Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,504
- 113,618
Naunga mkono hoja, huyu ni hazina ya kweli!, tena amshukuru sana Mungu, maridhiano yamevunjika!, vinginevyo Jimbo la Hai lilikuwa ni miongoni mwa majimbo ya kwenye mgao wa nusu mkate!, maridhiano yangeendelea, Saashisha Mafue, alikuwa atoswe!.
MAKONDA: MBUNGE SAASHISHA MAFUWE NI HAZINA
"Na hapa mna bahati ya kuwa na Mbunge Kijana (Saasisha Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai) na Mimi nilimuona Bungeni hata kabla sijawa Kiongozi anavyopigania hasa ardhi zenu, amehangaika sana na Vyama vya Ushirika na kutetea ardhi ya wana Hai ibaki mikononi mwenu lakini pia hakuchoka pale kwenye elimu anatamka, penye maji anatamka, kwenye Barabara anatamka wana Hai mnayo hazina" - Makonda
Paul Makonda ambaye ni Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo CCM amezungumza hayo, Jumanne Januari 22.2024 akiwa Hai, mkoani Kilimanjaro na kuongeza kwa kusema Jimbo la Hai limepata Hazina, Mbunge Saashisha Mafuwe ni Hazina nzuri kwa wana Hai.
P