Makosa Katika Historia ya Nyumba ya Julius Nyerere Mtaa wa Ifunda Magomeni Kama Ilivyoandikwa na Daily News 9 December 2023

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,920
30,261
MAKOSA KATIKA HISTORIA YA NYUMBA YA JULIUS NYERERE MAGOMENI KAMA ILIVYOANDIKWA NA DAILY NEWS

Daily News la tarehe 9 December 2023 (link hiyo hapo chini) imechapa makala yanayosema kuwa nyumba hiyo ya Mwalimu Nyerere ndipo alipoishi mara tu baada ya kuacha kazi ya ualimu St. Francis College Pugu.

Daily News linasema kuwa katika nyumba hiyo ndipo ikifanyika mikutano ya harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ukweli ni kuwa Nyerere baada ya kuacha kazi alikwenda kuishi na Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Nyumba hii ndipo ikifanyika mikutano yote ya siri kuanzia enzi za TAA 1950s hadi inaundwa TANU mwaka wa 1954.

Mikutano yote kuanzia vipi Nyerere ataingizwa katika uongozi hadi mipango ya safari ya UNO yote ikifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes.

Nyerere alifikishwa nyumba hii na Joseph Kasella Bantu alipokwenda kumjulisha kwa Abdul Sykes mwaka wa 1952.

Abdul Sykes alikuwa TAA Secretary na Act. President.

Kuanzia hapo 1952 hadi Nyerere anachukua uongozi wa TAA 1953 na kuundwa kwa TANU 1954 na baadae Mwalimu Nyerere alikuwa akihudhuria vikao vyote vya harakati katika nyumba hii.

Nyumba hiyo ya Magomeni Mwalimu aliijenga na kuhamia mwaka wa 1958 na kabla ya kuhamia hapo alipohama nyumbani kwa Abdul Sykes TANU ilimtafutia nyumba Magomeni Maduka Sita.

Mwalimu aliishi nyumba hii kwa miaka mitatu na alipotoka hapo ndipo alipohamia kwenye nyumba yake aliyojenga Mtaa wa Ifunda ambako si mbali na Maduka Sita.

Nyumba hii hakuishi hata zaidi ya mwaka akahamia nyumba ya serikali Sea View.
PICHA: Nyumba ya Julius Nyerere, Majumba Sita ikimwonyesha Nyerere akiingia ndani mwake.

Nyumba ya pili ni ya Abdul Sykes alipoishi Nyerere.

Nyumba hii picha ya tatu haipo imejengwa nyumba
nyingine.

1702292959972.png

1702293026742.png

1702293055192.png

 
Uhuru ulipatikana mwaka 1961.....
Kwa maelezo yako nyumba hiyo Nyerere alihamia mwaka 1958.
Je katika Miaka hiyo 3, mwalimu hakufanya vikao vyovyote Nyumbani kwake?
Kama alifanya basi hawajaandika uongo.
Ila tu hawajaandika kuhusu nyumba ya Sykes kama ulivyopenda iwe.
 
Uhuru ulipatikana mwaka 1961.....
Kwa maelezo yako nyumba hiyo Nyerere alihamia mwaka 1958.
Je katika Miaka hiyo 3, mwalimu hakufanya vikao vyovyote Nyumbani kwake?
Kama alifanya basi hawajaandika uongo.
Ila tu hawajaandika kuhusu nyumba ya Sykes kama ulivyopenda iwe.
Stalin...
Hapakuwa na vikao vya siri katika nyumba ile.

Baada ya Kura Tatu hali ilikuwa shwari na TANU sasa inazungumza ndani ya LEGCO, yaani Baraza Kutunga Sheria.
 
Thanks 👍
Ukipata wasaa tunaomba list ya watanganyika wasomi kabla ya Uhuru,

Maana wengi wadai aliyekuwa na degree kipindi hochi ni Nyerere Pekee, kitu ambacho naona Sio kweli
 
Malila...
Hilo la kukataa ukweli mimi halinizuii kueleza ukweli.
mara nyingi nimefaidika mno binafsi kuijua historia ya mambo yetu haya, usikate tamaa kutuongezea ukweli juu ya kile tulichodhani tunakijua kumbe ilikuwa magumashi. Kwa hilo mzee wetu una credit yako, hata kama hawataki.
 
