Mambo ya kuzingatia kabla hujasoma Biblia

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,596
15,393
1: Biblia sio kitabu cha kidini Sio kitabu cha kubishania, Ni maelezo ya Mungu mfalme aliyeumba sio tu dunia bali trillions za sayari zenye viumbe wasiohesabika. Hiyo lazima uyasome kwa adabu.

2: Usiende na ajenda yako mfukoni. Nenda kama mualikwa wa ikulu ya mbinguni kusikiliza hotuba na maelekezo ya mfalme wa wafalme. Hivyo sio kitabu cha wayahudi au wakristo ni cha kila mwanadamu.

3: Anza kwa maombi ili yeye aliyeandika akufunulie mistari itakayokusaidia wewe binafsi.

4: Maneno ya maandiko ni kama vifurushi vya nguvu, au kama zile namba za vocha ukiyaingiza moyoni yanabadilika kuwa nguvu au ujazo unaoleta athali chanya kwenye kila eneo la maisha yako. Soma ukiwa na mtazamo wa kupokea nguvu sio maelezo.

5: Amini kila neno aliloambiwa mtu yeyete katika biblia umeambiwa na wewe. Kila baraka zilizotamkwa ni zako pia. Kabla hujaanza kusoma biblia anza kujiepusha na watu wanaoiponda, mijadala isiyojengefu, watu wanaopenda mizaha na utani hata kama ni watumishi. Hii itakusaidia kuongeza umakini na kuwa na adabu kwa kauli za Mungu.

Ni hayo tu.

Kama umejifunza kitu, usisahau kucomment chochote.
 
5: "Amini kila neno aliloambiwa mtu yeyete katika biblia umeambiwa na wewe."



Sio kweli mkuu, kuna vitu ukisoma unaona kabisa hapa hapanihusu
Kwa maana nyingine kuna kitu cha kujifunza. Maana yameandikwa ili kutufundisha sisi.

Ndio maana Ibrahim alizini kwa kukoswa uvumilivu. Sisi tunajifunza kuvumilia maana Mungu sio muongo.

Kikubwa kujua application. Maana kila lilioandikwa linaaplication yake kwa kila mtu.
 
Kwa maana nyingine kuna kitu cha kujifunza. Maana yameandikwa ili kutufundisha sisi.

Ndio maana Ibrahim alizini kwa kukoswa uvumilivu. Sisi tunajifunza kuvumilia maana Mungu sio muongo.

Kikubwa kujua application. Maana kila lilioandikwa linaaplication yake kwa kila mtu.
Kitabu kinaeleza kabisa kwamba ni "Waraka wa kwanza kwa Timotheo"

Utasemaje umeandikiwa wewe?
 
Kitabu kinaeleza kabisa kwamba ni "Waraka wa kwanza kwa Timotheo"

Utasemaje umeandikiwa wewe?
Hakuandikiwa timotheo kama mtu binafsi. Timotheo alikuwa kiongozi wa kanisa, yeye alikuwa ni link na watu. Hayo ni maelekezo ambayo sio kwa ajili yake tu bali wote.
Ndio maana anaelezea hadi dalili za siku za mwisho. Waraka wa pili kwa Timotheo 3. Wakati hayo maneno hayamuhusu maana ameshakufa sasa.

Hizo ni hekima za juu sana ambazo Mungu ameamua kutumia kutufikishia ujumbe kwa njia nyingi. Ndio maana kumejaa unabii, nyaraka, mithali, mashairi, nyimbo, hadithi, mafumbo, sitiari, tashtiti, na kila namna ya uandishi ambao utagonga kila angle ya ubongo kuamsha ufahamu
 
Kitabu ambacho kilishindwa hata kuelezea umbo halisi la dunia cha kazi gani sasa.

Wakatoliki wakaamua kumuua mwanasayansi wa watu bure kisa tu alisema dunia ina umbo la tufe...
Galileo Galilei aliongozwa na Biblia kuchunguza anga na kugundua dunia ni duara. Kwanza katika kitabu cha Isaya kuna mstari unazunguzmia uduara wa dunia.

Wakatoliki dini yao ilikuwa chini ya influence kubwa ya greek mythology sio Biblia. Nadharia za misiolojia za kigiriki zilikuwa backbone ya upinzani wao kwa Galilei. Maana ilionekana anabishana na wasomi ambao kanisa liliwaamini.

