fangfangjt
JF-Expert Member
- Apr 25, 2008
- 571
- 139
Tatizo nafikiri hatufati kanuni za uadishi wa paper, ni lazima uli reference mahala fulani ili ku -justfy unachoongelea. Nani alikuambieni Sita, mwakyembe wanapigania masilahi yako. Fuatilia kwa makini mwanzoni mwa sakata la Richmord sita akiwa spika wakati huo wakiwa kundi moja na akina RA. Hoja alijaribu sana kuizima na kusema ulongo ulongo. Sita ameanza kupigana baada ya ku defect kutokana na kuzidiwa ujanja.
Tatizo wewe unaongea kama watoto wa Gadafi kumhasi baba yao na eti nao wamuite dictator baba yao, hasa unapowataja akina Mwinyi. Na vijana wachache waliopo wala sio wakutolea mfano kwa sababu wazee wamewa-abducted.
Tanzania hakuna mzee anayepigania haki ya Tanzania ila ni majambazi wawili wanapigania walichokipora, sasa mmoja anaonekana kulemewa. Na wengine wako pembeni wakitamani kuingia mahali hapo nao waibe.
- The dataz is: Ilikuwa either mabadiliko au six and the gang to Opposition!...ha! ha! ha! ha! ha! six won! ha! ha! ha!....ooooooh! six the man unapoweza kumtukana mkulu na akakupa uwaziri anyways! ha! ha! ha!
......stay ....tuned...!
Field Marshall Es!
Katiba ya Chama cha Mapinduzi inasema wazi kuwa majukumu ya kuleta nidhamu yako kwa Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC)katika ngazi mbalimbali za uongozi kitaifa. Katiba hiyo inasema hivi (Ibara ya 107 inayoshughulikia na Kazi za Halmashauri Kuu ya Taifa):
Kwa hiyo kwa vifungu hivyo viwili tu tunaweza kuona kuwa NEC inaweza kufanya mambo mbalimbali ikiwemo "kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake uifanywa na NEC".
Ibara ya 109 inaweka mojawapo ya mjukumu ya Kamati Kuu ya Taifa ni:
Halafu inabidi tuangalie kuwa Sekretariati ya CCM wajumbe wake wote wanaingia kutoka na nyadhifa zao. Hii ina maana hakuna ambaye anaingia kwa kuteuliwa na Mwenyekiti. Mwenyekiti wa CCM Taifa hana madaraka ya kumuondoa au kumsimamisha kiongozi yeyote wa CCM. Hata kama Mwenyekiti huyo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hii ina maana gani?
Ina maana ya kwamba lolote lililofanyika Dodoma litakuwa ni tendo la Kamati Kuu au Halmashauri Kuu ya Taifa. Tukumbuke kuwa Mwenyekiti ana kura ya turufu pale tu endapo kura za wajumbe zinalingana katika vikao visivyo husiana na vya uchaguzi - kwani huko ana kura moja.
Ina maana:
a. JK hakuvunja Sekretariati ya Halmashauri Kuu kwani hana madaraka hayo
b. JK hakuvunja Kamati Kuu kwani hana madaraka hayo
c. JK hakumuondoa mtu yeyote uongozi
Hii ina maana kuwa lolote lililotokea Dodoma limetokana na NEC au CC; na hii ina maana ya kwamba wale watu waliokuwa wanaonekana ni vigogo kweli na wana influence ndani ya Chama inawezekana hawana influence ambayo walidhania wanayo. The only x-factor katika hili lote ni kuwa Mwenyekiti wa CCM ndiye Rais vile vile na Katiba ya CCM haitoi maelekezo ya M/Kiti atumie madaraka yake vipi endapo ndiye Rais? Hivyo kama hana nguvu fulani kama mwenyekiti anaweza kutumia madaraka ya Urais kutimiza mambo mbalimbali.
Na hicho ndicho ambavyo kitakuwa kimetokea.
- The dataz is: Ilikuwa either mabadiliko au six and the gang to Opposition!...ha! ha! ha! ha! ha! six won! ha! ha! ha!....ooooooh! six the man unapoweza kumtukana mkulu na akakupa uwaziri anyways! ha! ha! ha!
......stay ....tuned...!
Field Marshall Es!
Watanzania watu wa ajabu sana
Yaani kwenu this is the most important news of all?
You guys never cease to amaze me
watu wamekutana na chama chao kicha wanaamua who has to go and who has to stay kwenu hiyo big news?
Hivi kweli matatizo yote tuliyonayo kuanzia TRA, bandarini na uchafu ulikokithiri na matatizo ya elimu na afya yatatatulika baada ya kuondolewa watu wawili au baada ya kuvunjwa kamati kuu ya CCM?
Msipotoshe watu JK hakufukuza mtu bali wamejiuzulu!!!!
soma hapa: Fresh start for CCM as CC, secretariat resigns
Wewe ndio unapotosha watu kwa kuwa unaamini kwenye propaganda na kiswahili chenu cha kizushi, Tumia akili kama mtu mzima, wamejiudhuru au wameamriashwa wajiudhuru ili kunusuru chama?. Unaka kutuambia wamehiari kufanya hicho kitendo cha kujiudhuru?. Nyie ndio mnaendelea kupotosha watu hata kusema Lowassa ni waziri mkuu msitaafu. Hivyo viswahili vya kisanii pelekeni majukwaani huko mnawadanganya na kuwapotosha watanzania, kwenye hili jukwaa la electronic hatuihitaji upuuzi wote tunajua kilichotokea Dodoma jana.
Marriage is a legalized prostitution