Mama hamtaki mchumba wangu

Mama hamtaki mchumba wangu

Siri mpe mama yako mapenzi mpe mke wako kaka wa mama wa siku hizi ni wakidigitali wewe kama mama hana 7bu za msingi za kumkataa mchumba wako wala usiumize kichwa nenda kaongee na wajomba zako pamoja na mama zako wadogo na wakubwa hao ndio wataweza msoma vizuri bimkubwa kua y anamchukia mrembo wako. Wama zetu nao ni shida tupu ukiwapuuza sana utawasikia nakupa radhi kuanzia leo mie sio mama yako na ukimuoa huyo sintokusamehe duniani wala mbinguni.
 
Hapo ndipo mgongano wa mawazo unapotokea. But nini sasa kifanyike?
Its not that easy to change her mind! na its not that easy for ur girl to accept the fact.
take time, talk to ur mom, change her though sio rahisi na it will need a lot of time but just u and ur GF be patient.

Mda unaenda and you need both (family bless *mom* and you need a woman you LOVE *this is very important*)

Good luck Buddy
 
Nitalifanyia kazi ... lakin braza.. kama anamchukia sasa hivi akiwa hana mimba...? Atamkubali akiwa anayo?
Na pia kama hamkubali... vikao vya ndoa vitafanyika kweli?
unahitaji kusimama na msimamo lakini pia utumie busara usimkwaze mama yako kiasi ya kwamba ataona unamdharau.Wakina mama wengi hupenda wajukuu na isitoshe kwa sasa bado hajamjua vizuri mkwewe.Kama una uhakika kwamba huyo mchumba wako hana tabia za ajabu ajabu ni suala la muda/wakati iwapo ataona hilo baadae atamkubali mkwewe.
 
Its not that easy to change her mind! na its not that easy for ur girl to accept the fact.
take time, talk to ur mom, change her though sio rahisi na it will need a lot of time but just u and ur GF be patient.

Mda unaenda and you need both (family bless *mom* and you need a woman you LOVE *this is very important*)

Good luck Buddy
Thanks man....
 
unahitaji kusimama na msimamo lakini pia utumie busara usimkwaze mama yako kiasi ya kwamba ataona unamdharau.Wakina mama wengi hupenda wajukuu na isitoshe kwa sasa bado hajamjua vizuri mkwewe.Kama una uhakika kwamba huyo mchumba wako hana tabia za ajabu ajabu ni suala la muda/wakati iwapo ataona hilo baadae atamkubali mkwewe.
Nitajitahidi kufanya hivyo... coz sitaki kimkwaza mama.. lakini sitaki pia kumuumiza mwanamke anae nipenda.
 
Lazima mama ana sababu za kumkataa;
Zaidi ya hapo atakuwa mke wako pekee yako;
jishauri, chukua hatua.
 
Mr jose.. uko right. I need to dig more deep.. mpaka nipate jibu sahihi ..na niweze kufanya maamuzi sahihi
Muhimu sana mkuu. mwisho wa siku tunatarajia kuishi na hawa watu muda mrefu kuliko tulioishi na wazazi wetu. usije kujaribu ku overlook chochote mkuu
 
Habari za asubuhi ndugu zangu, natumai mmeamka salama.

Lengo la kuleta hii mada ni kuomba ushauri kwa ajili ya jambo linalo nisumbua kwa muda mrefu.

Mimi ni kijana mwenye miaka 25, nimemaliza chuo miaka miwili iliyopita na namshukuru Mungu maisha yanaenda vizuri. Ndugu zangu nimekuwa kwenye mahusiano kwa miaka miwili na mchumba wangu. Tumesaidiana mengi na ameonesha mapenzi ya kweli kwangu kwani amejitoa kwa mengi nami nampenda sana kutoka moyoni.

Tatizo ni kwamba toka nilipomtambulisha kwa mama, mama ameonesha chuki waziwazi kwake. Nilijaribu kukaa na mama na kuongea nae lakini sasa hana sababu maalumu ya kumkataa.

