Camilo Cienfuegos
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 19,330
- 68,400
1966 - Black Panther Party yaanzishwa na Huey P. Newton na Bobby Seale.
Ni chama kilichojishughulisha na Harakati za kupigania haki za mtu mweusi.
Wakati kinaanzishwa, Mkurugenzibwa FBI wa wakati huo Edgar Hoover alidai chama hiko ni hatari kwa usalama wa ndani wa Marekani.
OkeyNimefatilia baadhi ya vyanzo mbalimbali vya habari, nimeconclude kifo cha Rommel kina utata sana, hakuna jibu sahihi jinsi alivyofariki.
Basi hata maiti yake kuwa na utata ni matokeo ya utata wa kifo chake nadhani.
1990 - Kiongozi wa Soviet, Mikhail Gorbachev anazawadiwa tuzo ya Nobel kwa mchango wake mkubwa katika kumaliza Vita Baridi iliyokuwepo kwa miaka takribani 30 kati ya Urusi na Marekani.
Gorbachev anachukuliwa kama pandakizi aliyekulia na kusomea Marekani na ambaye baadae CIA ilikuja kumuingiza kwenye siasa za Urusi na kushinda Urais na baadae kuvunja Umoja wa Kisoviet wa Kirusi ( USSR ).
Didier akiwa uwanjani huwa hakati tamaa, anajua kupigana akiwa uwanjani1968 - Didier Deschamps anazaliwa.
Kiungo mkabaji wa zamani na nahodha wa Timubya taifa ya Ufaransa.
Alikuwepo kikosini wakati Ufaransa inatwaa Kombe la Dunia mwaka 1998 katika ardhi ya nyumbani akiwa kama kepteni.
Pia Ufaransa ilivyobeba kombe la ulaya mwaka 2000.
Aliwahi kugombana na Eric Cantona kwenye timu ya taifa, baada ya Cantona kumuita Deschamps mbeba maji " Water Carrier " kwakuwa alikuwa anacheza namba 6 kazi yake kuu ni kupora mipira na kumpa Cantona achezeshe timu hivyo hakuwa na ufundi.
Kauli hiyi ilimfanya Cantona kutoitwa tena kwenye Timu ya Taifa.
1920 - Mario Puzo anazaliwa.
Ni mwandishi mashuhuri wa vitabu hasa Novel toka nchini Marekani.
Ndio aliyeandika Novel maarufu ya " The Godfather "
Mapacha1971 - Andy " Andrew " Cole anazaliwa.
Ni mchezaji wa zamani wa Newcastle United, Man Utd na timu ya taifa ya England.
Anakumbukwa zaidi wakati wake akiwa klabuni Man Utd alipotengeneza kombinesheni hatari na Dwight Yorke.
1968 - Didier Deschamps anazaliwa.
Kiungo mkabaji wa zamani na nahodha wa Timubya taifa ya Ufaransa.
Alikuwepo kikosini wakati Ufaransa inatwaa Kombe la Dunia mwaka 1998 katika ardhi ya nyumbani akiwa kama kepteni.
Pia Ufaransa ilivyobeba kombe la ulaya mwaka 2000.
Aliwahi kugombana na Eric Cantona kwenye timu ya taifa, baada ya Cantona kumuita Deschamps mbeba maji " Water Carrier " kwakuwa alikuwa anacheza namba 6 kazi yake kuu ni kupora mipira na kumpa Cantona achezeshe timu hivyo hakuwa na ufundi.
Kauli hiyi ilimfanya Cantona kutoitwa tena kwenye Timu ya Taifa.
HBD Oziliiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii1988 - Mesut Ozil anazaliwa.
Ni kiungo kutoka Arsenal na timu ya taifa ya Ujerumani mwenye asili ya Uturuki.
Anasifika kwa soka la akili lisilo tumia nguvu.
Ameshinda kombe la dunia mwaka 2014.
DahLeo katika Historia:
1940 - Lluis Companys ananyongwa.
Alikuwa ni Rais wa jimbo la Catalonia ( Katalunya ), Jimbo ambalo linapigana ili kujitenga na Spain.
Alinyongwa kwa amri ya Dikteta wa Hispania, Jenerali Fransisco Franco wkati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
1969 - Vitor Baia anazaliwa.
Ni golikipa wa zamani wa Porto, Barcelona na timu ya taifa ya Ureno.