MAKOSA KATIKA HISTORIA YA NYUMBA YA JULIUS NYERERE MAGOMENI KAMA ILIVYOANDIKWA NA DAILY NEWS

Ukweli ni kuwa Nyerere baada ya kuacha kazi alikwenda kuishi na Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.
Naunga mkono hoja, ila pia tusimlaumu mwandishi kwasababu the source ni fasihi simulizi.

Mwandishi amesema "After he had left his job at St Francis, Mwl Nyerere moved in with other political activists but these new dwellings were deemed perilous for a man of his stature. He was given the Magomeni Usalama plot by one Sheikh Abeid Karuta, where he built the house from scratch and moved into his new home in January 1959, two years before independence in 1961. Mwalimu stayed at the complex for only eight months", hivyo harakati za uhuru hazikudumu kwa miezi 8, tuu. Na mwandishi kasema baada ya Mwalimu kuacha kazi "moved in with other political activists" sio lazima kumtaja!.

Niliwahi kupelekwa kumsalimia Mama Daisy pale upanga mkabala na Califonia dreamer, alinihadithia kuhusu Nyerere kuishi kwao, ni yeye ndiye aliyemfundisha Mama Maria kukanda chapati, vitumbua na maandazi, iliwemo kwenda kuokota makumbi mitaa ya gerezani hadi mission quoters. Walikuwa wanatembea peku!.

Sio kwamba walikuwa hawana viatu au kuvaa ndala, bali walitembea peku ili kufanania na wanawake wengine wote wa enzi hizo.

Mama Daisy ndie alimfundisha Mama Maria, mwanamke kujishughulisha na sio wanawake ma golikipa!.

Kuna event nikakutana na Mama Maria, nikamsalimia na kutaka kumpiga zile vox pop zangu, mlinzi wake akaniambia niandike barua na kuweka maswali, nikubaliwe ndipo nikaulize. Kiukweli barua sikuandika!.

 P
 
Naunga mkono hoja, ila pia tusimlaumu mwandishi kwasababu the source ni fasihi simulizi.

Mwandishi amesema "After he had left his job at St Francis, Mwl Nyerere moved in with other political activists but these new dwellings were deemed perilous for a man of his stature. He was given the Magomeni Usalama plot by one Sheikh Abeid Karuta, where he built the house from scratch and moved into his new home in January 1959, two years before independence in 1961. Mwalimu stayed at the complex for only eight months", hivyo harakati za uhuru hazikudumu kwa miezi 8, tuu. Na mwandishi kasema baada ya Mwalimu kuacha kazi "moved in with other political activists" sio lazima kumtaja!.

Niliwahi kupelekwa kumsalimia Mama Daisy pale upanga mkabala na Califonia dreamer, alinihadithia kuhusu Nyerere kuishi kwao, ni yeye ndiye aliyemfundisha Mama Maria kukanda chapati, vitumbua na maandazi, iliwemo kwenda kuokota makumbi mitaa ya gerezani hadi mission quoters. Walikuwa wanatembea peku!.

Sio kwamba walikuwa hawana viatu au kuvaa ndala, bali walitembea peku ili kufanania na wanawake wengine wote wa enzi hizo.

Mama Daisy ndie alimfundisha Mama Maria, mwanamke kujishughulisha na sio wanawake ma golikipa!.

Kuna event nikakutana na Mama Maria, nikamsalimia na kutaka kumpiga zile vox pop zangu, mlinzi wake akaniambia niandike barua na kuweka maswali, nikubaliwe ndipo nikaulize. Kiukweli barua sikuandika!.

 P
Ndo hapo mzee wetu anaumia ,hawa wanoitwa kwa jina la jumla "other polical activicts " nimuhimu mno wakatajwa kwamajina

Kizazi cha kivaa mlegezeo kikawafahamu pia au kizazi cha wafuta midomo hatua mbili mbele wanafuta mdomo
 
Back
Top Bottom