Ila alishaombwa msamaha na wakatoliki miaka ya 90 kuwa walikosea kumuhukumu msomi Galileo.
 
Unaposema biblia ni maneno ya Mungu, huo uhakika unaupata wapi?

Ulimuona Mungu kaka anaandika hiyo biblia, au Mungu alishawahi kusema hayo ni maneno yake?
Mungu ananjia nyingi za kufikia watu hasa wa dunia hii yenye iq ndogo kabisa iliyodunishwa na dhambi. Alitumia watu kuwapa ujumbe kwa lugha ya kawaida kabisa ili tuelewe.
Tusimpangie Mungu eti kila kitu aje aseme moja kwa moja. Tumuache atumie hekima zake kutusaidia.
 
1: Biblia sio kitabu cha kidini Sio kitabu cha kubishania, Ni maelezo ya Mungu mfalme aliyeumba sio tu dunia bali trillions za sayari zenye viumbe wasiohesabika. Hiyo lazima uyasome kwa adabu.

2: Usiende na ajenda yako mfukoni. Nenda kama mualikwa wa ikulu ya mbinguni kusikiliza hotuba na maelekezo ya mfalme wa wafalme. Hivyo sio kitabu cha wayahudi au wakristo ni cha kila mwanadamu.

3: Anza kwa maombi ili yeye aliyeandika akufunulie mistari itakayokusaidia wewe binafsi.

4: Maneno ya maandiko ni kama vifurushi vya nguvu, au kama zile namba za vocha ukiyaingiza moyoni yanabadilika kuwa nguvu au ujazo unaoleta athali chanya kwenye kila eneo la maisha yako. Soma ukiwa na mtazamo wa kupokea nguvu sio maelezo.

5: Amini kila neno aliloambiwa mtu yeyete katika biblia umeambiwa na wewe. Kila baraka zilizotamkwa ni zako pia. Kabla hujaanza kusoma biblia anza kujiepusha na watu wanaoiponda, mijadala isiyojengefu, watu wanaopenda mizaha na utani hata kama ni watumishi. Hii itakusaidia kuongeza umakini na kuwa na adabu kwa kauli za Mungu.

Ni hayo tu.

Kama umejifunza kitu, usisahau kucomment chochote.

Mkuu ni mara nyingi naona unapost kuhusu biblia na mambo yahusuyo injili, inawezekana unatamani sana kufikisha habari njema kwa watu kama ilivyo amriwa kwa wakristo especially ukisoma marko 16:15-18.

Maoni yangu kwako ni kuwa, tafuta kujieleimisha sana kuhusu neno kabla hujaenda kujaribu kuelimisha wengine vinginevyo utawapa sababu zaidi watu wasipokee habari za ufalme kwa kuwa uko ‘shallow’ sana bado.

Mfano unaposema “amini kila neno aliloambiwa mtu kwenye biblia umeambiwa wewe” si sahihi. Kuna mambo kwenye biblia wameambiwa wayahudi na yanaeahusu wao tu (kumbuka myahudi si mkristo) mfano; watumi 7 utaona Paulo anaongea na wayahudi kwa kuwa ndio waliokuwa chini ya sheria na mwenyewe anasisitiza kuwa anasema na wale waijuao sheria (those who under the law).

Usilete hisia na mtazamo wako binafsi unapojadili kuhusu biblia kwa kuwa biblia yenyewe inajitosheleza haihitaji maoni yako kuitetea, hivyo tumia vifungu vya biblia kuzaa hoja ya kuzungumza na si kuanzisha hoja zako kisha uanze kutafuta vifungu kwenye biblia vinavyo support hoja zako.

Kumbuka hata shetani ukisoma luka sura ya 4 na mathayo sura ya 4 pia alikuwa na ajenda zake zisizo za kimungu na alijaribu kutumia vifungu vya biblia kumhadaa Yesu.
 
Galileo Galilei aliongozwa na Biblia kuchunguza anga na kugundua dunia ni duara. Kwanza katika kitabu cha Isaya kuna mstari unazunguzmia uduara wa dunia.

Wakatoliki dini yao ilikuwa chini ya influence kubwa ya greek mythology sio Biblia. Nadharia za misiolojia za kigiriki zilikuwa backbone ya upinzani wao kwa Galilei. Maana ilionekana anabishana na wasomi ambao kanisa liliwaamini.

