Mamlaka husika zinawaza nini kuhusu Stendi ya Mbagala Rangi Tatu? Ni kero kipindi cha mvua

Mamlaka husika zinawaza nini kuhusu Stendi ya Mbagala Rangi Tatu? Ni kero kipindi cha mvua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
654
Reaction score
1,598
Hali ni mbaya kwenye stendi hiyo yenye daladala na ofisi za mabasi yanayoenda mikoani hasa mikoa ya kusini, abiria tunaofika kwenye stendi hiyo tunakumbana na kero kubwa, daladala na mabasi kuna wakati yanapata shida ya kupita kutokana na tope.

Lakini inashangaza kwa miaka yote Watu wa daladala na mabasi wanatozwa tozo lakini stendi imejaa tope, mashimo kila kona kama vile haina wasimamizi.

Kutokana na hali hiyo Wito wangu kwa mamlaka zinazosimamia stendi hiyo zitenge fungu la kufanya uboreshaji wa stendi hiyo hata wa muda mfupi endapo kutakuwa na mpango mwingine wa kujenga stendi mpya yenye ubora zaidi ili kuepusha kero iliyopo sasa.



photo_2025-05-23_13-48-31.jpg

photo_2025-05-23_13-48-27.jpg

photo_2025-05-23_13-47-44.jpg
 
Sio hapo tuu kila mahali(Segerea, kawe, Makumbusho(hii ina mabonde mabonde)tegeta, n.k)na barabara muhimu ni kero sana Dar.
Barabara ni mashimo mashimo tupu.

Sijui wanaposifia serikali huwa wanaishi dunia ipi yan maana sio kwa kero hizi tunazoziona
 
Hali ni mbaya kwenye stendi hiyo yenye daladala na ofisi za mabasi yanayoenda mikoani hasa mikoa ya kusini, abiria tunaofika kwenye stendi hiyo tunakumbana na kero kubwa, daladala na mabasi kuna wakati yanapata shida ya kupita kutokana na tope.

Lakini inashangaza kwa miaka yote Watu wa daladala na mabasi wanatozwa tozo lakini stendi imejaa tope, mashimo kila kona kama vile haina wasimamizi.

Kutokana na hali hiyo Wito wangu kwa mamlaka zinazosimamia stendi hiyo zitenge fungu la kufanya uboreshaji wa stendi hiyo hata wa muda mfupi endapo kutakuwa na mpango mwingine wa kujenga stendi mpya yenye ubora zaidi ili kuepusha kero iliyopo sasa.

Hii hali ipo tanzania nzima
 
Hali ni mbaya kwenye stendi hiyo yenye daladala na ofisi za mabasi yanayoenda mikoani hasa mikoa ya kusini, abiria tunaofika kwenye stendi hiyo tunakumbana na kero kubwa, daladala na mabasi kuna wakati yanapata shida ya kupita kutokana na tope.

Lakini inashangaza kwa miaka yote Watu wa daladala na mabasi wanatozwa tozo lakini stendi imejaa tope, mashimo kila kona kama vile haina wasimamizi.

Kutokana na hali hiyo Wito wangu kwa mamlaka zinazosimamia stendi hiyo zitenge fungu la kufanya uboreshaji wa stendi hiyo hata wa muda mfupi endapo kutakuwa na mpango mwingine wa kujenga stendi mpya yenye ubora zaidi ili kuepusha kero iliyopo sasa.

Ingekuwa Masaki hii Kero ingeshughulikiwa chap kwa haraka ila kwasababu ni Mbagara huko msubiri uchaguzi
 
Hiyo stendi haimilikiwi na serikali bali mtu binafsi
 
Back
Top Bottom