Kwenye sekta ya elimu serikali iangalie kwa jicho la tatu, pesa inayopelekwa ni kidogo ukilinganisha na mahitaji ya shule husika, mfano shule inapelekewa sh 140,000 kama admistation cost maanake hapo wanunue vifaa vya kufundishia, walipe walinzi nk Ambapo pes hiyo haitoshi kabisa. Je hapo unategemea elimu kuwa bora au bora elimu?
Kingine mpango huu wa elimu bure haukuwa umeandaliwa mapema kutoka kwenye bunge la bajeti 2015/2016 hivyo shule zilikuwa na wazabuni wa huduma mbali mbali waliotoa huduma kwa shule hizo, mfano shule nyingi zina madeni kwa wazabuni mfano madeni ya kudurufu mitiani nk ambapo shule husika ilitegemea january makusanyo yakishakuwa mazuri kutoka kwa wanafunzi ilipe madeni, lakini sasa zinashindwa fanya hivyo kutokana na pesa inayopelekwa kuwa kidogo sana na vile vile kutokuwa na kifungu hicho. Hvyo serikali iangalie kwa jicho la pili juu ya madeni hayo make vinginevyo itasababisha mgogoro mkubwa baina ya shule na wazabuni