Mama Samia Suluhu anaapishwa lini?

Mama Samia Suluhu anaapishwa lini?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,156
Reaction score
137,179
Ni baada ya muda gani ndo makamu wa Rais anaapishwa kuwa Rais baada ya Rais aliyepo madarakani kufa au kujiuzuru?

Mama Samia bado ni makamu wa Rais kwa sasa au keshakaimu Urais tayari?

Kama ameshakaimu Urais, rasmi anatambulikaje? Kaimu Rais hadi pale atakapoapishwa rasmi au?

Maswali ni mengi mno!
 
Si wamesema baada ya siku saba na tayari speaker kisha waita Wabunge waende Dodoma na kesho kutwa CCM wanakaa na kuchagua jina la makamu...
 
Ndani ya siku saba kwa mujibu wa katiba.
Na ingependeza zaidi iwe kabla ya kuzikwa Marehemu nchi haipaswi kukaa bila Mkuu wa nchi na amiri Jeshi mkuu kwa muda mrefu hata wa siku hizo saba.

Mind you hii ni tofauti na pale tunapokuwa tumetoka kwenye uchaguzi, Tunapotoka kwenye General election tunakuwa tunae Rais na wanabadilishana wakati wa kuapishwa lakini kwasasa ni kwamba kiti kipo wazi that is too bad.
 
Ni baada ya muda gani ndo makamu wa Rais anaapishwa kuwa Rais baada ya Rais aliyepo madarakani kufa au kujiuzuru?

Mama Samia bado ni makamu wa Rais kwa sasa au keshakaimu urais tayari?

Kama ameshakaimu urais, rasmi anatambulikaje? Kaimu Rais hadi pale atakapoapishwa rasmi au?

Maswali ni mengi mno!
Anaapishwa kabla hata ya mazishi.
 
Hata kama moderator mumefuta replay yangu nachojaribu ni kuwambia watu kwamba Tundu hatokuja kuwa raisi hata baada ya 2025 kosa langu liko wapi hapo ?
Sijatukana mtu ila natoa taarifa tuu
Ndio hata kuja kuwa raisi mfahamu hilo
 
Hata kama moderator mumefuta replay yangu nachojaribu ni kuwambia watu kwamba Tundu hatokuja kuwa raisi hata baada ya 2025 kosa langu liko wapi hapo ?
Sijatukana mtu ila natoa taarifa tuu
Ndio hata kuja kuwa raisi mfahamu hilo
Jikite Kwenye Mada, kutoka kumtetea Jiwe kwamba yuko fit mpaka kuja kuhamisha magoli.
 
Kwa mujibu wa Kigogo ni tarhe 25. Sijui kama ni kweli. Ila Samia kuapishwa itakuwa ni tukio dogo la watu muhimu, lisilo na shangwe ma popote wanapoona panafaa.
Aah tar 25 mbali sana, hebu wawe serious si nikuapa tu au Kuna kingine?
 
Back
Top Bottom