Wapeleke Azimio la kutokuwa na imani na Rais tuone kama watakataa kujiuzulu hao wezi.
Huko ni mbali!
Jibu ni rahisi.linapendekeza na si kuazimia-na hili au mamuzi hayo hayana harufu anayodai Makinda ya kuingilia Mamlaka ya Raisi.
Kufanya hivyo kumpa Raisi kufanya maamuzi sahihi- Yupi anondoka moja kwa moja au yupi arudi kwenye kundi baada ya kuvunja Baraza la Mawaziri.
Bunge linapendekeza kwamba Mamlaka ya Uteuzi itengue uteuzi wa nafasi ya uongozi na utendeji ya Viongozi na Watendaji walioshiriki katika uzembe huu au kwa kushindwa kuchukua hatua kujua au kuto juu katikati sakata nzima la mgogoro wa Escrow Akaunti iliyokuwa BOT ,kwa kadri kamati ya PAC ilivyo wasilisha taarifa ya ushiriki wao kupitia taarifa ya CAG na PCCB.Na kwa maana hiyo basi watajwa wanaopendekezwa katika pendekezo hili ni kama ifuatavyo.
1.PM
2.Waziri wa Nishati
3.Naibu waziri wa Nishati
4.Katibu Mkuu Nishati
5.AG
Kuna hili la Waziri Prof.Tubaijuka.
Bunge linapendekeza kwamba kuhusiana na Waziri ambaye ni sehemu ya Serikali (Baraza la Mawaziri) kuchukua kiasi cha pesa za Kitanzania 1.6bl na amekiri kufanya hivyo basi Mamlaka ya Uteuzi ipate kushauriwa na vyombo husika vya Serikali vya kichunguzi kuona kama kuliwa na vitendo vya uvunjifu wa Sheria na kama itadhihirika, hivyo basi hatua ya kutengua uteuzi wake ichukuliwa na hii ikiwa ni pamoja na kumfikishwa mbele ya Vyombo vya Sheria.
Hakuna namna nyingi labda wabaki ndani ya bunge wanaowatetea wazembe na wapitishe mapendekezo yao.