Kwa maswala ya kijeshi waachie wenyewe!
Uchumi wa Kenya kushuka, umeshaeleza sababu. Ila zingatia kuwa bado wako juu ingawa tunawazidi resources. Hii ina maana, tukipata viongozi wasioenda kujenga bandari kwa kigezo cha nyumbani, kiongozi anayeondoa mazingira ya uibaji hela za Umma, kiongozi anayepinga ufisadi kwa dhati, kiongozi atakayezingatia uwakilishi stahiki wa wazawa kumilikishwa sehemu ya raslimali ya nchi, nk; nchi yetu itapaa!
Mkuu Anjo, uko sahihi kabisa. Tanzania ni nchi yenye resources nyingi ila ilikosa watu(viongozi) wenye Akili wa ku-utilise hizo raslimali kwa maendeleo ya watu na nchi kwa ujumla. tuna kila kitu to mention in few, Bandari, mbuga za wanyama, madini, etc etc....lakini hatuna utofauti na kutokuwa nayo. bahati mbaya tumepoteza dira na tumebaki kulalamika. kinachoshangaza, ni kuwa kila mtu analalamika, kuanzia Rais, waziri mkuu, wabunge mpaka common mwananchi kama mimi bado nimebaki kulalamika. mkuu kama hautojali, nina hypothesis zifuatazo, kama utakuwa na majibu yake itapendeza;
(1) Kutoendelea kwa Tanzania kiuchumi, si kwamba kunasababishwa na sera mbovu na maono butu chini ya influence ya World bank na IMF
(2) Kulingana na Elimu duni tulizonazo sisi wananchi tumeshindwa kufanya maamuzi sahihi yenye kuleta Tija kwa nchi kwa kushinda tunashabikia vyama badala ya sera na kuwaweka madarakani vibaka wa uchumi wa nchi? je nani alaumiwe?
(3)kuna hearsay kuwa, mwaka 1984 tulikumbwa na baa la njaa nchini TZ na hali ilikuwa mbaya sana.(mimi mwenyewe shahidi) hivyo basi mwalimu Nyerere alikwenda USA kuomba msaada wa chakula. kweli US walitupa msaada wa chakula, unga wa yellow corn (yanga) ambacho kwao ni chakula cha kulisha mifugo. the point here is, unga ule ulikuwa na madhara makubwa kwa watumiaji (genetically). hivyo basi, side effect zimeendelea kuwepo vizazi kwa vizazi. ndo maana kuna tofauti ya thinking capacity kati ya generation ya miaka ya 70,80,90 mpaka leo. therefore our political leaders are victims of the circumstance. cant think beyond the box.
(Note: hii ni hearsay na sina uhakika nayo)