BI MKUBWA
( sehemu ya 8 )
Endeleaa..................
“Nenda chumbani kampake dawa ya kumzindua yule baba mwenye nyumba, aliamuru kiongozi wa wachawi. Haraka sana nilifumba macho huku nikiyafunua
kidogo, kwa kuwa kulikuwa na giza hakuweza kuona kuwa naona.
Nilimuona yule mchawi akifungua kibuyu kidogo akanywa ile dawa na kututemea,
Baada ya kututemea ile dawa akatoka na kuwafuata wenzake balazani wakapanda ndege yao na kuondoka mama mkwe aliingia chumbani kwake na kujipumzisha akitafakari yajayo.
Hatimaye kulikucha niiamshwa na kelele ya vijana watoto pamoja na wazee walikuwa Nyumba ya jirani wakishuhudia mchawi aliye nasa .
Asubuhi nyumba ya jirani ilikuwa imejaa watu ambao walikuwa wakipiga kelele.
“Mchawi, mchawi kanasa ndani.
"Mtoeni tumwone huyooo
"Na lazima apigwe aseme ukeweli
Umati ulikuwa mkubwa sana na kelele zikawa nyingi, mume wangu naye aliamshwa na zile kelele,
"Mke wangu vipi?
"Safi, umeamaje wewe?
“Mhhhh… johari, mwili unauma sana,
“Pole sana, kwani ulifanya kazi gani?”
“Hakuna, vipi mbona kuna kelele huko nje?
“Nasikia kuna mchawi kanasa katika nyumba ya huyo shoga yangu.
“Shoga yako yupi?
“Yule aliyekuja hapa nyumbani na kusema atatupeleka kwa baba yake akatufanyie zindiko.”
“Acha utani,
"Kweli tena
"kwake ameshikwa mchawi?”
“Siyo ameshikwa. Amenasa!”
“Unatania?
“Husikii kelele huko nje?
"Ndio nasikia.
"Njoo hapa dirishani uone.
“Kwani hapo dirishani huyo mchawi aliyenasa anaonekana?”
“Hapana …uje uone watu walivyojazana nje ya madirisha.
Mume wangu alifika dirishani ili na yeye aweze kuchungulia Nyumba ya jirani
“Kwa kuwa yule mama mwenye nyumba ni rafiki yako nenda kamuone,
"Ila naogopa sana mume wangu
"Unaogopa nini?
"Kuona wachawi unazani mchezo.
"Si kuna watu kibao kule?
"Ndio
"Nenda basi kashuhudie uje unipe habari
"Sawa basi ngoja niende.
Nilijitanda kitenge changu na kwenda kujionea japokuwa picha nzima nilikuwa naijua kutokana na kusikia waliyokuwa wakiyafanya wachawi usiku hapa nyumbani kwangu.
Nilifika pale na yule shoga yangu aliponiona aliniita pembeni akaanza kunisumulia:
“Unajua nini Johari?
"Niambie shoga yangu.
" kama nilivyokuambia jana kuwa mtaa huu Luna wachawi na nyumbani kwako kuna wachawi wanakuja kila siku usiku huku wengine wakitumia ungo.
"Kumbe ni kweli yaani nilikuwa sikuamini
"Umeamini sasa?
"Asilimia mia moja.
"Lakini nilikuambia?
“Nakumbuka uliniambia hivyo tena mbele ya mume wangu,
"Leo wameingia cha kike sasa.
"Chakike haswaa
"Sasa huyo aliyenaswa ni nani?
“Shoga namjua basi?
"Si umemwona au?
"Ndio, Labda wewe ukimuona unaweza kumfahamu.
Jirani yangu huyo alinipenyeza licha ya kuwepo watu wengi, walimpisha kwa kuwa walikuwa wanajua kuwa yeye ndiye mama mwenye nyumba, huku nami nikijitahidi kumfuata.
Tulifika ndani ya nyumba na kumkuta mchawi akiwa bado ameganda katikati ya sebule huku watu wakiwa wamejazana kwenye madirisha ili
waweze kumuona, alikuwa amevaa kaniki kiunoni.
Niliingiwa na hofu kubwa hasa niliposikia watu wengine wakisema mchawi yule achomwe moto.
Lakini hata mume wa rafiki yangu niliona ana wasiwasi baada ya kusikia maneno hayo kwani alianza kuhangaika kupigia simu kwa watu ambao mimi sikuwajua.
"Hellow
"Hellow
"Shikamoo mzee,,
"Marahaba, mnaendeleaje huko?
"Salama , ila kuna tatizo.
"Tatizo gani teni?
"Kuna mchawi kanasa hapa nyumbani
"Sawa basis nafika sasa hivi.