Ila alishaombwa msamaha na wakatoliki miaka ya 90 kuwa walikosea kumuhukumu msomi Galileo.
Hauwezi kuupinga ukatoliki then utumie biblia ambayo wao ndio wameitunza kwa maelfu ya miaka.
 
Mkuu ni mara nyingi naona unapost kuhusu biblia na mambo yahusuyo injili, inawezekana unatamani sana kufikisha habari njema kwa watu kama ilivyo amriwa kwa wakristo especially ukisoma marko 16:15-18.

Maoni yangu kwako ni kuwa, tafuta kujieleimisha sana kuhusu neno kabla hujaenda kujaribu kuelimisha wengine vinginevyo utawapa sababu zaidi watu wasipokee habari za ufalme kwa kuwa uko ‘shallow’ sana bado.

Mfano unaposema “amini kila neno aliloambiwa mtu kwenye biblia umeambiwa wewe” si sahihi. Kuna mambo kwenye biblia wameambiwa wayahudi na yanaeahusu wao tu (kumbuka myahudi si mkristo) mfano; watumi 7 utaona Paulo anaongea na wayahudi kwa kuwa ndio waliokuwa chini ya sheria na mwenyewe anasisitiza kuwa anasema na wale waijuao sheria (those who under the law).

Usilete hisia na mtazamo wako binafsi unapojadili kuhusu biblia kwa kuwa biblia yenyewe inajitosheleza haihitaji maoni yako kuitetea, hivyo tumia vifungu vya biblia kuzaa hoja ya kuzungumza na si kuanzisha hoja zako kisha uanze kutafuta vifungu kwenye biblia vinavyo support hoja zako.

Kumbuka hata shetani ukisoma luka sura ya 4 na mathayo sura ya 4 pia alikuwa na ajenda zake zisizo za kimungu na alijaribu kutumia vifungu vya biblia kumhadaa Yesu.
Asante kwa maoni.
Kila ninachoandikwa huwa nakiandika kwa ushawishi wa maandiko. Sijiandikii tu mkuu.

👇👇👇👇👇👇👇👇
Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini.
Warumi 15:4

Kila kilichoandikwa kinakuhusu wewe. Lazima utafute link kati ya kila andiko hata kama amekuwa adressed shetani na wewe uangalie linakuhusuje katika kufanya au kutokufanya.

Kwanza Wakristo ndio wayahudi au waisrael na sio vinginevyo. Hawa tunaowaita waisrael (judaism) kimsingi ni wapagani kama walivyo watu wengine wasiommuamini Yesu.
 
Ndio maana Ibrahim alizini kwa kukoswa uvumilivu. Sisi tunajifunza kuvumilia maana Mungu sio muongo.

Tazama hapa pia unasema Ibrahim alizini, una ushahidi wowote wa kimaandiko unaosema kuwa Ibrahim alizini au ni mtazamo wako tu?

Ibrahim aliishi kabla ya sheria hivyo hakuna namna utasema alitenda dhambi. Biblia inasema sheria ndiyo huzaa dhambi na dhambi huzaa mauti, na kabla ya sheria mtu hakuhesabiwa dhambi. Soma warumi 5:13 na yakobo 1:14.
 
Hauwezi kuupinga ukatoliki then utumie biblia ambayo wao ndio wameitunza kwa maelfu ya miaka.
Wakatoliki hawaamini Bibilia. Biblia kwao inahadhi sawa na kauli za kanisa na kauli za kipngozi wao. Hivyo kwao biblia sio msemaji wa mwisho. Hawaamini katika Sola Scriptura.

Pia sio kweli kwamba wameitunza biblia. Mingu amekuwa na mfumo wa kutunza maandiko yake, ndio maana alianza kumwambia Musa aandike, Baadae Ezra na nehemia, wakati Jerome anakusanya tayari yalikuwa yameshasambaa sehemu nyingi. Wakati wa Mitume Petro anasema nyaraka zilikuwa simesambaq makanisa mengi ya awali. Paulo mwenyewe hata wakati yuko gerezani Rumi bado alikuwa na vitabu vingi vya ngozi vya maandiko ambavyo alimtuma kijana wake timotheo amletee.

