Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Katika mapenzi watu hukoseana na wakati mwingine hata kuchukizana na kukasirikiana. Na kuna wakati makosa hayo huzaa hadi vurugu na hata kusababisha matumizi ya nguvu (violence) na katika matukio mengine makosa hayo hufikia kukatishia maisha.
Makosa yapo mengi kuanzia madogomadogo kama mtu kuwa msahaulifu, kufanya kitu ambacho kinasababisha usumbufu n.k na yapo makosa makubwa kama kwenda nje ya mahusiano na kuzaa nje ya ndoa..
Makosa hayo yote huita mwitikio kwa pande zote mbili, kuna mwitikio wa uchungu, kisasi, hasira, wivu na hata kinyongo cha muda mrefu. Na wakati mwingine haya yote yanadumu siku baada ya siku, mwezi baada ya mwezi na hata miaka. Hivyo makosa haya ya mapenzi yanaweza kusababisha madhara ya kihisia, kisaikolojia na hata kimaumbile kwa yule ambaye amakutwa nayo.
Na kutokana na hayo kuna mambo ambayo watu hufikia mahali na kusema kuwa makosa fulani hayasameheki na kuwa mtu wake akifanya kosa x basi hawezi kumsamehe kamwe..
(itaendelea)...
Makosa yapo mengi kuanzia madogomadogo kama mtu kuwa msahaulifu, kufanya kitu ambacho kinasababisha usumbufu n.k na yapo makosa makubwa kama kwenda nje ya mahusiano na kuzaa nje ya ndoa..
Makosa hayo yote huita mwitikio kwa pande zote mbili, kuna mwitikio wa uchungu, kisasi, hasira, wivu na hata kinyongo cha muda mrefu. Na wakati mwingine haya yote yanadumu siku baada ya siku, mwezi baada ya mwezi na hata miaka. Hivyo makosa haya ya mapenzi yanaweza kusababisha madhara ya kihisia, kisaikolojia na hata kimaumbile kwa yule ambaye amakutwa nayo.
Na kutokana na hayo kuna mambo ambayo watu hufikia mahali na kusema kuwa makosa fulani hayasameheki na kuwa mtu wake akifanya kosa x basi hawezi kumsamehe kamwe..
(itaendelea)...