelewa kwamba point ni kocha siyo mmiliki.

Sasa mlivyotaka Amorim aondoke mlidhani nani angekuja? Zidane? Nagelsmann?

Pia mimi ni Arsenal
 
Reuben was humble guy mazingira yamemhukumu alihitaji miaka mitano ya kufanikiwa Ila Manchester ya Sasa Ina njaa ya kufukanikiwa kila msimu
.

Carrick na ole guna wasipewe timu hakuna kocha mule wanajua kupanga koni tu ..

Kwa EPL kocha wa kuivusha Manchester United Sasa ni tuchel tu
 
Yote kwa yote Amorim alikua ni tapeli 😁
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…