Kuhusu kumpinga Galilei haijalishi wawe nayo au wasiwe nayo Biblia. Maana hata Yesu aliuwawa na watu ambao wanazo biblia.
 
Wakatoliki hawaamini Bibilia. Biblia kwao inahadhi sawa na kauli za kanisa na kauli za kipngozi wao. Hivyo kwao biblia sio msemaji wa mwisho. Hawaamini katika Sola Scriptura.

Pia sio kweli kwamba wameitunza biblia. Mingu amekuwa na mfumo wa kutunza maandiko yake, ndio maana alianza kumwambia Musa aandike, Baadae Ezra na nehemia, wakati Jerome anakusanya tayari yalikuwa yameshasambaa sehemu nyingi. Wakati wa Mitume Petro anasema nyaraka zilikuwa simesambaq makanisa mengi ya awali. Paulo mwenyewe hata wakati yuko gerezani Rumi bado alikuwa na vitabu vingi vya ngozi vya maandiko ambavyo alimtuma kijana wake timotheo amletee.

Kuhusu kumpinga Galilei haijalishi wawe nayo au wasiwe nayo Biblia. Maana hata Yesu aliuwawa na watu ambao wanazo biblia.
Ukristo ni ukatoliki tu nyie wengne mlijiongeza ili nanyie mpige pesa kwa baadhi ya vifungu
 
Hakuandikiwa timotheo kama mtu binafsi. Timotheo alikuwa kiongozi wa kanisa, yeye alikuwa ni link na watu. Hayo ni maelekezo ambayo sio kwa ajili yake tu bali wote.
Ndio maana anaelezea hadi dalili za siku za mwisho. Waraka wa pili kwa Timotheo 3. Wakati hayo maneno hayamuhusu maana ameshakufa sasa.

Hizo ni hekima za juu sana ambazo Mungu ameamua kutumia kutufikishia ujumbe kwa njia nyingi. Ndio maana kumejaa unabii, nyaraka, mithali, mashairi, nyimbo, hadithi, mafumbo, sitiari, tashtiti, na kila namna ya uandishi ambao utagonga kila angle ya ubongo kuamsha ufahamu

Hakuandikiwa timotheo kama mtu binafsi. Timotheo alikuwa kiongozi wa kanisa, yeye alikuwa ni link na watu. Hayo ni maelekezo ambayo sio kwa ajili yake tu bali wote.
Ndio maana anaelezea hadi dalili za siku za mwisho. Waraka wa pili kwa Timotheo 3. Wakati hayo maneno hayamuhusu maana ameshakufa sasa.

Hizo ni hekima za juu sana ambazo Mungu ameamua kutumia kutufikishia ujumbe kwa njia nyingi. Ndio maana kumejaa unabii, nyaraka, mithali, mashairi, nyimbo, hadithi, mafumbo, sitiari, tashtiti, na kila namna ya uandishi ambao utagonga kila angle ya ubongo kuamsha ufahamu
Sasa kwanini iwe ni "waraka kwa Timotheo" na si kwa "kanisa"??

Ni lazima tujue imeandikwa lini, wapi aliandikiwa nani, kuhusu nini nk..
 
Tazama hapa pia unasema Ibrahim alizini, una ushahidi wowote wa kimaandiko unaosema kuwa Ibrahim alizini au ni mtazamo wako tu?

Ibrahim aliishi kabla ya sheria hivyo hakuna namna utasema alitenda dhambi. Biblia inasema sheria ndiyo huzaa dhambi na dhambi huzaa mauti, na kabla ya sheria mtu hakuhesabiwa dhambi. Soma warumi 5:13 na yakobo 1:14.
Uzinzi ulianza lini?
Maana Maandiko yanasema wakati wa Ibrahim sheria amri na maagizo ya Mungu yalikuwepo. Inaonekana unamaarifa ya upande mmoja.

Kwa sababu Ibrahimu alisikia sauti yangu, akayahifadhi maagizo yangu, na amri zangu, na hukumu zangu, na sheria zangu. Mwanzo 26:5

Pia ukumbuke dhambi ni uasi wa sheria za Mungu. Vinginevyo watu wa sodoma, watu wa kizazi cha Nuhu, Kaini kumuua Habiri wasingehesabiwa kosa maana hakukuwa na sheria.

Tumuelewe Mungu kwa mapana.
 
Back
Top Bottom