Niliwahi kumuuliza pole pole lakini akasema kuwa hajisikii amani moyoni mwake kuhusu mchumba wangu. Nikamuuliza kwanini hajisikii amani? Akakosa jibu akanipotezea.

Sasa mchumba wangu ameumia mno kiasi kwamba anataka tuvunje mahusiano baada ya kujua mama hampendi. Kwakweli nimejaribu kila njia katika kusuluhisha hili jambo lakini naona naelemewa.

Ndugu wa mwanamke wananielewa sana na imetokea kwao wamenikubali sana, haswa mama yake na baba yaani wakiniona wanafurahi. Lakini mama yangu mimi hamtaki na hana sababu maalumu ya kumkataa.

Nifanyaje wadau? Naombeni ushauri wenu.
Unajua wanawake huwa wana kitu kinaitwa intuition kali sana, sasa mama kwa mtoto ni zaidi . Aidha kuna mtaalam mmoja aligundua body language inaongea zaidi ya 80%. Inawezekana kuna kitu mama amekigundua kwa mchumba wako ambacho wewe kwa mahaba huwezi kukigundua. Hata hivyo despite ya kusema hayo usimuache msichana unayempenda kwani wewe ndio utakuwa nae masaa 24 ya siku. Sasa nikupe ,fano mzuri kuna mtu mmoja very close to me ( sitamu-identify kwa privacy yake na ukizingatia amemaliza maisha yake hapa duniani)
Huyo baba miaka ya 50 ( 1950s) alimpenda binti wa mjini yeye alikuwa wa kijijini. Wazazi wake hawakutaka kabisa amuoe binti wa mjini na sababu walikuwa nayo nzuri tu( kwa perception yao) kuwa mabinti wa mjini ni wahuni nadhani walilinganisha na wakikjijini/ Huyo baba wakati huo kijana wa kama miaka 30 alisimamia msimamo wake wa kuoa bila ya wazazi wake kuhudhuria kisa hawamtaki mchumba aliyemchagua na walikuwa wamekwishamchagulia binti wa kijijini wa kumuoa. Kumbuka hii nimiaka ya 50. Harusi yake akahudhuria mjomba wake.
Harusi ilikuwa kubwa mnoo. Mke aliyemuoa hakuonyesha chuki wala kinyongo chochote kwa mama mkwe wake akama alivyosema mwenyewe ' alimuelewa concerns zake' . Wote walikuwa wafanyakazi baada ya mwaka wakawa na mtoto wao wa kwanza wakachukua likizo wakaenda kijijini kwa mume wake. Huyo binti wakati huo akiwa na mtoto mmoja tu akajitahidiku-cope maisha ya kijijini, akawa anaenda teka maji pamoja na wake wenzie. Alisomea docmestic science na kushona alienda na vitambaa vi-3 vya gauni na aleinda na cherehani ya mkono ( mh Vijana jamani msije bisha zilikuwepo) akamshonea mama mkwe wake nguo na walimualika kwenda kuwatembeleea ila by the time anaondoka walikuwa wamekwisha elewana. Alipowatembelea walipokuwa wanafanyia kazi alijitahidi kumpa upendo mkubwa mama mkwe wake. Sasa je angechukulia kuwa kwa kuwa hanipendi basi na mimi simpendi ingekuwaj?
Waliweza kuishi na ndugu wa pande zote mbili na kuwazika wazazi wao wa pande zote mbili iKufupisha story waliishi miaka 57 ndani ya ndoa na walifanikiwa kupata watoto zaidi ya sita na waliweza kuwasomesha woote kwa level ya degree na kuweka mahusiano mazuri sana kwa pande zote mbili. Kifo ndio kimewatenganisha na naamini kwa sasa wako pamoja huko kwa Mungu.
Pendekezo: Mchumba wako asiweke kinyingo. kama mchangiaji mmoja aliyesema hapo juu kawivu kakiasili kapo , yeye aonyeshe upendo tu atamzoea tu na kumpenda asimuonyeshe kinyongo. Asikuache kwa ajili ya mama mkwe, amekupenda wewe ampende na mama mkwe wake a.k.a Mzaa Chema jinsi alivyo.
 
