Serikali ya Uingereza imetangaza rasmi kuiondoa Tanzania katika orodha ya Nchi ilizoziwekea vikwazo vya usafiri kutokana na janga la Covid 19 na sasa kuanzia October 10, 2021 Msafiri kutoka Tanzania hatokaa karantini akiingia Uingereza lakini sharti awe amepata moja ya chanjo nne ambazo Uingereza inazitambua ambazo ni Pfizer-BioNTech, Oxford- AstraZeneca, Moderna na Janssen na kwa zinazohitaji kuchomwa mara mbili Mtanzania atatakiwa awe amechoma mara zote mbili.
Tanzania sasa inaingia kwenye orodha ya Nchi nyingine 47 ambazo zimeondolewa kwenye red list ‘list nyekundu’ ya Uingereza ambapo sasa ni Nchi 7 pekee zimebaki kwenye red list ya kutoingia Uingereza ambazo ni Peru, Ecuador, Colombia, Panama, Haiti, Venezuela na Dominican Republic.
View attachment 1968492