“Mzee naomba uje haraka wasije kumdhuru huyu mchawi,
Baada ya kumwona yule mchawi ilibidi nitoke niende nyumbani, nikachomoka kwa kasi kuelekea nyumbani kwangu, njiani nikakutana na mume wangu ambaye alikuwa amevaa bukta, fulana na
makubazi miguuni.
"Mume wangu wapi tena?
"Naenda Kwann Hugo mchawi.
"Si ulisema Mimi niende nine kukupa habari?
"Nimegundua habari nzuri uisome mwenyewe.
"Makubwa!!!!
"Nenda basis nyumbani mke wangu?
"Sawa, ila uyo mchaei ni nona mme wangu
"Kwanini?
"Ukimwangalua tu anakutemea mate, na mate yake yanaruka kama nyoka.
"Basi siendi, twende nyumbani mke wangu.
"Hahaà kumbe mwoga nakutania bwana hatemi mate.
"Acha masihara wewe mchawi si mchezo.
"Sawa unaogoa wakati pale nyumbani unaishi nae.
"Nani mchawi palenyumvani naenda kumfanya bucha sasa hivi,
"Kwani wewe humjui ?
"Nitajie nani?
"Si wewe mme wangu.
"Acha masihara wewe mambo hayo sio ya masihara,
"Sawa yaishe mume wangu!!
“Ehee, huyo aliyenaswa unamfahamu?” "simjui,
"Yupo sehemu gani?
"Yupo tu pale sebuleni anang’aang’aa macho.
“Sasa wenye nyumba wanasemaje?”
“Baba mwenye nyumba nimemuona akihangaika kupiga simu kwa watu ambao siwajui,
“Amepiga simu polisi?”
“Sijui.”
“Lakini akishafika huyo mtu akamnasua, huyo mchawi atapita wapi?
"Kwanini?
" Ni wazi atauawa palepale nje ya nyumba yake ni vema akaita kwanza polisi.
“Hilo naona hajakumbuka, amepaniki, ni vema ukawahi kumpa ushauri huo.”
“Hapana turudi sote tukatoe ushauri kwa pamoja.
Nilikubaliana na mume wangu hivyo nikageuza njia na kuanza kuelekea tena kwa jirani yetu. Tulipofika watu ndiyo walizidi, bahati nzuri tulikuta kuna waandishi wa habari wa Gazeti la Uwazi
ambao baada ya kutuona walitukabili.
“Mama samahani, mimi ni dulla?
"Kwahiyo
"huyu ni bosi wangu anaitwa chid ni mwaandishi wa gazeti la Uwazi, tumeambiwa wewe ulikuwa
ndani, unamfahamu huyo mchawi aliyenaswa?”
“Kaka mimi huyo aliyenaswa kweli nimemuona lakini simfahamu kwa jina wala sijawahi kumuona hapa mtaani.”
“Lakini watu wanasema wewe na mama mwenye nyumba ni marafiki,
"Kwahiyo kama marafiki?
"je, umeonana naye na mmeshauriana nini?
"Nimeonana nae lakini mini sio msemaji wa Nyumba za watu mtafuteni mwenye nyumba,
"Sawa, basi Nina swali La mwisho Dada angu.
"Uliza,
"Tunaomba basi hata jina tu LA huyo mchawi?
"simfahamu kwa jina wala kwa sura,
"Ina maana ni mgeni?
"sijawahi kumuona hapa mtaani.
"Na kinachoendelea hapa Kwa sasa ni nini?
"Tumeshauriana kwamba waitwe polisi."
"Polisi wataweza kumnasua mchawi?
"Polisi ni Kwaajili ya ulizi tu si unaona watu walivyojaa hapa wanaweza wakampiga.
"Sawa asante sana dada,
"Sawa kwaherini
"Samahani tena kidogo Dada ,
"Vipi tena?
"Sijui unaitwa nani ?
"Siwezi kutaja jina, samahani kwa hilo.
Niliwaacha waandishi hao na kwenda kwa mama mwenye nyumba ambaye alikuwa na mumewe nami na mume wangu.
Mume wangu alipewa jukumu la kuita polisi naye akapiga namba 112 na polisi wakaitikia.
"Umepiga simu polisi station, naongea na nani?
"Mervin charz
" tukusaidie nini?
"Hapa Mtaa wa Pwiriri, kuna mchawi amenaswa.
"Polisi hatuhusiki na mambo ya kishirikina.
"Ndio, lakini sasa kanasa hapa?
"Sawa, sasa mnataka msaada gani kwa sababu sisi polisi hatuwezi kumnasua!"
"Sio kumnasua
"Ila nini sasa kama kanasa?
"Hapana msaada wetu ni kwamba tunataka mje kulinda usalama wake na wa mali pia kwa kuwa watu wanatishia kumlipua kwa mafuta ya taa.
"Kwahiyo akilipuliwa ?
