Chamviga,
Tangu nimekuwa mwanachama wa JF au mtandao mwingine wowote daima nimeingia kwa jina langu kamili Dr.W.Slaa. Ni kwa kuwa naamini kutumia jina bandia ni dalili ya uwoga. Yeyote mwenye anaweza kupima ninachoamini kwa kuonyesha identity yangu halisi. Hata hivyo, si vema kuvumilia upotoshwaji na udanganyifu wenye hill mbaya.
1) Leo niliposoma Gazeti la Mtanzania kwa nafasi yangu ya Katibu Mkuu nilimpigia simu Mama Zitto, kwanza kumpa pole na pili kujua hasa yaliyomsibu. Aliyoniambia mama Zitto yanapingana na yote yaliyoandikwa humo, mengine yakidhaniwa yamesemwa na mama Zitto, na mengine yakiandikwa na wachangiaji kwa his kali. Ni hatari sana taifa kuachia watu wakifanya utani na mambo yanayohusu maisha ya binadamu. Tutakuwa sio Taifa serious, linalogeuza kila kitu kuwa utani au ushabiki tu! Labda Mama Zitto akiniambia kuwa alinidanganya, na sioni ni kwanini anidanganye!
2) Nataka niweke wazi, mama Zitto hakuzungungumza nami, na wall kwa wakati wowote, sikumwambia amwone Hemedi Sabula. Yeye aliniambia amenitafuta, akanikosa, akamtafuta Sabula akamkosa. Hatimaye alimpata kwa simu ya Tendwa, afisa Ugavi, Makao Makuu. Pili, nimeongea na Mwenyekiti Mbowe, naye amenithibitishia hakuongea na Mama Zitto. Kauli hiyo inalingana na aliyoniambia Mama Zitto kuwa hakuwa amemjulisha Mwenyekiti Taifa. Ni dhahiri kauli zilizoandikwa kwenye mtandao huu zina malengo ambayo ni ya makusudi, na muda si mrefu tutayajua yote, lakini kwa vyovyote, dalili za awali zinaonyesha hazina nia njema na Chadema na viongozi wake.
3) Nimeongea na Afisa wangu Sabula kinachozungumzwa hap ni kinyume kabisa na alichozungumza na Mama Zitto, na nimethibitisha hayo kwa Mama Zitto Mwenyewe.
4) Nimewasiliana na viongozi wangu wa Jimbo na Kata, kuhusiana na kijiwe chochote kinachojengwa. Taarifa sahihi ni kuwa hakuna kijiwe chochote kinachojengwa na kilichoombewa fedha kwa Mama Zitto. Ila kuna Ofisi ya Kata inakarabatiwa ndiyo iliyoombewa fedha, na wahusika walifika kwa mama Zitto na wakapewa fedha 30,000. Sitaki kuingilia uchunguzi wa Polisi, ninataka tu kuwasaidia walioingia kwenye Mtandao wengi wao kwa ID bandia na kutoa kauli nzito juu ya mambo wasioyoyafahamu na kutoa uhukumu.
Nimetoa taarifa hii kwa wote wanaotaka kujadili kwa nia njema, na stoa taarifa kwa mujibu wa majukumu na nafasi yangu kwa kuwa wanaozungumzwa wote ni viongozi ninaowahudumia kwa mujibu wa Katiba ya Chadema. Aidha, ni jukumu langu kulinda jina la Chadema pale ninapoona intake kuchafuliwa bila msingi, wala utafiti wowote. Mengine nitaendelea kuwajulisha aunkuyaweka hadharani kwa kaduri yatakavyokuwa lazima. Naamini kwa wale wenye nia njema haya yatawasaidia kujadili kwa Tija thread hii.
Nimefuatilia kwa umakini coment za BACHELONA na uandishi wake humu ndani na hata anavyoandika ukilinganisha na atamkapo wakati anaongea nimegundua "BACHELONA NI DQ WILBROAD SLAA" nakuombeni mfuatilie coment za slaa humu ndani unganisheni na Barca mtajua niko right au la.