Makosa na Msamaha katika mapenzi

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Katika mapenzi watu hukoseana na wakati mwingine hata kuchukizana na kukasirikiana. Na kuna wakati makosa hayo huzaa hadi vurugu na hata kusababisha matumizi ya nguvu (violence) na katika matukio mengine makosa hayo hufikia kukatishia maisha.

Makosa yapo mengi kuanzia madogomadogo kama mtu kuwa msahaulifu, kufanya kitu ambacho kinasababisha usumbufu n.k na yapo makosa makubwa kama kwenda nje ya mahusiano na kuzaa nje ya ndoa..

Makosa hayo yote huita mwitikio kwa pande zote mbili, kuna mwitikio wa uchungu, kisasi, hasira, wivu na hata kinyongo cha muda mrefu. Na wakati mwingine haya yote yanadumu siku baada ya siku, mwezi baada ya mwezi na hata miaka. Hivyo makosa haya ya mapenzi yanaweza kusababisha madhara ya kihisia, kisaikolojia na hata kimaumbile kwa yule ambaye amakutwa nayo.

Na kutokana na hayo kuna mambo ambayo watu hufikia mahali na kusema kuwa makosa fulani hayasameheki na kuwa mtu wake akifanya kosa x basi hawezi kumsamehe kamwe..

(itaendelea)...
 
Approach ni ishu sana katika mlolongo mzima wa mkosaji katika kuomba msamaha.

Mimi nasema hakuna kosa lisilosameheka...Mbona ni watu kibao mtaani tunawajua wanawasamehe wake/waume zao kwa makosa ambayo wengine walishaapa kwamba hawatasamehe?
Inategemeana na mtenda na mtendwa pamoja, mioyo yao ikoje.

Kosa moja linamuudhi mtu x kidogo tu, na anasamehe, wakati kosa hilohilo linamgharimu mtu y kutoa talaka au kutoa uhai wa mkosaji.

Tunatofautiana sana katika kuhimili uvumilivu na subira pindi tukosewapo!
 
Wapendwa mimi nadhani mwanaume siku zote ndio huwa mgumu sana kusamehe, yaani anaumia rohoni na kutamani hata kutoa roho ya mtu, Mimi nafahamu wanandoa fulani kabla ya kuoana past ya mwanamke ilikuwa chafu kidogo, lakini hakumwambia mwenzie pengine kwa kuhofoa kutemwa labda kwakuwa alimpenda sana, lakini hadi wasiochelewa na wenye visa na mkewe wakaanza kumsemea kwa mumewe, mume hadi leo hajasamehe kwa kile anachokiita ati mkewe hakuwa mkweli kwake, na tayari wana miaka minne ya ndoa yao kwa sasa na watoto. Lakini mwanamke kuna wakati aligundua uhusiano wa mumewe na msichana wa zamani kabla ya wao kuwa kitu kimoja, mume aliomba kusamehewa na alisamehewa, ingawa si kwa urahisi lakini ALISAMEHEWA, lakini hiki cha sasa cha huyu bibie,.. mume anashindwa kusamehe, ndoa imekuwa ndoano, sijui wataishia wapi. Point yangu ni kuwa mwanaume siku zote ni mgumu sana katika kusamehe!
 
Katika mapenzi watu hukoseana na wakati mwingine hata kuchukizana na kukasirikiana. Na kuna wakati makosa hayo huzaa hadi vurugu na hata kusababisha matumizi ya nguvu (violence) na katika matukio mengine makosa hayo hufikia kukatishia maisha.

Makosa yapo mengi kuanzia madogomadogo kama mtu kuwa msahaulifu, kufanya kitu ambacho kinasababisha usumbufu n.k na yapo makosa makubwa kama kwenda nje ya mahusiano na kuzaa nje ya ndoa..

Makosa hayo yote huita mwitikio kwa pande zote mbili, kuna mwitikio wa uchungu, kisasi, hasira, wivu na hata kinyongo cha muda mrefu. Na wakati mwingine haya yote yanadumu siku baada ya siku, mwezi baada ya mwezi na hata miaka. Hivyo makosa haya ya mapenzi yanaweza kusababisha madhara ya kihisia, kisaikolojia na hata kimaumbile kwa yule ambaye amakutwa nayo.

Na kutokana na hayo kuna mambo ambayo watu hufikia mahali na kusema kuwa makosa fulani hayasameheki na kuwa mtu wake akifanya kosa x basi hawezi kumsamehe kamwe..

(itaendelea)...

