Makusanyo Januari kufikia Sh tril 1.5

Makusanyo Januari kufikia Sh tril 1.5

Mkuu hapa naomba ufafanuzi zaidi. Hizo pesa Tshs. 140,000/= ni matumizi ya mwezi na ni lazima zitumike, hivi Mkuu wa shule ataiba Shs. ngapi katika hizo? Umesema hizo pesa zitatimia kwa vipi na mahitaji ni ya kila mwezi?.
Nishule ipi iliyo pelekewa 140000
Na while muhimu hapo ni secondary
 
Ni kweli TZ ni tajiri sana.Kwa jinsi tunavyokwenda kwenye makusanyo nadhani ingekuwa busara tukajiwekea lengo la Trill.2.5 ili jamaa wasilale.Na lengo hili naamini linawezekana.Uvujaji wa mapato ulikuwa mkubwa mno.
Nakuunga mkono ndugu
 
Hao unaowaita nyumbu ndio wenye kazi nzuri kutokana na kisomo chao hivyo mishahara yao ni mikubwa na wanalipa kodi kubwa. Wengine wao ni wafanyabiashara wazuri sana kwa vile wanaakili hivyo wanalipa kodi kubwa sana na makusanyo yanaonekana.
Sasa wewe kuna kila dalili kuwa huna mchango wowote katika kuchangia mapato ya nchi hii na ni bora afugaye mbuzi anaweza kumkamua maziwa kuliko hasara ya kuwa na raia wa aina yako.
Hahaha Umepanic
 
Iv haya makusanyo ni mwezi mmoja yaani ya mwezi wa 1 tu au wanaongezea na zile ambazo walikusanya awali?
 
POROJO TUPU!
Nadhani kuna tatizo kubwa sana when it comes to usahihi wa taarifa. Mimi nilisikiliza taarifa ya habari na kuwasikia hao mabwana wa TRA wakidai kuwa lengo la makusanyo ya January 2016 ilikuwa ni shilingi trilioni moja na bilioni 45. Mpaka jana walikuwa wamekusanya trilioni moja na bilioni 31, na kwamba kufikia Jumatatu wanategemea kuvuka hilo lengo walilojiwekea.
Sasa naliona tatizo hapa kwa mwandishi wa habari hii: trilioni 1 na bilioni 45 sio sawa na trilioni 1 na bilioni 450...(1.045 trilion sio sawa na 1.450 trilioni).

Mods, rekebisheni hii taarifa, wengi watapotoshwa hapa
 
Hizi sindimba mbona zinakua kila kukicha..???

Hayo makusanyo SISI wananchii yanatuhusu nini??..
Wanatakiwa watupatie mipango ya maendeleo ya miaka mi5 kwakutegemea hizi pesa hewa wanazo turingishia kila mwisho wa mwezi.
Acheni maigizo sababu hayatusaidii chochote hasa hizo hotuba zenu za makusanyo ya kila mwezi
 
wale wakwepa kodi walikuwa wanafikiri mgombea wao atakuwa rais sasa wameula wa chuya cha muhimu hayo makusanyo yafanye kazi inayotakiwa
 
Hahaha Umepanic
Sio ku panic, bali huyo jamaa eti kwa akili yake anaona makusanyo kuwa makubwa ni kama kuwakomoa wapinzani. Utadhani hao wapinzani wanachangia kodi zao kwa serikali ya Msumbiji.
Hospitali zikipata pesa na kuboreshwa wanakwenda wote, mapato yakiwa mazuri na barabara zikitengemaa wanapita wote, sasa utaonaje kuwa hilo jambo mwingine kakomolewa?
Hizo ni akili zake matope tuu, maana mie naweza kuwa mfuasi wa Chadema na mama yangu akawa mfuasi wa CCM na mjomba ni ACT lakini wote tunafarijika na kazi ikifanyika ya kukusanya na wote tukapata huduma nzuri za kijamii.
 
Hongera Rais Magufuli.Tunaomba atenge shs bilion 4 kwa TBC ili wananchi tuendelee kupata habari kwa wakati muafaka.
 
Much as tungependa makusanyo yaongezeke hata kufikia trilioni mbili, lakini napenda kuwapa angalizo wana JF. Taarifa hizi, kama zilivyoripotiwa na gazeti la habari leo, sio sahihi. Mwandishi, pamoja na mwariri wake, wamechanganya mambo. Lengo la makusanyo lilikuwa trilioni 1 na bilioni 45, na mpaka taarifa inatoka zolishakusanywa trilioni 1 na bilioni 31. Wanatarajia kufikia Jumatatu wafunge mahesabu ya Januari wakiwa na zaidi ya trilioni 1 na bilioni 50.

Tatizo ni mwandishi kushindwa kutofautisha trilioni 1.045 likiwa lengo la Januari, na trilioni 1.4 (trilioni 1 na bilioni 400) zilizokusanywa December 2015.

Huu ndo ule ukanjanja unaozungumziwa kuhusu waandishi wetu walio wengi
 
Kweli Tz hamnazo nchi inaweza kukusanya zaidi ya trilioni 8 us$ 4billion minimum wanashangilia 1.5 na kujipongeza. Tuachane na siasa finyu,nchi hii ina rasilimali watu ,ina bahari pana tu,ina ardhi yenye rutuba ya kutosha kubwa tu,ina madini hata sisemi ,ya pili duniani kwa vivutio vya utalii,bandari ......halafu some loons wanasherehekea kukusanya 1.5tr. tatizo kubwa viongozi wetu wanautaka uongozi wakiupata hawajui waufanyie nini ndio maana mwingine anahangaika na kutumbua majipu.Una uwezo wa kupata mia unahangaika na 1.5? Naomba kazi TRA
 
Jakaya wakati anaingia Madarakani Serikali ilikuwa inakusana 170Bilioni.... Akaongeza hadi kufikia 900Bilioni.
Katika hizo, ni kiasi gani zilikuwa kwa safari zake na ufisadi wa mchana kweupe?
Tatizo lilikuwa hapo. Kodi ni kukusanya na matumizi mazuri
 
Back
Top Bottom