Manara apigwa chini CCM kwa utapeli wa magari

Sumbalawinyo

JF-Expert Member
Sep 22, 2009
1,282
247
KATIBU Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Haji Manara, amejiuzulu wadhifa huo baada ya kuhusishwa na tuhuma za utapeli. Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Kirumbe Ng’enda, jana alilithibitishia gazeti hili kuwa wamekubali barua ya kujiuzulu kwa Manara iliyowasilishwa kwao juzi.

Manara aliyechaguliwa kushika wadhifa huo miaka miwili iliyopita, amekumbwa na kashfa ya kukodisha magari kwa watu mbalimbali yanayofikia 40, na kuyaweka rehani kwa watu mbalimbali Dar es Salaam na mikoa mingine nchini.

Anadaiwa kukodisha magari hayo kutoka katika kampuni tofauti za kukodisha magari nchini akitumia jina la CCM kwamba inayahitaji kwa kazi maalumu. Anadaiwa kuingia makubaliano ya kukodisha magari hayo kwa gharama ya Sh 60,000 kwa siku.

Tayari suala lake liko katika vyombo vya Dola baada ya wenye magari wanaotuhumiwa kutapeliwa na Katibu Mwenezi huyo kuwasilisha malalamiko yao kwa Polisi na sasa suala hilo linashughulikiwa na Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Lakini jana Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, alisema barua ya Manara ya kujiuzulu wadhifa wake imekubaliwa na suala lake linaachwa katika vyombo vya Dola vifanye kazi yake.

“Ni kweli jana (juzi) Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam, ilikutana na mbali na ajenda nyingine, ilikutana kupokea na kujadili barua ya Haji Manara ya kujiuzulu wadhifa wa Katibu Mwenezi.

“Halmashauri Kuu ya Mkoa imekubali uamuzi wake wa kujiuzulu na haikutoa tamko lolote jingine, badala yake imeviachia vyombo vya Dola vifanye kazi yake kwa kuwa suala hilo limefikishwa huko,” alisema Ng’enda alipozungumza na gazeti hili kwa simu jana.

Alisema katika barua yake ya kujiuzulu, Manara amesisitiza kuwa hilo ni suala lake binafsi, na halina uhusiano na chama hicho, na atapata fursa ya kulielezea vizuri katika siku zijazo. Lakini kwa mujibu wa Ng’enda, Manara amewaomba radhi wana-CCM wenzake, viongozi na wakereketwa wa chama hicho kutokana na namna suala hilo lilivyowasononesha, na kwamba amejiuzulu ili kukisafisha chama na kashfa hiyo.

Katibu wa CCM Mkoa alisema kikao cha juzi chini ya Mwenyekiti wao, John Guninita hakikuwa na pingamizi na uamuzi wa Manara kwa sababu suala hilo linazungumzika. Kuhusu kama CCM ilikuwa na taarifa za utapeli unaodaiwa kufanywa na kiongozi wake, Ng’enda alisema mmoja wa walalamikaji alifikisha suala hilo kwao na baada ya kuoneshwa nyaraka zilizokuwa na nembo za CCM, lakini zikagundulika ni za kughushi, walimshauri aende katika vyombo vya Dola.

“Sisi ndio tuliomshauri aende katika vyombo vya Dola baada ya kumueleza kuwa CCM haihusiki na suala hilo na hata nembo zilizotumika, zimeonekana ni za kughushi.

Kwa hiyo, hatukuficha kitu na ndio maana tulimpa ushirikiano mhusika kwa sababu sisi sio chama cha kuficha madhambi,” alisema.

Aidha, alisema kwa ujumla CCM ni chama cha binadamu, na akafananisha na familia inayoweza kuzaa watoto ambao miongoni mwao wakawemo mchungaji, shehe au mwizi; kwa hiyo, lililomkuta Manara linaangukia humo, ingawa alisisitiza, ni Mahakama pekee inayoweza kusema kada huyo ni mkosaji.

“Haya yanatokea kwa sababu chama ni cha binadamu, sisi kama taasisi tuna watu wa aina mbalimbali, lakini la msingi ni kuzingatia maadili na miiko ya uongozi, na huo ndio mwito wetu kwa wana-CCM wengine.

Tuzingatie maadili ya uongozi,” alisema Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam. Manara hakupatikana jana kuzungumzia hatima yake baada ya kujiuzulu, lakini kijana huyo machachari alieleza wiki iliyopita anapanga kulizungumzia atakapozungumza na wanahabari.
 
we have our laws, saying sorry and resigning should not be taken as a punishment, he need to face the full wrath of the law to be as a lesson to all who abuse their political, economic etc status!
 