Kwenye swala la kuombwa msamaha au kuomba, inategemea ni nani anakuomba msamaha hapo hatuangalii ni kosa gani, tunaangalia anayeomba, unaweza kukuta ni mtu wako wa maana sana amekukosea kumkosa hutaki na unaamini ankupenda ameteleza tu kumsamehe ni rahisi. Ila inatofautiana kwa mtu na mtu
 
Wapendwa mimi nadhani mwanaume siku zote ndio huwa mgumu sana kusamehe, yaani anaumia rohoni na kutamani hata kutoa roho ya mtu, Mimi nafahamu wanandoa fulani kabla ya kuoana past ya mwanamke ilikuwa chafu kidogo, lakini hakumwambia mwenzie pengine kwa kuhofoa kutemwa labda kwakuwa alimpenda sana, lakini hadi wasiochelewa na wenye visa na mkewe wakaanza kumsemea kwa mumewe, mume hadi leo hajasamehe kwa kile anachokiita ati mkewe hakuwa mkweli kwake, na tayari wana miaka minne ya ndoa yao kwa sasa na watoto. Lakini mwanamke kuna wakati aligundua uhusiano wa mumewe na msichana wa zamani kabla ya wao kuwa kitu kimoja, mume aliomba kusamehewa na alisamehewa, ingawa si kwa urahisi lakini ALISAMEHEWA, lakini hiki cha sasa cha huyu bibie,.. mume anashindwa kusamehe, ndoa imekuwa ndoano, sijui wataishia wapi. Point yangu ni kuwa mwanaume siku zote ni mgumu sana katika kusamehe!
Pamoja na ugumu wa kusamehe, ili tuishi maisha yasiyo na presha, ni lazima tujifunze kusamehe. Hakuna jinsi maana sisi kama binadamu hatuwezi kuacha kukosa. Imagine, itabidi uamue kusihi na malaika kama hutataka kusamehe
 
Na mwanaume je?

hawa ndo wabaya zaidi.....
kila wakati reference kwenye lile kosa basi maisha yanakuwa magumu kupindukia na mwisho wa siku unaweza kubwaga manyanga kuepusha mengi zaidi

ngumu sana kuwa na mwanume mwenye gubu/mwanamke mwenye gubu
kama umeamua kusamehe samehe yaishe sio leo umesamehe na kesho unaanza ku-refer ulokwisha sema umesamehe......
 
Pamoja na ugumu wa kusamehe, ili tuishi maisha yasiyo na presha, ni lazima tujifunze kusamehe. Hakuna jinsi maana sisi kama binadamu hatuwezi kuacha kukosa. Imagine, itabidi uamue kusihi na malaika kama hutataka kusamehe

furaha ya kusamehe ni kubwa mno kuliko hata ya kuombwa msamaha....

ukikaa ni kinyongo moyo huwa mzito mno na daima hutapata furaha tofauti na unaposamehe.....
 
Katika mapenzi watu hukoseana na wakati mwingine hata kuchukizana na kukasirikiana. Na kuna wakati makosa hayo huzaa hadi vurugu na hata kusababisha matumizi ya nguvu (violence) na katika matukio mengine makosa hayo hufikia kukatishia maisha.

Makosa yapo mengi kuanzia madogomadogo kama mtu kuwa msahaulifu, kufanya kitu ambacho kinasababisha usumbufu n.k na yapo makosa makubwa kama kwenda nje ya mahusiano na kuzaa nje ya ndoa..

Makosa hayo yote huita mwitikio kwa pande zote mbili, kuna mwitikio wa uchungu, kisasi, hasira, wivu na hata kinyongo cha muda mrefu. Na wakati mwingine haya yote yanadumu siku baada ya siku, mwezi baada ya mwezi na hata miaka. Hivyo makosa haya ya mapenzi yanaweza kusababisha madhara ya kihisia, kisaikolojia na hata kimaumbile kwa yule ambaye amakutwa nayo.

Na kutokana na hayo kuna mambo ambayo watu hufikia mahali na kusema kuwa makosa fulani hayasameheki na kuwa mtu wake akifanya kosa x basi hawezi kumsamehe kamwe..

(itaendelea)...
Mimi nashida na kimaumbile kivipi mtu anaweza kuathirika kimaumbile,unamaanisha kwa kupigwa?
 
Mimi nashida na kimaumbile kivipi mtu anaweza kuathirika kimaumbile,unamaanisha kwa kupigwa?

hapana yaani kutokana na kutokusamehe mwili utaanza kuonesha udhaifu na hata magonjwa mbalimbali yanaweza kuukumba. Kwa sababu kuna uhusiano usiotenganishwa kati ya afya ya akili (mental health) na afya ya mwili (physical health)..
 
hapana yaani kutokana na kutokusamehe mwili utaanza kuonesha udhaifu na hata magonjwa mbalimbali yanaweza kuukumba. Kwa sababu kuna uhusiano usiotenganishwa kati ya afya ya akili (mental health) na afya ya mwili (physical health)..

Nashukuru.Mwandishi wewe,Dakatari wewe,Mwanasaikolojia wewe.Haya hongera bwana.
 
-Kusamehe kunahitaji Moyo mkubwa na pia kuomba radhi nako kunahitaji mtu msyaarabu.

Kimsingi ustaaarabu na kuheshimiana ndiko kwenye kuleta suluhu,suluhu huleta maridhiano na hayo ndiyo yatakayozaa msamaha
 
Back
Top Bottom