Mambo gani yanaweza kubatilisha WOSIA?

Endapo nitaandika wosia kuhusu jinsi gani Mali zangu zigawanywe kwa wategemezi wangu kama mke watoto na ndugu!

Mfano:
Nina watoto wanne kwa mke mmoja na katika wosia wangu nikaeleza kuwa Mali zangu zigawanywe kwa mke, watoto watatu na nikawataja kwa majina, pia nikaeleza mtoto mmoja asihusike kwenye urithi wa Mali zangu bila kuweka wazi sababu za kufanya hivyo! Je, wosia wangu utabaki kuwa halali endapo nikifariki?

Je, ni mambo gani au mazingira gani yanaufanya wosia kuwa batili?
ndugu, kuna kitabu kimoja kizuri sana kimefafanua hayo mambo yooote kwa kiswahili, ukikipata kitabu hiki hauna haja ya mwanasheria kabisa. bofya hapa www.sheriakwakiswahili.blogspot.com halafu nipe update.
 
Utabaki halali sababu wosia hata siku moja hauwezi kubadilishwa...u can not challenge nor change a will.So kama umeandika asipewe ni hapewi kitu hata kimoja.


Sasa hiyo sentensi ya Kiingereza ilikuwa na ulazima gani hapo?
 
Sijui kwa imani zngine, lkn kwa imani nnayofuata mimi, mke na watoto, iwe umewapa chao ktk wosia ama hukuwapa, bado watarithi na kwa hiyo wasia wako ni batili!

Lkn pia kama uluchogawa ktk wasia ni kikubwa kuliko mali iliobaki baada ya wasia, wasia wako
 
Wosia utakua batili kama

Kumeandikwa wosia mwingine mpya

2. Kama mashahidi wote wamekufa

3. Kama hukuwekwa saini eidha ya dole gumba au ya kawaida

Pia kama HUKU wosia huo hukushuhudiwa na watu japo wawili toka kwenye ukoo wako

Kama ni wosia wa maneno utabatilishwa kama utaandikwa wa maandishi

Pia kama wosia huo utafanyiwa marekebisho kwa maana ya kufuta baadhi ya maneno au kuongeza kutafanywa na mtu ambae si testator


Mkuu nikuulize shwali kwenye maelezo yako hapo juu

Je kama wosia umewekwa sahihi lakini hauna mashahidi zaidi ya wawili, pili warithi wakaridhia kuwa kuwa ule ni urithi halali wa marehemu na wakaamua kuuheshimu.

Ila baada ya miaka kama 3 kupita mmoja wa wale warithi akafungua kesi mahakani kupinga ule urithi si halali.

Basi ikiwa huyo mmoja kati hao warithi hakubaliani na huo urithi hivyo anaweza kuufanya kuwa batili?
 
Hivi baada ya kuandika wosia inatakiwa niuhifadhi wapi? Mahakamani au nyumbani? Na wagawaji watajuaje kuwa kuwa niliandika wosia na upo sehem flani, na je wakijua wosia upo sehem flani na mtoto mmojo sio miongoni mwa warithi haweZi anzisha zogo?
 
Hivi baada ya kuandika wosia inatakiwa niuhifadhi wapi? Mahakamani au nyumbani? Na wagawaji watajuaje kuwa kuwa niliandika wosia na upo sehem flani, na je wakijua wosia upo sehem flani na mtoto mmojo sio miongoni mwa warithi haweZi anzisha zogo?
Hapo ndo maana wanasema wosia ni vizuri uwe siri maana mnufaikaji akijua anweza anzusha zogo endapo akiona hajatendewa haki au akamuua hata mzazi wake aliyeandika wosia endapo ataona ameandikiwa kurithi mali nzuri na mzee anavuta tuu muda hataki kufa.
 
Hivi baada ya kuandika wosia inatakiwa niuhifadhi wapi? Mahakamani au nyumbani? Na wagawaji watajuaje kuwa kuwa niliandika wosia na upo sehem flani, na je wakijua wosia upo sehem flani na mtoto mmojo sio miongoni mwa warithi haweZi anzisha zogo?
mkuu swali zuri sana hili. ngoja,wataalamu wa mirathi waje watujibu...!
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom