Malema awahamasisha wanajeshi kudai haki zao.

Gumzo

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
211
7
Mwanaharakati wa kisiasa nchini Afrika Kusini Julius Malema, amewashauri wanajeshi wenye manung'uniko kujipanga vyema na kupigania kazi zao.

Malema aliyatoa matamshi hayo kwa wanajeshi wanaokabiliwa na makosa ya kinidhamu yaliyotokana na maandamano waliyoyafanya mwaka 2009 wakidai mishahara mizuri na mazingira bora ya kazi.

Kambi za jeshi leo ziliwekwa katika hali ya tahadhari kabla ya hotuba yake kwa wanajeshi hao, ikiwa ndio mara ya kwanza hatua kama hii kuchukuliwa tangu kumalizika kwa enzi ya ubaguzi wa rangi.

Bwana Malema ni mwanasiasa anayeibua mgawanyiko hapa. Hivi maajuzi alifukuzwa kutoka chama cha ANC na kwa sasa anafanyiwa uchunguzi kuhusiana na kashfa ya ufisadi.

Lakini hajaondoka ANC kimya kimya. Badala yake ametumia mauaji ya hivi maajuzi katika mgodi wa Marikana kuanzisha kampeni kali dhidi ya mabepari nchini Afrika Kusini na kutaka yafanyike mapinduzi ya kiuchumi.

CHANZO: GUMZO LA JIJI
 
"Mapinduzi ya kiuchumi"
This poem has to be continued . continued and continued (by mutabaruka)
 
i luv julius malema,a true son of africa...

 
Last edited by a moderator:
Angekuwa hapa Tz angeshapelekwa Mabwepande kushughulikiwa

Kama siyo Mabwepande hivi tunavyoongea tayari anachunguzwa sana na NPA watamuibulia likashfa kubwa tu

Malema ana kampeni kali ya kuhakikisha Zuma hapati fursa ya kugombea ngwe ya pili ya urais. Kwa hilo Zuma hayuko tayar . Na Zuma ni mjanja sana
 
i luv julius malema,a true son of africa...



Opportunist tu yule. Sema ni vizuri kuwa na watu kama hao ambao ni muhogo mchungu kwa watawala

Jana asema;
" ndo maana kukawa na mauaji ya Marikana kwasababu serikali inapanic bila sababu tangu lini mkutano ukawa ni tishio kwa usalama wa taifa"

Natumaini kama CCM itazingatia ujumbe wa aina hii basi itaepusha mauaji mengi
 
Last edited by a moderator:
Kama siyo Mabwepande hivi tunavyoongea tayari anachunguzwa sana na NPA watamuibulia likashfa kubwa tu

Malema ana kampeni kali ya kuhakikisha Zuma hapati fursa ya kugombea ngwe ya pili ya urais. Kwa hilo Zuma hayuko tayar . Na Zuma ni mjanja sana

Malema ndie alieplay part kubwa sana kuhakikisha zuma anakuwa mwenyekiti wa ANC na badae Rais wa South,malema ni tishio kwa zuma kwa kuwa ana ushawishi(kama mtikila angekua serious) na anaungwa mkono na watu wengi wenye maisha ya chini,wanamuona ni mwenzao na wako connected nae,
 
Kijana huyo ni moto wa kuotea mbali, nilibahatika kuangalia moja ya hotuba zake, kwa kweli UVCcm na Umoja wa Vijana Chadema mnapaswa kuangalia na kujifunza jinsi wenzenu ANCYL wanavyoendesha shughuli zao.
 
Opportunist tu yule. Sema ni vizuri kuwa na watu kama hao ambao ni muhogo mchungu kwa watawala

Jana asema;
" ndo maana kukawa na mauaji ya Marikana kwasababu serikali inapanic bila sababu tangu lini mkutano ukawa ni tishio kwa usalama wa taifa"

Natumaini kama CCM itazingatia ujumbe wa aina hii basi itaepusha mauaji mengi

 
Last edited by a moderator:
Malema yupo OK ANC ni sawa na Magamba yaani ni kama kaka na dada,Wameshindwa kuwawezesha weusi kuishi maisha bora.Maisha South Africa ni magumu sio mchezo akuna mjomba kule unaeweza kwenda na kuishi kwake kama hapa Tanzania,kule kila mtu na mwanae.kule kama una pesa ya kula unalala na njaa na unakufa,kodi ikiisha kule autupiwi vitu nje bali vinataifisha na mwenye nyumba ili aviuze apate kodi yake.Viongozi wa ANC wana utajiri uliopitiliza,wakati maelfu wanaishi kwenye vibada vya mabox na mabati
 
Malema ndie alieplay part kubwa sana kuhakikisha zuma anakuwa mwenyekiti wa ANC na badae Rais wa South,malema ni tishio kwa zuma kwa kuwa ana ushawishi(kama mtikila angekua serious) na anaungwa mkono na watu wengi wenye maisha ya chini,wanamuona ni mwenzao na wako connected nae,

Nachoweza kusema ni kwamba ndiyo Malema alimsaidia Zuma kumuangusha Mbeki lakini ni kwasabu Zuma alikuwa capable. Role kubwa was played by Zuma himself. Soma hiyo link hapa chini

http://www.flyafrica.info/forums/showthread.php?34888-Wikileaks-exposes-SA-spy-boss-Mo-Shaik
 
Hili swala la wanajesh kudai haki zao ni swala ambalo hata wanajesh wa JWTZ wanapaswa kulizingatia.wanahaki nyingi ambazo hazitekelezwi kabisa ama kuchelewa kutekelezwa,hii inaweza kuondoa hamasa kwa askar.Huwa najiuliza hiv hata wakuu wa mikoa,wilaya,mawazir nao huwa wanacheleweshewa mishahara,malipo ya uamisho n.k?Napata tabu sana kumeza hii kitu.big up malema
 
Nachoweza kusema ni kwamba ndiyo Malema alimsaidia Zuma kumuangusha Mbeki lakini ni kwasabu Zuma alikuwa capable. Role kubwa was played by Zuma himself. Soma hiyo link hapa chini

Wikileaks exposes SA spy boss Mo Shaik
Malema anaujua udhaifu mwingi wa zuma ndio maana hamuogopi na kila kukicha anamshambulia live...malema licha ya udhaifu wake anajua kufanya siasa,anajua wananchi wanataka kusikia nini ndio mana amekua akijizolea umaarufu mkubwa miongoni mwa watu wa tabaka la chini ambao ndio wengi,jz hizo nguvu na uwezo aliokua nao wakati ule ni kwa sababu alikua na timu imara nyuma yake ikiongozwa na juju,hivyo juu bado atabaki kuwa alama ya ushindi wa zuma dhidi ya mwanasiasa mkongwe msomi na mwenye maarifa mengi mzee mbeki.Jz kwa sasa timu yake ina marafiki zake wafanyabiashara wa kiasia wakiongozwa na mtuhumiwa wa rushwa shabir sheik ambae ni rafiki wakufa wa jz ambae alikua tayari kwenda jela na akaenda jel kweli ili kumnusuru rafiki yake jz kisiasa kwani kwenye kashfa iiyompeleka jela shabir jz pia alikua na mkono
 
Huyu jamaa ana msimamo na ari ya kutetea wanyonge,karibun ndio anaongoza movement za wafanyakaz migodin A.kusini.JE ANGEKUA CCM ANGESALIMIKA?
 
Malema anaujua udhaifu mwingi wa zuma ndio maana hamuogopi na kila kukicha anamshambulia live...malema licha ya udhaifu wake anajua kufanya siasa,anajua wananchi wanataka kusikia nini ndio mana amekua akijizolea umaarufu mkubwa miongoni mwa watu wa tabaka la chini ambao ndio wengi,jz hizo nguvu na uwezo aliokua nao wakati ule ni kwa sababu alikua na timu imara nyuma yake ikiongozwa na juju,hivyo juu bado atabaki kuwa alama ya ushindi wa zuma dhidi ya mwanasiasa mkongwe msomi na mwenye maarifa mengi mzee mbeki.Jz kwa sasa timu yake ina marafiki zake wafanyabiashara wa kiasia wakiongozwa na mtuhumiwa wa rushwa shabir sheik ambae ni rafiki wakufa wa jz ambae alikua tayari kwenda jela na akaenda jel kweli ili kumnusuru rafiki yake jz kisiasa kwani kwenye kashfa iiyompeleka jela shabir jz pia alikua na mkono
Nafurahishwa sana na ufahamu wako wa Malema. Hata hivyo the fact remains Malema hamuwezi Zuma.

