Makapuku Forum

JE WAJUA ?

[emoji179]chumvi ikizidi kwenye wali weka kiazi mviringo katikati kikiwa kimemenywa chumvi itapungua.

[emoji179]kama choo chako, kina harufu, ya mkojo na huna dawa washa kiberiti chooni harufu itakwisha

[emoji179]chukua ganda la limao lichome na vipisi vya karafuu weka kila pembe ya chumba mbu utawasikia kwa jirani

[emoji179]kutoa harufu kwenye wali uliongua weka kipande cha mkaa harufu ya kuungua itakata

[emoji179]km umepika mchuzi upo maji maji yaani mwepesi labda maji yamezidi chukua kiazi kikune na cha kukunia nyanya weka chuzi litakuwa rost

[emoji179]kuivisha maharage faster chukua maji yalochemka tia maharage weka kwenye chupa ya chai funga kesho mimina kwenye sufuria pika nusu saa harage litakuwa lishaiva

[emoji179]ukipika mchuzi vitunguu vikiungua weka sukari kidogo harufu ya kuungua haitasikika

[emoji179]Ukiamaliza kuosha vyombo still wire iweke kweny maji haiharibiki utaendelea kutumia kesho

[emoji179]big g ikiganda kwenye nguo weka kweny friza ikiganda itatoka kirahisi

[emoji179]kuondoa harufu ya uvundo kwenye fridge weka baking soda kwenye kikombe na maji kidogo weka kwenye fridge
 
Safi sana mkuu nimejifunza vitu japo vingi vinahusu mapishi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…