Mama Samia Suluhu Hassan alindwe Afya yake

Mama Samia Suluhu Hassan alindwe Afya yake

Lord Denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
23,494
Reaction score
57,871
Amani iwe nanyi.

Naona kuna upuuzi washauri na wasaidizi wa Rais wetu mama yetu Samia Hassan Suluhu wanataka kuufanya kwa mama yetu, nao ni kumuweka kwenye risk ya kupata maambukizi ya ugonjwa huu hatari wa corona. Hawampi barakoa na pia wanamuacha ashikane mikono na watu. Nasema hapana.

Sote tumeona jinsi gani corona ilivyopiga top layer ya Magufuli kutokana na watu kujitoa tu ufahamu na kupuuzia tahadhari za msingi na kitaalamu. Hata Kama Magufuli alikuwa na Tatizo la moyo, naweza sema kuna uwezekano mkubwa kuwa infection ya corona imechangia sana kupelekea kupatwa na Tatizo lililompata kutokana na kuleta complications kwenye mfumo wake wa umeme wa moyo.

Ni wakati sasa Mama yetu alindwe afya yake Kwa sababu nae ni mtu mzima (above 60). Apewe barakoa kwenye mikusanyiko na asiruhusiwe kushikana au kusogeleana na mtu. Walinzi wake nao wawekewe utaratibu maalumu wa kuepuka kupata maambukizi ili wasimuambukize.

Mwisho nitoe pongezi za dhati Kwa Rais wetu wa sita, Mama Samia Suluhu Hassan. Kwa kifupi ushauri wangu kwako kwenye maeneo ya kubadirisha na kurekebisha

1. Endelea kuanzia pale alipoishia JK kwenye uwekezaji na biashara. Wawekezaji na uwekezaji ndo vipewe kipaumbele cha kwanza kwenye sera zako za uchumi. Kamwe usiruhusu wawekezaji wapate madhira na unyanyasi waliopata kipindi cha msaidizi wako

2. Rekebisha sekta ya utoaji Haki. Ondoa unyanyasi mkubwa uliogubika sekta hii kwenye utawala wa Mtangulizi wako. Waliohusika watoe wote na weka wapya wenye mawazo na mlengo wa kuhudumia watu kwa haki na wala sio kwa uonevu.

3. Kwenye mipango miji na ardhi. Wekeza sana kwenye upimaji wa ardhi na mipango miji. Rekebisha uchafu ulioenea kwenye miji yetu. Wamachinga wasinyanyaswe ila wawekwe kwenye maeneo yenye mzunguko wa watu na kuwekekewa mazingira mazuri ya biashara huko.

4. Ondoa tatizo kubwa la ukabila na ukanda lililokuwa limeifunika nchi. Najua wajua kuwa kuna watu walishajimililisha hii nchi.

5. Miradi ya Umeme ( Stigglers) na Treni(SGR) imalizie Ila hakikisha mradi mkubwa wa Kiuchumi wa Bandari ya Bagamoyo unaanza maana hii ndo itakuwa mlango wa Tanzania kutoka kiuchumi.

6. kwenye ulinzi na usalama hatujawai kuyumba hapo tupo vizuri ila ondoa wanasiasa kuvitumia vikosi vyetu vya ulinzi na usalama kwa maslahi yao.

7. Usiruhusu Biashara yeyote kufungwa Kwa sababu ya madai ya kodi. Iboreshe na kuifumua positively TRA. Wajikite kuwa taasisi rafiki na wafanyabiashara na wala sio kikwazo cha biashara na uwekezaji. Pia taasisi nyingine za serikali zinazohusika na biashara na wafanyabiashara wapewe maelekezo kuwa sasa rasmi wawe wafanikishaji no 1 wa biashara na uwekeaji ili kutengeneza ajira nyingi kwa vijana wetu


8. Kwenye nishati na madini boresha zaidi na ondoa mkanganyiko na misuguano na wawekezaji. Sheria tulizotunga mwaka 2017 sio mbaya ila ifanywe harmonization kuepuka migogoro na makesi na wawekezaji. Ongeza uwazi zaidi kwenye sekta hii na hakikisha miradi mikubwa ya gesi inaanza

9. Mahusiano ya Kimataifa. Hapa mtangulizi I wako aliharibu sana. Boresha sana eneo hili wala usiliache nyuma. Hapa unaweza pata hela nyingi na ukazifanyia mambo makubwa sana kwa usimamizi mzuri utakaouweka.

10. Weka uhuru wa vyombo vya habari na raia kwenye kutoa maoni. TCRA wajikite kuboresha biashara ya mawasiliano na telnolojia na wasiwe chombo cha kufikisha watu mahakamani na kunyima watu uhuru wao wa mawazo. Wawe regulatory authority.

Kila la kheri Mama.
 
Mwambie pia na sisi watumishi wa umma tunamchora tu! 🙄 Akiendekeza itikadi za mtangulizi wake za kutumia hela zetu za kupandishwa madaraja kununulia bombardier, basi ajue na yeye tutamuandama na kumlaani mpaka kifo.

Ni mwaka wa sita huu tunaishi kwa mishahara na madaraja yale yale! Jambo ambalo ni la kichokozi, dhuluma na lililo jaa uonevu usio pimika!
 
Mwambie pia na sisi watumishi wa umma tunamchora tu! 🙄 Akiendekeza itikadi za mtangulizi wake za kutumia hela zetu za kupandishwa madaraja kununulia bombardier, basi ajue na yeye tutamuandama na kumlaani mpaka kifo.

Ni mwaka wa sita huu tunaishi kwa mishahara na madaraja yale yale! Jambo ambalo ni la kichokozi, dhuluma na lililo jaa uonevu usio pimika!
Hili najua atalifanyia kazi. Watumishi msihofu. Huyu ni Mama.
 
Mlinzi wa kwanza wa Afya yake ni yeye mwenyewe... Sa kama Madame SSH mwenyewe hajiongezi hata wamlinde na mavifaa mengi mengi kama kipindi cha JPM ni kazi buree.
Mwambieni ukweli...
Kisayansi viruses wapo... Madaktari na wataalamu wa afya tunao!
Na WHO ni shirika la kimataifa...
So miongozo ya kisayansi ifuatwe...
Tuheshimu taaluma za watu...!!
 
asee unajua siamini kama bavicha watoto wa nyumbu ndo wamedevela hivi 😂😂😂😂😂 msnambie mmemsahau yule shoga kilema wa ulaya?

🎶🎶ccm ni ileeilee 💃💃🕺ooh ni ileilee📯🤸‍♂️
 
Kiongozi asiyejua kuhusu usalama wake mwenyewe huyo ni kama mbuzi.
Ndio maana kipo kitengo cha usalama na ni kipana kuliko unavyodhania ni vile mtangulizi wake alikifukia kwa kila alichosema ilikua sahihi mimi niliumia na sikuangalia alipokua anafungua Magu huko stand ya mbezi kipindi wave tuu imepamba Moto kupitia msumbiji na mtwara na wataalanu wetu walitulia kimya wakiaminishwa madudu na kuyakubali...
 
We are still celebrating demise na kuondoka kwa dictator japo silently as police are raiding on us kutushika.

Jana ninekunywa na kuwanywesha jamaa zangu sana bia kwa furaha, bia zilikuwa zaidi na utamu kutokana na furaha ya mauti ya dictator.

Dictator should go to hell.
Acha unafiki haya mambo yote yanayotokea mimi siwezi kuyaamini na wala sitokuja kuamini eti ni corona, kawadanganye wengine, nenda youtube huko kajiangalizie unabii.
 
Back
Top Bottom