Kiranja Mkuu
JF-Expert Member
- Feb 18, 2010
- 4,066
- 4,085
Mimi naabudu kwenye lile kanisa.
Pale panapofanyika miujiza ishara na maajabu ya kila namna.
Mwingine nae anaabudu pale pengine, tunapoambiwa wanaabudu miungu mingine.
Je kweli sisi tunaabudu kwa namna ambavyo mungu wetu anataka tumuabudu?
Mchungaji wengu ni mbaguzi, anawaweka mbele ya madhabahu walio matajiri na sisi massikini tunaambulia siti za nyuma na wakati mwingine kusimama.
Haturuhusiwi kuvigusa wala kuvikaribia viti vya mbele vinavyokaliwa na wenye nazo.
Mchungaji mwingine ni mbishi, hatii mamlaka iliyopo madarakani, anashupalia miundo mbinu isipite jirani na kanisa lake.
Anawatesa watu kwa kuwafanya wakeshe usiku na mchana kwa miezi miwili mfululizo huku wakipigwa na mvua, jua, upepo, vumbi , mioshi ya magari na dhoruba zote.
Mchungaji mwingine kazui yake ni kuponda tu huduma za watu wengine na kusema kwamba ishara na miujiza ya kwake peke yake ndio iliyotoka mbinguni.
Mwingine ana skendo ya kuua mtu arusha na sasa amehamia dar es salaam baada ya soko kumuendea kombo.
jamani hivi hawa sio manabii wa uongo?
mbona matendo yao yanatutia mashaka?
ona walivyo matajiri , wamejilimbikizia mali, hawana upendo hata kidogo kwa waumini wao.
wanawanyonya wenzao.
siku za mwisho watu watakuwa ni wenye kupenda mali na upendo wa kweli utapoa.
naomba tuendelee kuyachunguza matendo ya waheshimiwa wetu huku tukiyalinganisha na maagizo aliyotuachia bwana wetu yesu kristo.
inatubidi tubadilishe namna za ibada zetu na tuanze kumuabudu mungu katika roho nakweli, badala ya kuwa tunasema kuwa naabudu kanisa lile.
mungu anawataka wamuuabudio halisi.
wale wanaomuabudu katika roho na kweli.
Pale panapofanyika miujiza ishara na maajabu ya kila namna.
Mwingine nae anaabudu pale pengine, tunapoambiwa wanaabudu miungu mingine.
Je kweli sisi tunaabudu kwa namna ambavyo mungu wetu anataka tumuabudu?
Mchungaji wengu ni mbaguzi, anawaweka mbele ya madhabahu walio matajiri na sisi massikini tunaambulia siti za nyuma na wakati mwingine kusimama.
Haturuhusiwi kuvigusa wala kuvikaribia viti vya mbele vinavyokaliwa na wenye nazo.
Mchungaji mwingine ni mbishi, hatii mamlaka iliyopo madarakani, anashupalia miundo mbinu isipite jirani na kanisa lake.
Anawatesa watu kwa kuwafanya wakeshe usiku na mchana kwa miezi miwili mfululizo huku wakipigwa na mvua, jua, upepo, vumbi , mioshi ya magari na dhoruba zote.
Mchungaji mwingine kazui yake ni kuponda tu huduma za watu wengine na kusema kwamba ishara na miujiza ya kwake peke yake ndio iliyotoka mbinguni.
Mwingine ana skendo ya kuua mtu arusha na sasa amehamia dar es salaam baada ya soko kumuendea kombo.
jamani hivi hawa sio manabii wa uongo?
mbona matendo yao yanatutia mashaka?
ona walivyo matajiri , wamejilimbikizia mali, hawana upendo hata kidogo kwa waumini wao.
wanawanyonya wenzao.
siku za mwisho watu watakuwa ni wenye kupenda mali na upendo wa kweli utapoa.
naomba tuendelee kuyachunguza matendo ya waheshimiwa wetu huku tukiyalinganisha na maagizo aliyotuachia bwana wetu yesu kristo.
inatubidi tubadilishe namna za ibada zetu na tuanze kumuabudu mungu katika roho nakweli, badala ya kuwa tunasema kuwa naabudu kanisa lile.
mungu anawataka wamuuabudio halisi.
wale wanaomuabudu katika roho na kweli.