" Sasa wakifanya hivyo akiwa ndani ni wazi kwamba vitu vingi pamoja na nyumba vitatekelea, tafadhalini njooni,
"Nimekuelewa, tunakuja,
Nje ya nyumba fujo zilizidi na wakati tunatafakari nini cha kufanya, aliingia mtu mmoja ambaye alikuwa ni mzee wa makamo.
"Baba karibu sana.
"Asante sana,
"Shikamoo mzee,
"Marahaba vipi hapa salama?
"Salama sio sana , kama unavyo ona
"Sawa, haina shida.
"Baba Umekuja na teksi?
"Ndiyo," alijibu mzee huyo.
"Sawa. Shilingi ngapi anataka?"
"Nimeshamlipa," alijibu mzee.
Jirani zangu huyu ni baba yangu mzazi na ndiye aliyenitengenezea nyumba hii ili wachawi wasiingie, akatutambulisha.
"Shikamoo baba, tulijishitukia mimi na mume wangu tukimuamkia kwa pamoja kama vile kuna mtu alituamuru kufanya hivyo.
"Marahaba, marahaba
"Mzee hawa ni jirani zangu, tunaishi nao vizuri. Ilikuwa tuwalete kwako Jumapili ijayo ili kuwazindikia nyumba yao," alisema baba mwenye nyumba.
"Bado hamjachelewa, walete tu. Tumalize kwanza hili lililonileta," akasema.
"Hapana baba tusubiri kwanza polisi.
"Polisi wanini?
"Si unaona jinsi fujo zilivyotanda hapo nje?
Kabla hajajibu lolote tulisikia ving'ora vikilia nikajua kwamba hao ni polisi wanakuja. Hata hivyo, nilishanga kusikia ving'ora vya magari mawili nikajiuliza kwa nini wamekuja na magari mawili kana kwamba kuna fujo tayari zimefumuka.
Nilichungulia dirishani nikaona kumbe walikuwa wameongozana na gari la Kikosi cha Zima Moto. Watu waliokuwa wamejazana mlangoni akiwemo mama mkwe wangu walipisha na kuweka njia bila hata kuamrishwa baada ya kumuona mkaguzi wa polisi yaani Inspekta Kijo akija ndani pamoja na maofisa wengine wa polisi.
Aliingia akiwa na askari sita wote wakiwa na silaha za kivita, Semi Machine Gun (SMG).
"Nani mhusika mkuu hapa,
"Muhusika wa nini inspekta?
"Namaanisha mwenye nyumba?
"Ni mimi hapa, hawa ni jirani zangu na huyu ni mke wangu na huyu ni baba mkwe wangu.
"Na huyu handsome ndio.....
"Huyu ndiye mchawi aliyenasa hapa?"
"Ndiyo, anaonekana tu
"Sisi sijui tungetoka nje tuwapishe muongee, alisema johari
"Jirani bakini tu haina shida
"Ina maana hawezi kujisogeza kabisa?" aliuliza swali yule inspekta wa polisi, swali ambalo halikuwa na jibu kwa sababu alimuona na kama angeweza kujisogeza tusingesema alinasa.
"Ndio Inspekta
"Sasa mtamnasuaje?
"Yupo mtu wa kumnasua,
"Nani huyo mtaalamu?
"huyu baba mkwe wangu,
"Kumbe mtaalamu yupa hapahapa?
"Ndio, tulikuwa tunawangoja nyinyi mje kwa usalama wa huyu mchawi.
"Mmefanya vizuri sana
" Tulifikiri kama tungemnasua bila nyinyi kuwepo, watu wenye hasira wangeweza kumuua."
"Kwani anaitwa nani huyu?
Swali hilo LA Inspekta lilianzisha mada mpywa na ngumu kuliko tulivyofikilia nikajua sasa hapa mama mkwe anaenda kuumbuka.
"Kwa kweli hatumjui inspekta
"Hata jina kumbe hamlijui?
"Ndio inspekta
"Kwani sio mwenyeji wa hapa
"Ndio, sio mwenyeji
Baba mkwe akadakia
"Basi kama sio mwenyeji wa hapa wanangu kuoni makini atakuwa ana MTU wake nyuma huyu,
"Kweli kabisa baba angu, alijibu mama kibela
"Basi Mimi simtoi hapa mpaka amtaje huyo mwenyeji wake
"Baba bora tu umtoe atakaa mpaka saa ngapi?
"Mwanangu kumnasa huyu ujue umeanzisha vita mpywa na wachawi
"Ni kweli kabisa mama kibela, niliongeza chumvi
"Sawa wewe kijana naomba utoe majibu nitakayokuliza, kwanza uniambie unaitwa nani unatoka wapi na mwenyeji wako nani, ili nikunasue.
Itaendelea..............