Mambo ya kufanya ili usimchoke mke wako

Mambo ya kufanya ili usimchoke mke wako

saddyy

Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
58
Reaction score
54
Mambo ya kufanya ili usimchoke mke wako;

1. Kuwa na ratiba maalumu ya kufanya tendo la ndoa na sio vurugu vurugu au kila wakati.

2. Mpendezeshe mkeo kwa mavazi na chakula bora kwani atakuwa na siha(afya) nzuri na hivyo kumona mpya.

3. Jambo la muhimu kuliko vyote ni maneno mazuri juu ya mkeo kwani humfanya awe mtulivu wa nafsi na atanawiri kwa kuridhika kwa maneno mazuri kutoka kwako na faraja unayompa na atakupenda kuliko kitu chochote.

4. Kumbuka kuwa upendo ni faraja ya maneno na kucheka na mkeo hata kama kuna jambo la kukutia hasira basi lifiche kwa mkeo na kama ni kuomba ushauri basi pia kwa upole.

5. Mfanye mkeo awe huru kukuambia anachopenda ili umridhishe, ilimradi tu liwe ndani ya uwezo wako.

6. Msifanye mapenzi kila mara, mtachokana.

7. Mwanamke unapomletea zawadi hufurahi sana kuliko kumpatia hela akanunue zawadi. aliyemletea mkewe mtandio wa sh 10,000 na aliyempa mkewe 50,000 akanunue kitu chochote. basi aliyeletewa mtandio atakuwa na faraja zaidi.

8. Kumbuka kuwa mwanamke ni kama mtoto mdogo, hupenda sana kudeka na hasa ukijua kudekeza na atakupenda sana ukifanya hivyo.

9. Uaminifu ndiyo kitu bora baina yenu, na uaminifu huja kwa kufuata dondoo za juu hapo.hizo ndizo siri za nyinyi kudumisha upendo wenu na hata mkiishi miaka 100 lakini mtaonana wapya siku zote.
 
wanawakw siyo watu wa kawaida hata ungemfanyia nini ipo siku atakuona ----- tuu,,,,, na siku hizi vijana hatuowi tuna kula na kutembea
 
saddyy

Kumbe wewe unamchokaga mkeo. Basi fanya wewe hayo mambo kwani hakuna mtu mwingine aliyewahi kumchoka mkewe zaidi yako wewe.
 
Last edited by a moderator:
saddyy

Na ili mwanamke asichokwe yampasa aache ku Nag...Nagging.....
(kulalama lalama kwa sauti ya ki chini chii bila kuelewa ana maanisha nini hasa.)
 
Last edited by a moderator:
wanaume mbona mnakua wakali hivyo. km limekugusa fanyia kazi
 
Mwanamke anahitaji attention tu mengine yote mbwembwe
 
hata mmea bila matunzo haukui na ukikua kamwe hauwi ni wenye afya nzur well said.
 
Zote mbwembwe tu,siku hizi mianamke hata uifanyie nini kama imeamua kuchapwa nao watachapwa nao,
nami nasema hakuna namna wachapwe nao tu na joka jeusi.
Wamawake hawana utulivu sasa.
 
Maisha ya ndoa ni kama nguo - lazima ichafuke na kufuliwa tena hili iendelee kung'aa - mengine ni longolongo tu mitandaoni.

Kikubwa ni kuheshimiana tu - sio kuoneshana kila kitu.
 
wanawakw siyo watu wa kawaida hata ungemfanyia nini ipo siku atakuona ----- tuu,,,,, na siku hizi vijana hatuowi tuna kula na kutembea

utabaki hivo hivo na maneno yako cku utakula visivoliwa ndo utakuwa mwisho wako
 
hapa hakuna formula.. usikariri
hayo wafanyie wanafunzi wa Form 2C
 
Saddy umeoa au umesoma hizo dondoo mahali!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom