Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 69,538
- 122,962
Wakati wa Mwalimu Nyerere hatukusikia wala kuona hivi vituko vinavyotokea siku hizi,hata alipokuja Ali Hassani Mwinyi, Mkapa na yalianza kuchomoza kidogo wakati wa Kikwete na yamekuwa na kukuzwa kupita mipaka kwa Hayati Magufuli na sasa ndio usiseme Raisi Samia akikohoa utaona kwenye vyombo vya habari amekohoa kwa mbwembwe, yaani sasa ni kusifia kwa kwenda mbele.
Hii tabia inawafanya hawa wachaguliwa kujiona wamekamilika na wanaweza kufanya wanalo taka kama tuonavyo, wakati wake Mzee Julius Nyerere ulikuwa huoni mihemko ya kusifiwa sifiwa, sijui kajenga hili kafanya lile mangapi ameyafanya katika nchi hii? Leo mtu akifungua choo basi makelele nchi nzima.
Inakuwa ile hadithi ya mfalme, tuacheni ujinga huu,mimi naona ni ujinga ,ushamba na kutokujielewa tunafanya nini na tunakwenda wapi, hii haina tofauti na ile tabia ijulikanayo siku hizi ya kujipitisha, wanaosifu wanasifu kila kitu alimradi na wao waonekane mwisho mtakuja kusifia ujinga.
Hii tabia imeanza rasmi baada ya ccm kuanza kuzidiwa dhahiri na vyama vya upinzani,hasa awamu ya mwisho ya JK. Hivyo wanaccm wakaanza kujenga tabia ya kumsifia rais ili kuonyesha ni mchapa kazi. Alipoingia madarakani Magufuli maana aliingia kwa uchaguzi kuchezewa, yeye akatengeneza vikundi vya propaganda kabisa ya kumsifia, hii ilienda sambamba na kuhakikisha wapinzani hawaruhusiwi kufanya siasa, na yeye hakosolewi. Eneo hili sukuma gang hawakutaka mchezo kabisa hadi wakawa mpaka wanateka, kuua na kubambikia kesi wanaomkosoa Magufuli.
Sasa tabia ile imeota rasmi mizizi ndani ya ccm. Kila rais akiingia anakuwa na genge lake la kumsifia. Kwa sasa Msoga line ndio wanaendesha kundi la kumsifia Mama. Kila hela ya umma ikitoka inaitwa ni ya mama Samia. Ila inflation iliyopo sio ya Mama Samia bali ni sababu ya vita vya Ukraine! Sababu hasa ya ccm kufanya hizi siasa za ghiliba dhidi ya umma, ni kwakuwa hawako madarakani kwa ridhaa ya wananchi, hivyo wanashurutisha kukubalika.