Mambosasa: Tumempuuza Mwamakula na kumuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana

Walishajua kuwa huyu hana kpsa wakaona ngoja tukampekue nyumban kwake labda tunaweza mkuta na kosa wakakuta hamna kitu yaan mimi niwashaur tu achane SIASA alieshika mpin hajui siasa
 
Ndiyo maana alisema ni matembezi ya hiari ya kila kundi lisilozidi watu 20. Wewe unafikiri Askofu ni mjinga kama wanaCCM (TWAWEZA)?
Hao watu 20 si tayari mkusanyiko, na yakiwepo makundi makundi 100 ya watu 20 , ni watu 2000 hao, punguza mahaba kamanda.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemuachia kwa dhamana Askofu Emmaus Mwamakula wa kanisa la Uamsho la Moravian baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwake.

Taarifa za kushikiliwa Mwamakula zilitolewa na polisi jana Jumatatu Februari 15, 2021 kupitia mtandao wa kijamiii kabla ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuthibitisha kumshikilia.

Akizungumza leo Jumanne Februari 16,2021 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema baada ya jeshi hilo kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake limemuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

“Tumempuuza na baada ya kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake, mchana huu tumemuachia kwa dhamana baada ya kutimiza masharti,” amesema.

Awali polisi walieleza kumshikilia kumshikilia Mwamakula kutokana na taarifa aliyoichapisha mtandaoni iliyokuwa ikihamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi kuandamana kushinikiza kudai katiba mpya jambo ambalo ni kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Mwananchi
Mambosasa anachoweza ni kuvaa magwanda yenye nyota na kuita waandishi wa habari basi, ila kinachotoka kinywani mwake ambacho ni wakilisho la kilichomo kichwani mwake ni sifuri. Sijawahi kumwelewa huyu eti Kamanda
 
Anachoweza Mambosasa sana sana ni kwenda kunywa chai ya Mo baada ya kupatikana toka mateka
 
Mkuu hbari za mitandaoni huoni kama zina ukubwa wake nin??
Polisi huwa hawafanyii kazi habari za mitandaoni ,Rejea lissu alivyotoa malamiko ya kufatiliwa na wasiojulikana kabla hajapigwa risasi kupitia mitandao ya kijamii na polisi wakasema kwamba lissu hajawahi kuripoti kituo chochote na huwa hawanyii kazi taarifa za mitandao ya kijamii.
 
Hao watu 20 si tayari mkusanyiko, na yakiwepo makundi makundi 100 ya watu 20 , ni watu 2000 hao, punguza mahaba kamanda.
Watu 20 waliotengana hatua 2 wanatengeneza hatari ya maambukizi ya corona? Wewe unapingana na wataalam wa afya?
 
Polisi huwa hawafanyii kazi habari za mitandaoni ,Rejea lissu alivyotoa malamiko ya kufatiliwa na wasiojulikana kabla hajapigwa risasi kupitia mitandao ya kijamii na polisi wakasema kwamba lissu hajawahi kuripoti kituo chochote na huwa hawanyii kazi taarifa za mitandao ya kijamii.
Polisi wetu wenhi wamebakiza akili za kuvalia suluali na kofia. Zaidi ya hapo, hawana kitu kichwani.
 
Huyo askofu uchwara kaamua kutumia hii njia ili kujiongezea umaarufu kanisani kwake ili kapu lijae

Pongezi kwa jeshi la polisi kumshughulikia na kumpuuza
katiba anayoitaka ni kwa ajili ya manufaa na ustawi wako na kizazi kijacho, lkn kama una akili za kunguni kamwe huwezi kuona namna anavyojitoa kwa ajili ya hayo. Kungekuwepo na duka la kununua akili ningekushauri uende ukanunue lkn ndio hivyo, ujinga utakuandama hadi kiama.
 
Labda nianze na wewe miss zomboko,wewe unamuamini Mambosasa?Mimi toka aseme MO alitekwa na wazungu wawili na kesi imeishia hewani,mimi simuamini hata akisema jambo la kweli!
 
IMG_0966.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemuachia kwa dhamana Askofu Emmaus Mwamakula wa kanisa la Uamsho la Moravian baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwake.

Taarifa za kushikiliwa Mwamakula zilitolewa na polisi jana Jumatatu Februari 15, 2021 kupitia mtandao wa kijamiii kabla ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuthibitisha kumshikilia.

Akizungumza leo Jumanne Februari 16,2021 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema baada ya jeshi hilo kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake limemuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

“Tumempuuza na baada ya kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake, mchana huu tumemuachia kwa dhamana baada ya kutimiza masharti,” amesema.

Awali polisi walieleza kumshikilia kumshikilia Mwamakula kutokana na taarifa aliyoichapisha mtandaoni iliyokuwa ikihamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi kuandamana kushinikiza kudai katiba mpya jambo ambalo ni kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Mwananchi
Mkuu Mambosasa , ccm uliyoitumikia miaka yote imekubali Katiba Mpya
 
Back
Top Bottom