Mwambie hivi" unajua mama nilikuwa nakuficha, ila nina ujauzito wa miezi mitatu, baba mtoto nitamleta home nikipata likizo".Habari za wakati huu wana MMU, ni wiki ya pili sasa toka mama yangu mzazi aje kunitembelea.Nimefurahi na kiasi flani nyumba imechangamka.ishu iliyonisukuma kuandika uzi huu usiku huu ni kuwa mama ananilazimisha niolewe ama nizae ilhali mie siko tayari kwa sasa.ananiambia wamenitafutia mchumba huko nyumbani kwani shule nilishahitimu nina kazi na maisha yake mahali pake.kwahiyo jambo lililobaki ni kuolewa na kuanza familia.anasema wajomba wamemtuma na anatakiwa arudi na jibu.nimekosa raha kwakweli na nimekuwa nachelewa kurudi nyumbani from job,kwani nikitoka tu kazini napitia bar najilipua vya kutosha hadi mida mibovu nikirudi nakuta kalala.leo kanikamata kutwa nzima sijatoka na amenambia hataondoka hapa kwangu hadi nimpe jibu la uhakika.kwa mila za kwetu wajomba wana nguvu sana na nawaogopa sana wajomba zangu.wala sitaki kuwavunjia heshima.ila sina mpango wa kuolewa bali nimepanga kupata mtoto nayo si leo wala kesho.
nahitaji mchango wenu wa mawazo.huyu maza nampa jibu gani ili aniache niendelee kuishi life style niliyoizoea?​
anza kujifanya unachagua vyakula vya kula ili aanze kuhisi kitu kabla hauja-break news.
akishaondoka, kaa kama miezi miwili hivi siku moja umwambie, "mama, leo ndio nimeruhusiwa kutoka hospitali, ile mimba ilitoka,wamenisafisha kizazi, naendelea vizuri".