Watu wengi wamekuwa na ushabiki sana wakati huu Makonda kupewa usemaji wa CCM. Ukianza kuuliza maswali muhimu Je Makonda kafanya nini cha maana kimaendeleo wakati wake? Hakuna majibu ya maana.
Wakati bandari inapewa DP world bila kuweka mikataba mingine wazi, nchi ina tatizo la umeme, kampuni ya ujenzi wa reli ya uturuki ina matatizo makubwa ya pesa, hatujui hatima ya chaguzi zetu za 2024 na 2025 na mabadiliko ya sheria za chaguzi na katiba.
Inasikitisha hata wale wasome wameingia kwenye kiki mbalimbali na ushabiki na kupitwa na mambo muhimu ya nchi.
Ushabiki hasa unashangaza kwa mtu ambaye anajulikana kwa kutumia madaka vibaya. Makonda kunyanyasa vyombo vya habari mpaka kwenda kutishia studio, Makonda kusingizia watu wanatumia madawa ya kulevya, kunyanyasa wapinzani, kujaribu kuchukuwa mali za wafanyabiashara.
Lakini inashangaza watu hasa wale wasomi kuweka ushabiki kama vile Makonda alikuwa anafanya cha maana.
Amechaguliwa kuwa mwongeaji basi tuendelee na mambo ya msingi. Wezi wanatumia ujinga kama huu kufanya mambo yao wakati wananchi wanaleweshwa makonda!
Wakati bandari inapewa DP world bila kuweka mikataba mingine wazi, nchi ina tatizo la umeme, kampuni ya ujenzi wa reli ya uturuki ina matatizo makubwa ya pesa, hatujui hatima ya chaguzi zetu za 2024 na 2025 na mabadiliko ya sheria za chaguzi na katiba.
Inasikitisha hata wale wasome wameingia kwenye kiki mbalimbali na ushabiki na kupitwa na mambo muhimu ya nchi.
Ushabiki hasa unashangaza kwa mtu ambaye anajulikana kwa kutumia madaka vibaya. Makonda kunyanyasa vyombo vya habari mpaka kwenda kutishia studio, Makonda kusingizia watu wanatumia madawa ya kulevya, kunyanyasa wapinzani, kujaribu kuchukuwa mali za wafanyabiashara.
Lakini inashangaza watu hasa wale wasomi kuweka ushabiki kama vile Makonda alikuwa anafanya cha maana.
Amechaguliwa kuwa mwongeaji basi tuendelee na mambo ya msingi. Wezi wanatumia ujinga kama huu kufanya mambo yao wakati wananchi wanaleweshwa makonda!