Mama wa kambo kaniharibia kila kitu

Alikua anathamini watoto wake kuwarithisha elimu kuliko mambo mengine. Ndugu wengine walikua hawajikita sana huko ndio kisa chakutengwa
Ooh basi sawa, kama upo Dar nita kulink kwa mtu flani kikubwa uwe na ushahidi wote wa chuo mpaka death certificate ya mzee, ikiwa bahati yako utasaidika, ni kumuomba Mungu tu.
 
Ooh basi sawa, kama upo Dar nita kulink kwa mtu flani kikubwa uwe na ushahidi wote wa chuo mpaka death certificate ya mzee, ikiwa bahati yako utasaidika, ni kumuomba Mungu tu.
Ndio nipo Dar
Nitashukuru
 
Mimi na mama wa kambo hatuna bifu kwakuwa sijawahi onesha dalili za kutaka mali yoyote. Mzee bado yupo sana na kwake hata sipajui, mali zake sizijui sasa nitadai nini.
Nishaacha kumuomba mzee lolote na hata hatuwasiliani tena, ada mwenyewe sijamalizia lakini naamini itaisha bila tatizo.
Mzee nimesave namba yake ili akinitafuta nisiulize 'we nani?'
Muhimu kwangu, nina strong bond na ukoo. Sasa ole wake mzee mimi niwe Naseeb, yeye ndo atakuwa mzee Abdul.
 
Ndo mana unaambiwa fuatilia mahakamani.kwani wewe sio mtoto halali wa marehemu?kama aliwekeza kwenye elimu sasa aliwekeza nini?kwa njia gani?ili hali sasa unapata shida.

Ni kweli baba alikuwa anaumwa mpka umauti unamkuta,nakupa pole kwa hilo mkuu.lkin hata kiwanja hana,alikuwa hafanyi kazi?kwanini hakukugawia japo kiasi kidogo wakati yuko hai ili hali wewe ni mwanae na huyo mwanamke sio mama yako mzazi?

Comment zako nikizisoma nipata ukakasi sana.
Pole kwa kuondokewa na mzazi uliyekuwa unamtegemea na pole kwa changamoto unazopitia.
 
Kwa hiyo hukushirikishwa wakati wa ugawaji mali? Baada ya msiba kumalizika hamkukaa kikao kujadili suala la mirathi? Nani alichaguliwa kusimamia mali zilizoachwa na marehemu?
 
Halafu ingekuwa vizuri thread kama hizi mnakuja na utambulisho halisi.
Mfano mimi John Frank mwanafunzi wa mwaka wa 2 chuo kikuu UDSM college ya ÙDBS nikichukua BCOM.
Unaweza ku-upload student ID, selfie(passport size) etc.
Sasa wadogo zetu mnataka msaidiwe ila identity zenu mnajifisha .
 
Pole sana mkuu ndo dunia ilivo
ila mzee wako naweza sema alikosea kujitenga na ndugu zake na kuwa mbinafsi(kulingana na maelezo yako) sasa hapo nizamu yako kutengwa pia na ndugu wa mzee wako.
tukibarikiwa kuwa na chochote tujitahidi kufikiria na kesho yetu na familia zetu
 
pole kabla ya kufatilia miradhi nikuulize hvi kwani mama ako mzazi alifunga ndoa na baba ako?ama we ni mtoto wa kambo kivipi? pia mama ako wa kambo alifunga ndoa (? kwa watoto wa kambo kama mi tusipo pewa urithi na baba zetu huwa ni tabu sana maana ata sheria aitutambui
 
Kaa chini kila siku lia kwa sanaaa na kila kitu kitaenda vizuri.
 
Mimi nitakushauri kisheria nenda kaongee na ndugu wa baba yako muitishe kikao cha familia ukatengue uteuzi wa usimamizi wa mirathi ma mali zigawanywe upya kama bado zipo..ingawa utachelewa chuo kama vipi ahirisha masomo fanya mchakato huo mkuu
Hili kisheria linawezekana kabisa
 
Nenda kwenye vyombo vya sheria au kwa mfumo wa sasa piga shortcut nenda kwa mkuu wa wilaya au mkoa.

Angalizo:Utakapofanikiwa heshimu mali za mzazi wako ziendeleze miaka mitano ijayo watu watataka mrejesho.
 

Siku ukijua umepoteza na ukaamini umepoteza utakuwa na uwezo wa kupata kila kitu na zaid ulivyopoteza
 
Mkuu umesema baada ya mambo yote kuisha kunabaadhi ya Mali ziliingia kwenye mkono wa mama wa kambo, nani alimkabidhi?au alijichukulia tu kienyeji? maana taratibu za ugawaji mali za marehemu unafanyika pindi msiba unapoisha , ndugu wa marehemu wanakaa pamoja na kila kitu hugawanywa kwa utaratibu fulani
 
Da inasikitisha ,ila usikalili kuwa kila mama wa kambo ni mbaya,inawezekana ulimkwaza mahali muombe radhi muendelee na maisha, mama wakambo wenye ubinadam wapo
mama wa kambo akifika stage hii hapo huyo ni mnyama wazazi wetu tunawakosea sana mbona hawafanyi hivi
 
Mkuu mimi huyu mama wa kambo sikuwa na habari naye mpaka mzee aliponiacha kwasababu mambo mengi alikua akifanya mzee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…