Unajua wanawake huwa wana kitu kinaitwa intuition kali sana, sasa mama kwa mtoto ni zaidi . Aidha kuna mtaalam mmoja aligundua body language inaongea zaidi ya 80%. Inawezekana kuna kitu mama amekigundua kwa mchumba wako ambacho wewe kwa mahaba huwezi kukigundua. Hata hivyo despite ya kusema hayo usimuache msichana unayempenda kwani wewe ndio utakuwa nae masaa 24 ya siku. Sasa nikupe ,fano mzuri kuna mtu mmoja very close to me ( sitamu-identify kwa privacy yake na ukizingatia amemaliza maisha yake hapa duniani)
Huyo baba miaka ya 50 ( 1950s) alimpenda binti wa mjini yeye alikuwa wa kijijini. Wazazi wake hawakutaka kabisa amuoe binti wa mjini na sababu walikuwa nayo nzuri tu( kwa perception yao) kuwa mabinti wa mjini ni wahuni nadhani walilinganisha na wakikjijini/ Huyo baba wakati huo kijana wa kama miaka 30 alisimamia msimamo wake wa kuoa bila ya wazazi wake kuhudhuria kisa hawamtaki mchumba aliyemchagua na walikuwa wamekwishamchagulia binti wa kijijini wa kumuoa. Kumbuka hii nimiaka ya 50. Harusi yake akahudhuria mjomba wake.
Harusi ilikuwa kubwa mnoo. Mke aliyemuoa hakuonyesha chuki wala kinyongo chochote kwa mama mkwe wake akama alivyosema mwenyewe ' alimuelewa concerns zake' . Wote walikuwa wafanyakazi baada ya mwaka wakawa na mtoto wao wa kwanza wakachukua likizo wakaenda kijijini kwa mume wake. Huyo binti wakati huo akiwa na mtoto mmoja tu akajitahidiku-cope maisha ya kijijini, akawa anaenda teka maji pamoja na wake wenzie. Alisomea docmestic science na kushona alienda na vitambaa vi-3 vya gauni na aleinda na cherehani ya mkono ( mh Vijana jamani msije bisha zilikuwepo) akamshonea mama mkwe wake nguo na walimualika kwenda kuwatembeleea ila by the time anaondoka walikuwa wamekwisha elewana. Alipowatembelea walipokuwa wanafanyia kazi alijitahidi kumpa upendo mkubwa mama mkwe wake. Sasa je angechukulia kuwa kwa kuwa hanipendi basi na mimi simpendi ingekuwaj?
Waliweza kuishi na ndugu wa pande zote mbili na kuwazika wazazi wao wa pande zote mbili iKufupisha story waliishi miaka 57 ndani ya ndoa na walifanikiwa kupata watoto zaidi ya sita na waliweza kuwasomesha woote kwa level ya degree na kuweka mahusiano mazuri sana kwa pande zote mbili. Kifo ndio kimewatenganisha na naamini kwa sasa wako pamoja huko kwa Mungu.
Pendekezo: Mchumba wako asiweke kinyingo. kama mchangiaji mmoja aliyesema hapo juu kawivu kakiasili kapo , yeye aonyeshe upendo tu atamzoea tu na kumpenda asimuonyeshe kinyongo. Asikuache kwa ajili ya mama mkwe, amekupenda wewe ampende na mama mkwe wake a.k.a Mzaa Chema jinsi alivyo.
Dah braza umegusa penyewe... asante kwa huu ushauri.. nitaufanyia kazi
 
Habari za asubuhi ndugu zangu, natumai mmeamka salama.

Lengo la kuleta hii mada ni kuomba ushauri kwa ajili ya jambo linalo nisumbua kwa muda mrefu.

Mimi ni kijana mwenye miaka 25, nimemaliza chuo miaka miwili iliyopita na namshukuru Mungu maisha yanaenda vizuri. Ndugu zangu nimekuwa kwenye mahusiano kwa miaka miwili na mchumba wangu. Tumesaidiana mengi na ameonesha mapenzi ya kweli kwangu kwani amejitoa kwa mengi nami nampenda sana kutoka moyoni.

Tatizo ni kwamba toka nilipomtambulisha kwa mama, mama ameonesha chuki waziwazi kwake. Nilijaribu kukaa na mama na kuongea nae lakini sasa hana sababu maalumu ya kumkataa.

Niliwahi kumuuliza pole pole lakini akasema kuwa hajisikii amani moyoni mwake kuhusu mchumba wangu. Nikamuuliza kwanini hajisikii amani? Akakosa jibu akanipotezea.

Sasa mchumba wangu ameumia mno kiasi kwamba anataka tuvunje mahusiano baada ya kujua mama hampendi. Kwakweli nimejaribu kila njia katika kusuluhisha hili jambo lakini naona naelemewa.

Ndugu wa mwanamke wananielewa sana na imetokea kwao wamenikubali sana, haswa mama yake na baba yaani wakiniona wanafurahi. Lakini mama yangu mimi hamtaki na hana sababu maalumu ya kumkataa.

Nifanyaje wadau? Naombeni ushauri wenu.
Dogo mimi nilikuwa na tatizo kama lako. Ila mama yangu alinipa sababu kuwa hataki nioe mchagga (alikuwa mchaga) kwa kuwa aliamini Mwanamke wa Kichaga hawezi kumjali yeye na ndugu zangu. Mama yangu aliamini kwenye family zaidi, na mimi nililelewa kifamilia zaidi huku ndugu zangu masikini walikuwa wakinichangia kidogo walichonacho ili mimi niweze kwenda shule na kuwa mtu bora kama nilivyo leo. Mafanikio yangu, Mama yangu aliamini na ndivyo ilivyo yalitokana na michango midogomidogo ya masikini dada zangu hivyo basi kuolewa na mwanamke atakayekosa kulielewa hili ni mtihani mkubwa kwa familia kwakuwa nilikuwa ninatakuwa kwakiasi kikubwa kuchangia kushiriki kuondoa umasikini na ndo maana familia iliamani wakinisomesha mimi na kufikia nilipofikia ningeweza kifikia lengo hilo ambalo nimelitimiza kwa kiasi kikubwa. Kwa kulielewa hilo na kumwelewa mke wangu kwa wakati ule akiwa mchumba kwanza sikutaka ku stereotype kuwa wanawake wote wa Kichaga hawapendi familia ya mwanaume. My instincts ziliniambia kuwa yule mwanamke alikuwa unique na hawazi kufanya hivyo na ndivyo ilivyokuwa hadi leo. Nilimshawishi mama na ilibidi nimtumie wazee wa heshima kijijini kwetu kuniombea kwa mama na kumshawishi akubalian nami na finally ilikuwa hivyo.

Kwako sasa, jitahidi kujua sababu za kwa nini mamako hamtaki huyo mwanamke. Ukishajua, umshawishi mamako kuwa mke unayetaka kuoa si wa aina ambayo yeye anaifikiria. Akishindwa kukupa sababu za kwanini hamtaki, mhakikishie kuwa mchumba wako atakuwa mwanake bora atakayemjali yeye na familia kwa jumla kama huo ni wasiwasi wao. Ikishindikana pia tumia wazee ambao mama yako anawaheshimu na kuwasikiliza ili wamshawishi, wazee ni dawa. Chukua nafasi hiyo pia kumfahamisha mchumba wako juu ya hilo na nini wewe unategemea yeye a behave atakapokuwa mke ili aweze kum prove wrong mamako na hatimae wawe marafiki watakaoishi kwa amani na upendo. Mwenzako mama yangu na mke wangu walikuwa marafiki sana kiasi cha kulala kitanda kimoja mke wangu anapotembelea kijijini kwetu peke yake. Mke wangu alimlea, kumuuguza na kumzika mamangu kwa heshima na taadhima na alipata radhi za mkwe. Kwahiyo uwe imara juu ya hili, uwe jasiri na ulisimamie na uwe na ushawishi kwa mama na mchmba wako. Kwenye jambo la kheri has la ndoa mambo huenda kikherikheri. Mungu akubariki sana kwa jambo hili la kheri na akufanyie wepesi juu ya hili ili unachokihitaji kama kina kheri nawe basi kifanikiwe kwa urahisi kwa mapenzi yake lakini usifosi. Angalizi: Mchumba wangu wa kwanza ilishindikana kutokana na tofauti za dini ingawa alikuwa mwema sana alkini ilishindikana mamangu alikataa katakata na nilimsikiliza. Aliniambia kuwa baba, pamkoja na kuwa mchumba wako ni mwema sana kwetu lakini suala la dini ni zito, nakuomba uangalie uwezekana wa kuachana naye kwa wema na Mungua takupa tu mwanamke mwingine aliyemwema kama huyu na wa dini yako, na kweli nilimskiliza mama na ndivyo ilivyotokea. So usipush sana ukiona mama hataki kabisa ujui si vyema kufosi, wanawake wema bado wapo wengi na utapata yule ambaye mamako atamridhia. Kila la kheri.
 
Ndoa ni makubaliano ya watu wawili ambao wamepatana kuishi pamoja. Watu wengine ni pande ya tatu ya uhusiano wenu (third party). Nashauri umsikilize mama yako anachosema na kaa nae kama asiporidhika basi achana na huyo binti ili usimuudhi mama yako maana laana ya mama ipo na kama mtu amekuleta duniani kwa uchungu na afurahishwi na maamuzi yako basi ni sawa na laana wala usilazimishe wazazi haswa mama ni Mungu wa duniani msikilize
 
Mara nyingi wamama hawa wanakuwa na wivu kwa watoto wao wa kiume...utakuta ni wivu tu unamsumbua.
sasa wivu kwa mwanae ina maana anataka mtoto awe anambandua huko chini au??hee wamama jirekebisheni
 
sasa wivu kwa mwanae ina maana anataka mtoto awe anambandua huko chini au??hee wamama jirekebisheni
Noo haihusiani na kumbandua...anakuwa tu insecure. Anahisi atamkosa kwa muda anaotaka,au ata-base kwa wakwe zake zaidi...
 
Noo haihusiani na kumbandua...anakuwa tu insecure. Anahisi atamkosa kwa muda anaotaka,au ata-base kwa wakwe zake zaidi...

ila ni kweli...wababa wanapenda sana mabinti zao na wamama wanawapenda vijana wao wa kiume
 
Jay_the_analyst,
Swala la ndoa lina mambo mengi tunaweza kuangalia kama ifuatavyo:-
1.Kuna baadhi ya wazazi huangalia makabila Au koi Fulani,hivyo mtu kukataa kuoa/kuolewa na Kabila Au koo kutokana na sababu za kihistoria,hadithi Nk
2.Kuna baadhi huangalia malezi hapa kuna wigo mpana kidogo wengine huangalia mahusiano ya wazazi wenza nk,kuna familia mtoto wa kike kalelewa bila baba au mama hivyo huwa na tabia fulani kutokana na mazingira hayo e.g.,kutojua sauti ya mwanamme ndani ya nyumba,wengine kukosa huruma ya kimama etc
3.Mtoto kuwa na msaada chanya kwa familia hii humuogofya mzazi kupungua kama si kukatika kwa misaada hiyo pindi tu atakapoazisha himaya yake,wazazi wengine huamua kumpangia mtoto mke wa kuoa akiamini atakuwa anamuheahimu mama/mzazi kana kwamba kuwa ndio watakuwa wamemtafutia deal mwolewaji hivyo kumcontrol na kuwa na heshima kwao
4.Nafasi za kiuchumi katika familia hizi mbili.
5.Chuki binafsi
 
Kujibu maswali yako.. nianze na hili.
- nyumbani mimi ndie wa kwanza
-nyumbani tumezaliwa watatu, wakiume wawili ,wakike mmoja
-nimelelewa katika malezi ya baba na mama.. na but mostly mama kwa sababu baba alikuwa hakai nyumban mara nyingi kutokana na kazi yake.
-imani ya mpenzi wangu na mimi viko sawa, kwani wote huwa tunaenda kanisani pamoja.
-mpenz wangu ana swag zankawaida tu.. ni mtu muelewa sana.. alaf mpole but ana msimamo sana.
-mpenz wangu hakai mtaa mmoja na mimi
-kabila lake ni mkuria... mimi mchaga
-familia yangu na ya mpenzi wangu hawajawahi kugombana kwa sababu hawafahamiani na wala hawaja wahi kuonana.
-umri wa mpenz wangu ni 22.
MSIMAMO WA MCHUMBA UNAWEZA KUWA CHACHU YA MAMA KUSHINDWA KUINGIZA HOJA/AU REQUEST ZAKE KWANI MPAKA SASA WEWE NDIE UNAONEKANA NI MSAADA MKUBWA KWA FAMILIA MAMA ANAHOFU KUKATIKA KWA MRIJA
 
MSIMAMO WA MCHUMBA UNAWEZA KUWA CHACHU YA MAMA KUSHINDWA KUINGIZA HOJA/AU REQUEST ZAKE KWANI MPAKA SASA WEWE NDIE UNAONEKANA NI MSAADA MKUBWA KWA FAMILIA MAMA ANAHOFU KUKATIKA KWA MRIJA
Nimeshawahi kuwaza kitu kama hiko.. maybe hiyo ndio sababu kubwa lakini anakwepa kuniambia.

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Jay_the_analyst,
Swala la ndoa lina mambo mengi tunaweza kuangalia kama ifuatavyo:-
1.Kuna baadhi ya wazazi huangalia makabila Au koi Fulani,hivyo mtu kukataa kuoa/kuolewa na Kabila Au koo kutokana na sababu za kihistoria,hadithi Nk
2.Kuna baadhi huangalia malezi hapa kuna wigo mpana kidogo wengine huangalia mahusiano ya wazazi wenza nk,kuna familia mtoto wa kike kalelewa bila baba au mama hivyo huwa na tabia fulani kutokana na mazingira hayo e.g.,kutojua sauti ya mwanamme ndani ya nyumba,wengine kukosa huruma ya kimama etc
3.Mtoto kuwa na msaada chanya kwa familia hii humuogofya mzazi kupungua kama si kukatika kwa misaada hiyo pindi tu atakapoazisha himaya yake,wazazi wengine huamua kumpangia mtoto mke wa kuoa akiamini atakuwa anamuheahimu mama/mzazi kana kwamba kuwa ndio watakuwa wamemtafutia deal mwolewaji hivyo kumcontrol na kuwa na heshima kwao
4.Nafasi za kiuchumi katika familia hizi mbili.
5.Chuki binafsi
3 na 4 ndio namashaka nazo

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
 
Nimeshawahi kuwaza kitu kama hiko.. maybe hiyo ndio sababu kubwa lakini anakwepa kuniambia.

Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
SASA LA MSINGI KAMA INAWEZEKANA TAFUTA JINSI YA KUWAWEKA STABLE FINANCIALLY KIFAMILIA EITHER BUSINESS WISE AU KWA KUCHUKUA BAADHI YA MAJUKUMU KUWA YAKO KWA KIPINDI FULANI KWANI KWA AHADI NA FUFANYA KUWEKA MEMBER MWINGINE WA FAMILIA ESP WA KIKE ILI AWE NGUZO
 
Back
Top Bottom