Mama wa Mtoto Mwenye Kilo 251 Apandishwa Kizimbani

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
2373370.jpg


Mtoto Alexander Draper mwenye kilo 251

Mama mmoja wa nchini Marekani amepandikishwa kizimbani kwa kufanya uzembe na kupuuzia afya ya mtoto wake na kupelekea mtoto huyo kuwa mnene kuliko kawaida, kwani pamoja na kuwa na umri mdogo wa miaka 14 mtoto huyo ana uzito wa kilo 251 . Katika kesi hiyo ambayo imekuwa gumzo nchini Marekani mama huyo mkazi wa South Carolina, Jerri Gray mwenye umri wa miaka 49 anatuhumiwa kufanya uzembe na kupuuzia afya ya mtoto wake wa kiume na kupelekea mtoto huyo awe na kilo 251 akiwa na umri wa miaka 14.

Jerri Gray ameachiwa kutoka jela kwa dhamana ya dola 61,000 lakini bado yupo kwenye kupigania kujumuika na mwanae Alexander Draper ambaye alichukuliwa na maafisa wa ustawi wa jamii.

Mahakama iliambiwa kwamba mama huyo alikimbia na mtoto wake pindi baada ya maafisa wa ustawi wa jamii kumfikisha mahakamani wakitishia kumnyang'anya mtoto wake.

Polisi walifanikiwa kugundua sehemu aliyokuwa amejificha baada ya kufuatilia simu zake alizokuwa akiwapigia marafiki zake.

Mama huyo alikamatwa na kupandishwa kizimbani huku mtoto wake akichukuliwa na maafisa wa ustawi wa jamii.

Mama huyo alijitetea kwamba kama asingelazimika kufanya kazi mbili basi hali ya mtoto wake ingekuwa tofauti.

Mama huyo alidai kuwa alikuwa hana uwezo wa kugharamikia matibabu ya mtoto wake huyo 'Kibonge' mwenye uzito wa kilo 251 hivi sasa.

Kesi ya mama huyo imewavutia watu wengi sana nchini Marekani huku baadhi ya wapiga picha wakichukua video za mama akitoka jela kwa nia ya kutengeneza documentary itakayohusu maisha ya mtoto wake.

Mtoto huyo bado yupo kwenye uangalizi wa maafisa wa ustawi wa jamii.


Source: nifahamishe.com
 
He! siye uko Afrika tuna watoto teleeee wa mitaani na wazazi wao,seuze kujishughulisha na wellfare ya jamii kama wenzetu hawa, Ustawi wa Jamii wetu sijuwi wanastawisha nini?
 
Hizo kilo balaa miaka 14 kilo 251 ??? anamlisha nini au ni ugonjwa huu...heri mimi mkondefu.
 
Hizo kilo balaa miaka 14 kilo 251 ??? anamlisha nini au ni ugonjwa huu...heri mimi mkondefu.

Mkuu si unajua tena hata ulafi ni dhambi. Marekani kuona watu wanene si kitu cha ajabu awe mtoto, mzee, mweusi, mweupe yani kazi. Obesity rate ya Marekani ni kubwa.
 
Huyu mtoto amekuwa obese kwa sababu ya umasikini wa mama yake wa kutokula nutritional food ktk uwiano unaotakiwa..

Sasa sijui hapa kosa ni la nani? mama ? ustawi wa jamii? au society ? na pia kuendelea kumtia jela huyu mama kutasaidiaje afya ya mtoto wakati maji tayari yameshamwagika?
 
Huyu mtoto amekuwa obese kwa sababu ya umasikini wa mama yake wa kutokula nutritional food ktk uwiano unaotakiwa..

Sasa sijui hapa kosa ni la nani? mama ? ustawi wa jamii? au society ? na pia kuendelea kumtia jela huyu mama kutasaidiaje afya ya mtoto wakati maji tayari yameshamwagika?
Unaonaje wakimpeleka huyu mtoto mtaa tandika/mazense alelewe na mama wa kibongo mtaa wa uswazi chai mandazi na mihogo (asubuhi na jioni) halfu shule km tatu sita kwenda na kurudi kwa miguu!!..only two years jamaa kilo kama yangu chin ya 60!!! just suggest kulikokumpeleka ustawi wa jamii.
 
Unaonaje wakimpeleka huyu mtoto mtaa tandika/mazense alelewe na mama wa kibongo mtaa wa uswazi chai mandazi na mihogo (asubuhi na jioni) halfu shule km tatu sita kwenda na kurudi kwa miguu!!..only two years jamaa kilo kama yangu chin ya 60!!! just suggest kulikokumpeleka ustawi wa jamii.

SORRY thats is not scientific way of dealing with this problem!
 
hapa ndio utaona tofauti ya siasa na uchumi tunaohubiliwa na wamarekani na utekelezaji wa siasa hizo, uwaga wanapiga kelele kwamba serikal ktk nchi za kiafrica zijitoe ktk mambo yote ya huduma za bure na mambo ya uchumi, na kweli serikali zetu zinafata hhayo maelekezo ya kibwege, lakini wao wamarekani wapo makini sana na mambo yao, raia mmoja wa ,marekani ana thamani kubwa sana na serikali kwa kweli inmfatilia mno, lakini huku kwetu thamani ipo kwa wenye pesa tu, kuna maskini na vilema wa kila aina, lakini serikali inashindwa hata kuwasaidia, hivi hii issue ya kuua albino mimi naona serikali inafanya kama mchezo wa kuigiza tu,
Matonya amekuwa ni kama kichekesho tu, lakini ukimuangalia ni mtu mzima(mzee) ambaye serikali ingepaswa kumsaidia kwa njia moja ama nyingine kuliko kwenda kumdump dodoma sasa sijuhi akale mawe?
 
SORRY thats is not scientific way of dealing with this problem!
There are different ways of handling the problems, this is one of the options?? do you believe that every problem can be solved scientifically?
 
There are different ways of handling the problems, this is one of the options?? do you believe that every problem can be solved scientifically?

This kind of problem needs a scientific approach .. NUKTA.
 
Back
Top Bottom