WADAU WAKATI KILA MTU ANAONGEA KIVYAKE KUHUSU MADAI YA MADAKTARI HEBU TUANGALIE JINSI KAZI ZINAZOLIPA MNO HUKO MAREKANI KUWA NI ZA MADAKTARI WENGINE WANAFUATA. NAFIKIRI HUKU KWETU - TZ MAMBO NI KINYUME. WATU WANAWEZA CHANGIA KWA KULINGANISHA NA UCHUMI NA FINANCIAL RESOURCE LAKINI POINT HAPA NI KWAMBA INATAKIWA KWA RESOURCE TULIZONAZO TUTOE VIPAUMBELE KWA KADA MUHIMU
No. 1 Best-Paying Job: Anesthesiologists
Average Annual Pay: $234,950
Employees in Field: 33,310
No. 2 Best-Paying Job: Surgeons
Average Annual Pay: $231,550
Employees in Field: 42,340
No. 3 Best-Paying Job: Obstetricians and Gynecologists
Average Annual Pay: $218,610
Employees in Field: 20,540
No. 4 Best-Paying Job: Oral and Maxillofacial Surgeons
Average Annual Pay: $217,380
Employees in Field: 5,800
No. 5 Best-Paying Job: Orthodontists
Average Annual Pay: $204,670
Employees in Field: 5,040
Statistics! Statistics! Statistics!!!!!
Ukitumia takwimu vibaya unaweza kujiponza! hata kam utalinganisha na majirani zetu angalia GDP ya nchi hizo, angalia ukubwa wa Private sector, angalia historia ya sekta ya afya. Private Practices kwenye sekta ya afya inaukubwa na ushindani kiasi gani? vinginevyo tutakuwa tunalinganisha oranges and apples!
Tatizo la Tanzania siyo madai ya madaktari, au mfumo uliopo ni uwezo wa ukubwa wa uchumi kukidhi mahitaji yote ya kitaifa, kuanzia ulinzi, usalama, Public service na udogo wa wigo wa kodi kutokana na kuwepo kwa uwembamba wa sekta binafsi ya utabibu ambayo haitowi mbadala wa mishahara mikubwa kwa madaktari, na wanataaluma wengine. kwasababu nchi yetu siku si nyingi ilitoka katika ujamaa ambapo kila kitu kinafanywa na serikali, na kwa bahati mbaya sana mentality hii bado inaendelea na kila kukicha wanacnachi wanaamini kuwa matatozo yao yote yatatatuliwa na serikali. Ujamaa Legacy!
Kinachotakiwa kufanyika ni kubadilisha mtazamo, na wanasiasa wote CCM na hata hao CHADEMA waache kuwadanganya Watanzania kuwaambia kuwa mkinichaguwa matatizo yenu yatakuwa yamekwisha. WIGO wa UCHUMI NA KODI iliyopo Tanzania ya leo hawezeshi kuondoa matatizo yetu hata kam nia ipo.
Marekani wamekuwa huru tangu July 04 1776, lakini mpaka leo bado wanabishana kuhusu bima ya afya kwa wananchi wote. Ugua leo ukiwa Marekani, au Mungu apishe mbali yakukute yaliyomkuta Dkt. Ulimboka na upo Marekani na hauna Bima, Ukubwa wa Mshahara wa Dakatari wa Marekani hautakusaidia, kitakachokuokoa ni Bima yako ya Afya.
Serikali yetu inapaswa kutupia macho sekta hii na kuhakikisha kuwa vitendea kazi na kupanua wigo wa private practice kwa madaktari, lakini pia kuhakikisha hawa waliopo na hospitali zilizopo zinakidhi mahitaji ya sekta hii.
Na Watanzania kwa ujumla wanapata decent medical service kama civilized human beings.
Na nyie Madaktari hacheni siasa, fanyeni kazi, mkigoma watanzania wanakufa, mchawi wenu siyo serikali iliyopo madarakani au CCM. ni ukubwa wa Uchumi uliopo na hii si kwa Tanzania pekee yake, hata Marekani bado hili linawasumbua. Hata CHADEMA siku wakuja kutawala nchi hii Mungu apishe mbali, hawataweza kuwaongezea mishahara na kukamilisha kila kinachoitajika bila kufinya maeneo mengine ya Tanzania kama Elimu, Ulinzi, au Miundombinu, kwa hiyo tutumie hekima na Uzalenda Uchumi wa Tanzania tuliyonayo sasa hauwezi kubeba madai ya kila mmoja wetu, na kama mtu akija anakwambia hilo linawezekana anakudanganya kwani atakachofanya ni: He will rob Mwita to pay Mushi or vice versa, kumbukam kuwa hawawote ni Watanzania:-(
Msigome fanyeni kazi, siasa waachieni wanasiasa.
Na kwa kwale wanaopenda kujibu hoja kwa matusi na kebehi, uwanja upo wazi
🙂)))