Mambo ya kiungwana ambayo mtu akiyafanya huonekana wa ajabu machoni pa wajinga

HUO ndio ulimbukeni tulioiga kwa wakenya lakini sisi wa tz asili yetu twaamini kuwa binadamu wote ni ndugu tutajuanaje tusipoanza kusalimiana ukiimbiwa habari za jioni ukajibu salama unapungukiwa nini au aliyekusalimia unakuwa umemwongezea nini?. Acheni hivyo huwezi kujua nani atakufaa wakati wa dhiki. Vijana wawili walianza kukorofishana kwenye gari na kurushiana matusi ya nguoni kwenye gari alikuwemo Sajenti wa JKT akaamua kuwapeleka Polisi walipoulizwa particulars zao kumbe wote babu yao ni mmoja ambaye anaishi BAGAMOYO KWA HIYO KWA namna moja ama nyingine sisi sote ni ndugu

Ulimbukeni ndio huo wa kutaka kusalimia kila unayekutana nae! Eti kuwaiga Wakenya; kwani Wakenya ndo nani?! Watu wanatembea na mambo yao kichwani huku wengine wakiwa wana-digest mambo ya msingi...watu wakiwa katika state kama hiyo, we unaanza "habari za leo...!" Then, wht next?! Kusalimia tu; basi?! Kama unanisalimia ili uniulize jambo (kama unazani ni lazima kufanya hivyo), then fine lakini kunisalimia tu bila la ziada ni upuuzi! Utasalimia wangapi na utaitikia salamu za wangapi?! Unakuta mtu umetulia kwenye daladala tulii, hakujui humjui anaanza kukuongelesha tena kwa stori zisizo na kichwa wala miguu...; huko ni kupotezeana muda bana....!! u can't share stories with some1 u don' know his/her interests! By the way, uzoefu unaonesha kwamba ukikutana na mtu akaanza kukusalimia kwa adabu zote, kinachofuata hapo ni mzinga wa "niongozee nauli" utafikiri ni wewe ndie ulimleta hiyo sehemu!! Wengine ni wezi na matapeli tu....anatafuta namna ya kukuzoea ili akulize! madogo nao siku hizi hawajambo; ukisikia "shikamoo..!" kinachofuata hapo...."naomba shing mia!" All in all, unanisalimia ili iweje?! Kama ni kusalimia tu, basi...then utasalimia wangapi?!
 
Aisee! Kweli hao watu walikosa ustaarabu. Ila huyo dada nae kwa ustaarabu huo atasalimia wangapi jamani jiji lenyewe hili!!
 
Nyingine ifananayo na hiyo,
Eti kwamba ukiwa muajiriwa TRA, BANDARINI , POLICE (TRAFIC) na ukafanya kazi yako , kwa maadili (ukajikataza rushwa na ufisidi) ukaja kuacha job kwa sababu zozote zile , ikiwa wakati huo unamiliki gari moja na nyumba umebakiza kuezeka tu ! Utawasikia
"yule jamaa mjinga/mpumbavu/**** kweli ! Miaka yote aliyokua pale , eti alikua anajifanya mlokole! Eti ka'gari kamoja !
Na ka'nyumba kamoja hata hakajaezekwa !
 
Nimekumbuka wakati fulani nilikula katika Hotel hapo Moshi tukiwa na jamaa zangu, nilipomaliza kula nilimshukuru yule dada aliyetuhudumia jamaa walinitolea macho na kunikashfu kuwa kwa nini nimwambie asante wakati nalipia ile huduma?
Nilichowajibu ni kuwa pamoja na kuwa nalipia huduma ile kushukuru kwa ajili ya huduma ni ungwana zaidi ni kukubaliana na huduma aliyoitoa kwangu/kwetu. Kiukweli jamaa hawakunielewa lakini huo ndo utaratibu wangu, nitashukuru kwa huduma yoyote nitakayopewa na nitamsalimia yeyote na popote.

My take: malezi tuliyopata ni tatizo sana hasa kwa kizazi hiki, na kwa kuwa tumegundua tatizo ni vema basi watoto wetu tuwalee katika mazingira chanya ya kuwa watii na wenye kutambua na kukubali michango ya wengine kwa maana ya kuwa wana-appreciate na kutamua utu wa watu popote katika mazingira ya kila siku!
 

Baada ya huko kunisalimia, then what next?! Kunisalimia tu, basi?!
Nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani.
Ila, kama tupo wawili tunaingia kwenye elevator au tunakaa kiti kimoja kwenye usafiri wa umma, mimi nitakusalimia. Nia ni kuanzisha conversation au kama wewe ni dada halafu ukajibu kwa tabasamu la kuua mtu, ndiyo lazima ni drop the repertoire!..... you never know.
But all in all kusalimiana ni dalili ya ustaarabu.
 
Nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani.
Ila, kama tupo wawili tunaingia kwenye elevator au tunakaa kiti kimoja kwenye usafiri wa umma, mimi nitakusalimia. Nia ni kuanzisha conversation au kama wewe ni dada halafu ukajibu kwa tabasamu la kuua mtu, ndiyo lazima ni drop the repertoire!..... you never know.
But all in all kusalimiana ni dalili ya ustaarabu.

Kwenye elevator, I agree with u especially whn u're only TWO of u; kwenye daladala, not necessary especially asubuhi ambapo wengine wameamka na ma-stress yao we unaanza kuwaongelesha ongelesha!! Jioni, nayo sio muafaka...watu washajichokea, wanahitaji kupumzika na ku-reflesh minds zao! Wengine kazi zao tangu wanaingia ofisini ni full kuongea na kujibu maswali....anafika kwenye daladala apumzike na stress za wateja; nawe unaanza kumuongelesha ongelesha tena! Kitaa, sawa; coz' wengi mtakuwa mnafahamiana...lakini city centre, kariakoo, mlimani city, quality centre, kitongoji ambacho wewe si mkazi (e.g., unaishi tameke, upo mwenge) na sehemu zingine kama hizo....HAPANA, unless kama una sababu za msingi za kufanya hivyo! tena unakuta wengine hawajisikii raha kwamba wamesalimia hadi wasimame kidogo...which means, nawe usimame kidogo kusikiliza na kuitikia salam! Halafu kuna hawa watu, ambao vile vile huwa wananikera sana! sawa, mnafahamiana; and in most case, juu juu tu...na huenda hata namba ya simu yako anayo! Mnakutana barabarani anaanza hadithi ndeeeeeeefu!! Usipokuwa careful, mtapoteza hadi robo saa! Mtu unajiuliza, kama alikuwa na shida na wewe kwanini hakukutafuta in advance; mnakutana barabarani ndo anaanza riwaya zake! Kama mi ndo nimefuatana na wewe; halafu barabarani tunakutana na mtu unaanza nae hadithi zisizoisha; hesabu nakuacha hapo hapo.
 
Salaam ni jambo jema sana..

Lakini kila jambo jema lazima lifanywe kwa HEKIMA...

Salaam pia kuna hekma inatakiwa kuzingatiwa..mahali, watu, wanafanya nini etc..
 

Kwenye elevator, I agree with u especially whn u're only TWO of u; kwenye daladala, not necessary especially asubuhi ambapo wengine wameamka na ma-stress yao we unaanza kuwaongelesha ongelesha!! Jioni, nayo sio muafaka...watu washajichokea, wanahitaji kupumzika na ku-reflesh minds zao! Wengine kazi zao tangu wanaingia ofisini ni full kuongea na kujibu maswali....anafika kwenye daladala apumzike na stress za wateja; nawe unaanza kumuongelesha ongelesha tena! Kitaa, sawa; coz' wengi mtakuwa mnafahamiana...lakini city centre, kariakoo, mlimani city, quality centre, kitongoji ambacho wewe si mkazi (e.g., unaishi tameke, upo mwenge) na sehemu zingine kama hizo....HAPANA, unless kama una sababu za msingi za kufanya hivyo! tena unakuta wengine hawajisikii raha kwamba wamesalimia hadi wasimame kidogo...which means, nawe usimame kidogo kusikiliza na kuitikia salam! Halafu kuna hawa watu, ambao vile vile huwa wananikera sana! sawa, mnafahamiana; and in most case, juu juu tu...na huenda hata namba ya simu yako anayo! Mnakutana barabarani anaanza hadithi ndeeeeeeefu!! Usipokuwa careful, mtapoteza hadi robo saa! Mtu unajiuliza, kama alikuwa na shida na wewe kwanini hakukutafuta in advance; mnakutana barabarani ndo anaanza riwaya zake! Kama mi ndo nimefuatana na wewe; halafu barabarani tunakutana na mtu unaanza nae hadithi zisizoisha; hesabu nakuacha hapo hapo.
baadhi ya maelezo yako yana point,ila baadhi ya maelezo umetype kwa kiukali.you need to calm down
 
baadhi ya maelezo yako yana point,ila baadhi ya maelezo umetype kwa kiukali.you need to calm down


Kama vile? The problem ni kwamba, wewe ni kisukari; kwahiyo hata ukikutana na kichungwa, utakiona kichachu tu!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom