Mahmood
JF-Expert Member
- Feb 9, 2008
- 7,908
- 2,478
Yesu ni Mtume wa Mungu.Mahmood
Hapo ndio tunapotofautiana kaka. Sisi hatuamini katika Yale ninyi mnayoyaamini!
Tunataratibu zetu, Mungu wetu ni wa utatu mtakatifu, Je ninyi mnalikubali hili? Lah!
Kamwe narudia kamwe huwezi kutumia Quran katika kujustfy NENO.lolote katika Biblia. Tunaamini katika kusamehe ninyi katika kulipiza ni haki!
Hakuna uhusiano wa kiimani Kati yetu kwa MTU aliyeshika sawasawa imani yake. Huwezi Mueleza Muislam swafi Kuwa anaamini katika imani ya kikristo! Never! Na hivyo hivyo kwa wakristo!
Ila ni sisi ambao labda tunakaeli dunia tunajaribu kujenga upatanisho ktk dini mbili hizi. Uislam Na Ukristo ni vitu viwili tofauti. ni sawa dunia Na.mbinguni, nyeusi Na nyeusi! kamwe si kitu kimoja!
Tuendelee kuheshimiana kwa "imani" maana kila kitu anachoamini MTU ktk imani yake ni sawa, hatuna haja ya kutofautiana Na kulazimishana Kuwa dini flani ni Bora zaidi ya nyingine.
Shika sana ulichonacho Mkuu, usiruhusu MTU kukutoa ktk imani yako. Lakini kama utajitafutia maarifa Na ukagungua kwa hiari yako Kuwa upo katika wrong tracks using'ang'ania kubaki ulipo. HAMA. Hiii ni kwa wote. sio kwa wakristo au waislam tu!
Yesu kasema wazi kabisa kwamba yeye ni mtu na katumwa na Mungu.
Katika Injili ya (Yohana 8:40), Yesu kasema, "Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu..."
Yesu anasema wazi kabisa" mnatafuta kuniua mimi mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu."
Hapo Yesu anajitambulisha kwamba yeye ni mtu katumwa na Mungu.
Kuiacha dhana ya Mungu mwenye mwili na Utatu hakumwaibishi Yesu, ispokuwa kunamuweka Mungu katika utukufu, upweke,
ukuu na nafasi ya pekee isiyo na mfano ya kuwa yeye ni Mungu wa pekee anayestahiki kuabudiwa.
Yesu si Mungu, ila ni Mtume na Mjumbe `mkuu wa Mungu!
Yesu anasema;
Katika Yohana 20:17
"Mungu wangu naye ni Mungu wenu".
Yafaa hapa ujiulize sana, Yesu alikusudia nini aliposema: "Mungu wangu naye ni Mungu wenu"?
Jiulize je inawezekana kwa kiumbe kumzidi ukuu Mungu wake?
Pia katika John 5:30
Yesu kasema;
" Mimi siwezi kufanya kitu kwa uwezo wangu mwenyewe. Mimi nina hukumu kama ninavyosikia kutoka kwa Mungu, nayo hukumu yangu ni ya haki. Nia yangu si kufanya nipendavyo mwenyewe, bali apendavyo yule aliyenituma."
Tafakarini ndugu zanguni kwa Adam, before it is too late.
Mwenyezi Mungu anasema katika Quran (3-59-91):
"Hakika mfano wa Yesu kwa Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam; alimuumba kwa udongo kisha akamwambia: Kuwa! Basi akawa.
Hii ni kweli itokayo kwa Mola wako Mlezi. Basi usiwe miongoni mwa wanao fanya shaka.
Watakao kuhoji katika haya baada ya kukufikilia ilimu hii waambie: Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu, na wake zetu na wake zenu, na sisi wenyewe na nyinyi wenyewe, kisha tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo.
Hakika haya ndiyo maelezo ya kweli. Na hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu tu, na hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye nguvu na Mwenye hikima.
Na kama wakigeuka basi Mwenyezi Mungu anawajua waharibifu.
Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa miungu badala ya Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka basi semeni: Shuhudieni ya kwamba sisi ni Waislamu.
Enyi Watu wa Kitabu! Mbona mnabishana juu ya Ibrahim, na hali Taurati na Injili hazikuteremshwa ila baada yake? Basi hamzingatii?
Angalieni! Nyinyi mlibishana katika yale mliyo yajua. Mbona sasa mnabishana katika yale msiyo yajua? Na Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye, na nyinyi hamjui.
Ibrahim hakuwa Yahudi wala Mkristo, lakini alikuwa mwongofu Muislamu, wala hakuwa katika washirikina.
Watu wanao mkaribia zaidi Ibrahim ni wale walio mfuata yeye na Nabii huyu na walio amini. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wa Waumini.
Kipo kikundi katika Watu wa Kitabu wanao penda kukupotezeni; lakini hawapotezi ila nafsi zao, nao wenyewe hawatambui.
Enyi Watu wa Kitabu! Mbona mnazikataa Ishara za Mwenyezi Mungu ilhali nyinyi mnashuhudia?
Enyi Watu wa Kitabu! Mbona kweli mnaivisha uwongo, na kweli mnaificha na hali mnajua?
Na kikundi katika Watu wa Kitabu walisema: Yaaminini yale waliyo teremshiwa wenye kuamini mwanzo wa mchana, na yakataeni mwisho wake; huenda wakarejea.
Wala msimuamini ila anaye fuata dini yenu. Sema: Hakika uwongofu ni uwongofu wa Mwenyezi Mungu, kuwa apewe mtu mfano wa mlio pewa nyinyi au wakuhojini mbele ya Mola wenu Mlezi. Sema: Hakika fadhila zimo mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Humpa amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa na Mjuzi.
Yeye humchagua kumpa rehema zake amtakaye; na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye fadhila kubwa.
Na miongoni mwa Watu wa Kitabu yupo ambaye ukimpa amana ya mrundi wa mali atakurudishia, na miongoni mwao yupo ambaye ukimpa amana ya dinari moja hakurudishii isipo kuwa ukimsimamia kumdai. Haya ni kwa kuwa wakisema: Hatuna lawama kwa ajili ya hawa wasio jua kusoma. Na wanamzulia uwongo Mwenyezi Mungu, hali nao wanajua.
Sivyo hivyo, bali anaye timiza ahadi yake na akamchamngu basi Mwenyezi Mungu huwapenda wachamngu.
Hakika wanao uza ahadi ya Mwenyezi Mungu na viapo vyao thamani ndogo, hao hawatakuwa na sehemu ya kheri yoyote katika Akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama Siku ya Kiyama, wala hatawatakasa, nao watapata adhabu chungu.
Na wapo baadhi yao wanao pindua ndimi zao katika kusoma Kitabu ili mdhanie kuwa hayo yanatoka Kitabuni, na wala hayatoki Kitabuni. Na husema: Haya yametoka kwa Mwenyezi Mungu. Na wala hayatoki kwa Mwenyezi Mungu. Na wanamsingizia Mwenyezi Mungu uwongo na wao wanajua.
Haiwezi kuwa mtu aliye pewa na Mwenyezi Mungu Kitabu na hikima na Unabii kisha awaambie watu: Kuweni wa kuniabudu mimi badala ya Mwenyezi Mungu. Bali atawaambia: Kuweni wenye kumuabudu Mola Mlezi wa viumbe vyote, kwa kuwa nyinyi mnafundisha Kitabu na kwa kuwa mnakisoma.
Wala hatakuamrisheni kuwafanya Malaika na Manabii kuwa ni miungu. Je, atakuamrisheni ukafiri baada ya kuwa nyinyi Waislamu?
Na pale Mwenyezi Mungu alipo chukua ahadi kwa Manabii: Nikisha kupeni Kitabu na hikima, kisha akakujieni Mtume mwenye kusadikisha mliyo nayo, ni juu yenu mumuamini na mumsaidie. Akasema: Je, mmekiri na mmekubali kushika agizo langu juu ya hayo? Wakasema: Tumekubali. Akasema: Basi shuhudieni, na Mimi ni pamoja nanyi katika kushuhudia.
Watakao geuka baada ya haya basi hao ndio wapotovu.
Je, wanataka dini isiyo kuwa ya Mwenyezi Mungu, na hali kila kilichomo mbinguni na katika ardhi kimesilimu kwa kumt'ii Yeye kikipenda kisipende, na kwake Yeye watarejeshwa?
Sema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu, na tuliyo teremshiwa sisi, na aliyo teremshiwa Ibrahim, na Ismail, na Is-haak na Yaakub na wajukuu zao, na aliyo pewa Musa na Yesu na Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi. Hatubagui baina yao hata mmoja, na sisi ni wenye kusilimu kwake.
Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasiri.
Mwenyezi Mungu atawaongoaje watu walio kufuru baada ya kuamini kwao, na wakashuhudia ya kuwa Mtume huyu ni wa haki, na zikawafikia hoja zilizo wazi? Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhaalimu.
Hao malipo yao ni kuwa ipo juu yao laana ya Mwenyezi Mungu na ya Malaika na ya watu
Humo watadumu. Hawatapunguziwa adhabu wala hawatapewa nafasi.
Isipo kuwa wale walio tubu baada ya hayo na wakatengenea; kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu.
Hakika wale walio kufuru baada ya kuamini kwao, kisha wakazidi kukufuru, toba yao haitakubaliwa, na hao ndio walio potea.
Hakika wale walio kufuru, na wakafa hali ni makafiri haitakubaliwa kutoka kwa yeyote wao fidia ya dhahabu ya kujaza dunia nzima lau wangeli itoa. Hao watapata adhabu chungu, wala hawatakuwa na wa kuwanusuru.