Didier Gomes anaamini Simba wanaweza kuchukua Ubingwa wa Afrika miaka ijayo ingawa wanatakiwa kuwaweka pamoja wachezaji wao bora:
“Kama Simba wanataka ubingwa wasiuze nyota wao, wakikaa kwa pamoja muda mrefu na kuungana bila shaka watachukua ubingwa na kuwa timu tishio hapa Afrika zaidi ya sasa,”
.
“Wachezaji waliosajiliwa kwasasa wengi wao bado wanaendelea kukua hivyo wakija wakaungana na wale waliokuwepo bila shaka watakuwa tishio na hilo lipo wazi.”