KATIBU Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Haji Manara, amejiuzulu wadhifa huo baada ya kuhusishwa na tuhuma za utapeli. Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Kirumbe Ngenda, jana alilithibitishia gazeti hili kuwa wamekubali barua ya kujiuzulu kwa Manara iliyowasilishwa kwao juzi.

Manara aliyechaguliwa kushika wadhifa huo miaka miwili iliyopita, amekumbwa na kashfa ya kukodisha magari kwa watu mbalimbali yanayofikia 40, na kuyaweka rehani kwa watu mbalimbali Dar es Salaam na mikoa mingine nchini.

Anadaiwa kukodisha magari hayo kutoka katika kampuni tofauti za kukodisha magari nchini akitumia jina la CCM kwamba inayahitaji kwa kazi maalumu. Anadaiwa kuingia makubaliano ya kukodisha magari hayo kwa gharama ya Sh 60,000 kwa siku.

Tayari suala lake liko katika vyombo vya Dola baada ya wenye magari wanaotuhumiwa kutapeliwa na Katibu Mwenezi huyo kuwasilisha malalamiko yao kwa Polisi na sasa suala hilo linashughulikiwa na Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.

Lakini jana Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, alisema barua ya Manara ya kujiuzulu wadhifa wake imekubaliwa na suala lake linaachwa katika vyombo vya Dola vifanye kazi yake.

Ni kweli jana (juzi) Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam, ilikutana na mbali na ajenda nyingine, ilikutana kupokea na kujadili barua ya Haji Manara ya kujiuzulu wadhifa wa Katibu Mwenezi.

Halmashauri Kuu ya Mkoa imekubali uamuzi wake wa kujiuzulu na haikutoa tamko lolote jingine, badala yake imeviachia vyombo vya Dola vifanye kazi yake kwa kuwa suala hilo limefikishwa huko, alisema Ngenda alipozungumza na gazeti hili kwa simu jana.

Alisema katika barua yake ya kujiuzulu, Manara amesisitiza kuwa hilo ni suala lake binafsi, na halina uhusiano na chama hicho, na atapata fursa ya kulielezea vizuri katika siku zijazo. Lakini kwa mujibu wa Ngenda, Manara amewaomba radhi wana-CCM wenzake, viongozi na wakereketwa wa chama hicho kutokana na namna suala hilo lilivyowasononesha, na kwamba amejiuzulu ili kukisafisha chama na kashfa hiyo.

Katibu wa CCM Mkoa alisema kikao cha juzi chini ya Mwenyekiti wao, John Guninita hakikuwa na pingamizi na uamuzi wa Manara kwa sababu suala hilo linazungumzika. Kuhusu kama CCM ilikuwa na taarifa za utapeli unaodaiwa kufanywa na kiongozi wake, Ngenda alisema mmoja wa walalamikaji alifikisha suala hilo kwao na baada ya kuoneshwa nyaraka zilizokuwa na nembo za CCM, lakini zikagundulika ni za kughushi, walimshauri aende katika vyombo vya Dola.

Sisi ndio tuliomshauri aende katika vyombo vya Dola baada ya kumueleza kuwa CCM haihusiki na suala hilo na hata nembo zilizotumika, zimeonekana ni za kughushi.

Kwa hiyo, hatukuficha kitu na ndio maana tulimpa ushirikiano mhusika kwa sababu sisi sio chama cha kuficha madhambi, alisema.

Aidha, alisema kwa ujumla CCM ni chama cha binadamu, na akafananisha na familia inayoweza kuzaa watoto ambao miongoni mwao wakawemo mchungaji, shehe au mwizi; kwa hiyo, lililomkuta Manara linaangukia humo, ingawa alisisitiza, ni Mahakama pekee inayoweza kusema kada huyo ni mkosaji.

Haya yanatokea kwa sababu chama ni cha binadamu, sisi kama taasisi tuna watu wa aina mbalimbali, lakini la msingi ni kuzingatia maadili na miiko ya uongozi, na huo ndio mwito wetu kwa wana-CCM wengine.

Tuzingatie maadili ya uongozi, alisema Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam. Manara hakupatikana jana kuzungumzia hatima yake baada ya kujiuzulu, lakini kijana huyo machachari alieleza wiki iliyopita anapanga kulizungumzia atakapozungumza na wanahabari.
Manyara may be street smart but he is not street wise
 
Back
Top Bottom