Justine Marack
JF-Expert Member
- Jul 31, 2014
- 567
- 1,551
Ni kumbukumbu ya kilichotokea mwaka 2022 baada ya sakata la Makonda na GSM.
Ajabu ni pale ambapo Haji Manara bila kueleweka alikotokea, aliamua kuingilia ugomvi usio muhusu. Alimuanika Makonda mchana kweupe na kumdhalilisha vibaya mno.
Ni baada ya Makonda kuweka wazi hofu yake juu ya usalama wa uhai wake.
Ndipo Manara, ambaye sio familia ya GSM na wala hana share yoyote, akaibuka na kusema, "Makonda kwenda zako wewe, nani akuue wewe. Rudi kwenu Kolomije ukavue dagaa," haya pamoja na dhihaka nyingi. Manara alidhamilia kumdhalilisha Makonda, ilionesha kuwa anachuki naye sana na alikuwa anatafuta upendo wa kutapikia nyongo yake.
Hiki kilikuwa kipindi ambacho watu wengi walimkimbia bwana Makonda. Hata rafiki yake na Chawa namba moja, Lemutuz Mobimba, alikuwa tayari amemkimbia na kumuanika vibaya.
Naamini hata yeye angekua hai leo tungemkumbusha.
Manara kwa siku za karibu amekuwa na mikosi sana, baada ya kukimbiwa na wanawake zake na kufungiwa na mamlaka za mpira. Siku chache zilizopita aliibuka kulialia kama mtoto huku akitaka watu wamhurumie.
Uzi huu ni maalum kumfahamisha kuwa Ndugu Paul Makonda sasa amefika Kolomije.
Ajabu ni pale ambapo Haji Manara bila kueleweka alikotokea, aliamua kuingilia ugomvi usio muhusu. Alimuanika Makonda mchana kweupe na kumdhalilisha vibaya mno.
Ni baada ya Makonda kuweka wazi hofu yake juu ya usalama wa uhai wake.
Ndipo Manara, ambaye sio familia ya GSM na wala hana share yoyote, akaibuka na kusema, "Makonda kwenda zako wewe, nani akuue wewe. Rudi kwenu Kolomije ukavue dagaa," haya pamoja na dhihaka nyingi. Manara alidhamilia kumdhalilisha Makonda, ilionesha kuwa anachuki naye sana na alikuwa anatafuta upendo wa kutapikia nyongo yake.
Hiki kilikuwa kipindi ambacho watu wengi walimkimbia bwana Makonda. Hata rafiki yake na Chawa namba moja, Lemutuz Mobimba, alikuwa tayari amemkimbia na kumuanika vibaya.
Naamini hata yeye angekua hai leo tungemkumbusha.
Manara kwa siku za karibu amekuwa na mikosi sana, baada ya kukimbiwa na wanawake zake na kufungiwa na mamlaka za mpira. Siku chache zilizopita aliibuka kulialia kama mtoto huku akitaka watu wamhurumie.
Uzi huu ni maalum kumfahamisha kuwa Ndugu Paul Makonda sasa amefika Kolomije.