Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Wajasiriamali wadogo wakiwemo mamalishe, babalishe na vijana wa bodaboda mkoani Arusha leo Jumanne Agosti 12, 2025 wamejitokeza kwa wingi kumuunga mkono na kumdhamini mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan.
Wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenani Kihongosi, wajasiriamali hao walifika katika Ofisi za CCM Wilaya ya Arusha na kusaini fomu za udhamini, wakisema wameona mabadiliko makubwa katika maisha yao kutokana na sera na miradi iliyotekelezwa katika miaka minne ya uongozi wa Samia.
“Mama Samia ametupatia mazingira bora ya kufanyia biashara, mikopo yenye masharti nafuu na masoko ya bidhaa zetu. Ndiyo maana tupo tayari kumdhamini na kumpa kura zetu,” amesema Asha Mohamed, mama lishe kutoka Soko Kuu la Arusha.
Wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenani Kihongosi, wajasiriamali hao walifika katika Ofisi za CCM Wilaya ya Arusha na kusaini fomu za udhamini, wakisema wameona mabadiliko makubwa katika maisha yao kutokana na sera na miradi iliyotekelezwa katika miaka minne ya uongozi wa Samia.
“Mama Samia ametupatia mazingira bora ya kufanyia biashara, mikopo yenye masharti nafuu na masoko ya bidhaa zetu. Ndiyo maana tupo tayari kumdhamini na kumpa kura zetu,” amesema Asha Mohamed, mama lishe kutoka Soko Kuu la Arusha.