Maktaba yapokea Kitabu cha Vassanji kutoka Marekani

Maktaba yapokea Kitabu cha Vassanji kutoka Marekani

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
23,279
Reaction score
33,880
1777749328463.png

1777749373262.png

MAKTABA YAPOKEA KITABU CHA VASSANJI KUTOKA MAREKANI
Kwa wale waliokulia Kariakoo ya miaka ile akisoma kitabu chochote cha Vassanji ataiona ile Kariakoo ya enzi zetu na yote yaliyokuwapo miaka ile.

Niliijua kalamu ya Vassanji kwa mara ya kwanza Amsterdam nyumbani kwa dada yangu marehemu Haki Kilomoni.

Kwa kujua mapenzi yangu ya vitabu gumzo letu lilikuwa vitabu na yeye akaniambia kuwa akiwa na hamu ya kuikumbuka Kariakoo tuliyokulia husoma kitabu cha Vassanji: "And Home was Kariakoo."

Ndugu yangu huyu aliyenipa hidaya hii aliyeko mbali naamini kabisa na yeye akitaka kuikumbuka nyumbani anamsoma Vassanji.

Vassanji kaandika vitabu vingi na kingine kinachogusa Dar es Salaam kakipa jina, "Uhuru Street."
Vassanji kaondoka Tanzania miaka mingi iliyopita lakini moyoni haijamtoka.

Sishangai kuwa kila aliyekuwa ughaibuni dawa ya kupoza ukiwa wake wa kuwa mbali na nyumbani ni kurasa za Vassanji.
 
Mzee said ivi yule mrembo uliyemuoa ramadhan ya mwaka huu bado uko naye au baada ya ramadhan kuisha ukamtupa nje kama kawaida yako
 
Back
Top Bottom