Kama umefuatilia ile link mbona Zuma aliwakumbuka walomsaidia kwenye kampeni ya urais na siyo Malema?

Kingine ni kwamba ili uweze kuwa rais ni lazima upate support ya nchi za magharibi na umeona pale kwenye link jinsi Zuma alivyoorganise timu yake

Mwisho kulikuwa na watu wawili ambao inasemekana wangekuwa tishio kwa Zuma mwezi December huko Mangaung namely Nkosazana Dlamini Zuma na Motlante. Alichofanya Zuma ni kuhakikisha Nkosazana anapata ukatibu wa AU kwa gharama zote. Ashampangua adui wa kwanza. Huyu Motlante ndiyo tegemeo la Malema ukizingatia wote wanatoka Limpopo lakini hana ujanja wa kumshinda Zuma

Kwa nyongeza tu ile cabinet reshuffle Zuma aliifanya last time ilikuwa ni kujizatiti kwa kuwaweka maswahiba wake karibu come Mangaung December meeting
 
Kijana huyo ni moto wa kuotea mbali, nilibahatika kuangalia moja ya hotuba zake, kwa kweli UVCcm na Umoja wa Vijana Chadema mnapaswa kuangalia na kujifunza jinsi wenzenu ANCYL wanavyoendesha shughuli zao.

UVCCM na BAVICHA wanawaza madaraka tu,wote ni wachumia tumbo...Afrika itakombolewa na vijana wa kiAfrika endapo tukiamua kuungana na kushikirikiana pamoja kuondoa wakoloni.
 
Kuna kijana mmoja wa kisouth Afrika nipo naye masomoni huku ughaibuni anasema Malema ni pandikizi la Mbeki kuhakikisha wazulu (Zuma's tribe) hawapati nafasi awamu ya pili ya uongozi kuanzia ANC mpaka u-rais. Lakini huyu jamaa ni mzulu pia sasa naona kuna watu pia wanaomchukulia Malema kama mkabila na mwenye chuki zisizo na msingi kwa wazulu.Hasa ukizingatia kuwa Malema si Mzulu,pia anamu-accusse kwa ufisadi unaofanywa na makampuni yake ya contractors ambayo yanacheza faulo kwenye kugombea zabuni za ujenzi wa miundombinu mbalimbali ambayo mara zote yanashinda zabuni kwa rushwa,anaendelea kusema kuwa Malema si kweli kwamba anaushawishi kwa vijana bali ni kwa wale tu wenye ideologies za ubaguzi wa kikabila na wasio kuwa wazulu.
 
Malema yupo OK ANC ni sawa na Magamba yaani ni kama kaka na dada,Wameshindwa kuwawezesha weusi kuishi maisha bora.Maisha South Africa ni magumu sio mchezo akuna mjomba kule unaeweza kwenda na kuishi kwake kama hapa Tanzania,kule kila mtu na mwanae.kule kama una pesa ya kula unalala na njaa na unakufa,kodi ikiisha kule autupiwi vitu nje bali vinataifisha na mwenye nyumba ili aviuze apate kodi yake.Viongozi wa ANC wana utajiri uliopitiliza,wakati maelfu wanaishi kwenye vibada vya mabox na mabati

Malema yupo kama Zitto sema Zitto siyo mpayukaji. Malema anajifanya anatetea wanyonge wakati yeye ni filthy rich! Ana mansion in a rich people place inaitwa Sandton Jo'burg. Na jimbo analotoka hilo la Limpopo ndi jimbo maskini kuliko yote Afrika kusini

Kwa upande wake Zitto anajifanya kutetea wanye kipato cha chini wakati nyuma ya pazia anapiga mahela ya kufa mtu. Huku anajifanya anaishi maghorofa Tabata Bima. Tafakari ule mshahara tu wa wabunge kweli Zitto angeshindwa kufyatua matofali ya mfuko mmoja matofali arobaini au ndo he is trying to ingratiate himself with the poor to win their support?
 
Back
Top Bottom