Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210714_150801.jpg
 
Ni kauli ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu leo Dar es salaam kwenye kongamano la mwaka mmoja toka kifo cha Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa lililoandaliwa na

Pamoja na mambo mengine aliyoyaongea Rais Samia kuhusu Hayati Benjamin Mkapa, ametilia mkazo umuhimu wa Watu kuendelea kujikinga dhidi ya corona na kusisitiza pia kwamba chanjo Nchini Tanzania halitokua swala la lazima.

“Serikali inaendelea kumtaka kila Mwananchi kuchukua tahadhari dhidi ya Corona, tunaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na ugonjwa huu ambapo kwa sasa tunakamilisha taratibu za kuagiza chanjo kwa ajili ya kinga, mwelekeo ni kwamba kila atakayehitaji huduma ya chanjo iwe inapatikana na chanjo hiyo ni ya hiari” ——— Rais Samia.
20210714_192948.jpg
 
Meya wa Manispaa ya Temeke Abdallah Mtinika amemtamgaza Mkongwe wa Bongofleva Juma Nature kuwa Balozi wa Temeke huu ukiwa ni muendelezo wa Meya huyo kuwapa Ubalozi Wasanii na Watu mashuhuri na sasa Nature atakua kwenye orodha moja na Mkenya Erick Omondi na Mtanzania Mbwana Samatta.

“Leo ni siku kubwa sana kutembelewa na Legend wa TMK tumezungumza mengi sana juu ya kupambania Temeke yetu katika mengi, leo nimemtangaza rasmi kuwa Balozi wa Temeke kikwazo kilikuwa muda tu wa kuja rasmi kumpa bendera yake lakini tayari yeye ni Balozi wa Temeke tangu tulipoanza kutumia maandishi matatu (TMK)”

“Natumai atatusaidia kubeba ajenda za Temeke kama usafi, Watu warudi sokoni, ulinzi na usalama, Temeke bila madawa inawezekana na Temeke na maendeleo, pambana Mwanangu Juma Nature, tupo tunaangalia juhudi zako za kuibeba Temeke”————Mtinika

“Asante Meya Temeke kwa kunitambua na kunithamini, kuniteua kuwa Balozi wa Temeke leo hii” ——— Sir nature
20210714_193328.jpg
 
Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu amesema kwa sasa hakuna Shule ya Sekondari Nchini Tanzania ambayo haina Mwalimu wa Sayansi.

“Katika ajira 6,949 zilizotolewa June 2021, Walimu wa Physics walioajiriwa ni 1,360 na Walimu wa Mathematics ni 599 ambao wamesambazwa katika Shule ambazo hazikuwa na Walimu hao hapo awali”

“Ni imani yangu sasa hakuna shule yoyote ya Sekondari nchini ambayo haina Mwalimu wa sayansi hata mmoja, 2021/22 tunatarajia kuajiri Walimu 10,000 na kipaumbele tutakitoa katika kuajiri Walimu wa Sayansi, tumedhamiria kuboresha Elimu, kazi iendelee”——— Waziri Ummy Mwalimu.
20210714_193502.jpg
 
Uwanja wa mpira wa Lake Tanganyika Kigoma umekamilika kwa 90% kuelekea fainali ya Azam Confideretion Cup Jul 25 ambapo Katibu wa Kamati la Shirikisho la mpira Kigoma (KFA) Omary Gindi uwanja huo utakuwa na uwezo wa kuingiza Mashabiki 17,000 watakaokaa na kusimama.

Katibu huyo pia ametoa wito kwa Mashabiki kutofika uwanjani hapo kwa aajili ya kuchukua nyasi na udongo kwaajili ya kufanya mambo ya jadi "Tulilikemea na kuna baadhi ya Watu walitaka kuchukua mchanga uwanjani tukawatimua, tumeweka ulinzi kuhakikisha mambo ya jadi hayana nafasi, na hakuna shabiki atakayeruhisiwa kuingia uwanjani bila sababu ya msingi" ——— Omary Gindi (KFA)

Mkoa wa KIgoma unakwenda kuandika historia ya kipekee kwa Watani wa jadi Simba na Yanga kucheza mchezo wao mkubwa zaidi kwa Tanzania na Afirka mashariki katika uwanja wa Lake Tanganyika tangu uwanja huo ujengwe.
20210714_193827.jpg
20210714_193849.jpg
 
Hadi sasa idadi ya waliofariki kutokana na vurugu zinazoendelea Nchini South Africa imezidi Watu 70, uharibifu wa mali bado hasara yake ya jumla haijajulikana lakini malori ya mizigo yameendelea kushambuliwa na kuchomwa moto pamoja na nyumba mbalimbali.

Maandamano haya ambayo Wafuasi wanasema wameyafanya kushinikiza kuachiwa huru kwa Rais wa zamani wa South Africa yametoa mianya pia ya Watu kuvunja na kupora kwenye maduka na kuonyesha ghadhabu zao kutokana na ugumu wa maisha na ukosefu wa usawa miongoni mwa Watu wa matabaka mbalimbali ikiwa ni miaka 27 tangu kumalizika kwa utawala wa ubaguzi wa rangi.

Maduka pamoja na mabohari yameporwa au kuchomwa moto, hasa katika mkoa wa nyumbani kwa Zuma, KwaZulu Natal, katika mji mkuu Johannesburg na katika viunga vya mkoa wa Gauteng. View attachment 1853720View attachment 1853721
20210714_194141.jpg
 
Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambae amekita kambi kwenye Mkoa wa Kilimanjaro kushughulikia kero mbalimbali za Maji, amesema kuwa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa Tsh. BILIONI 10 ili zikasaidie kurekebisha miundombinu ya huduma za Majisafi kwenye Wilaya ya Rombo.

Wakati huohuo pia Waziri Aweso ameivunja kampuni ya Kijamii ya Kiliwater na kuelekeza kuanzishwa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Rombo na kumteua Mhandisi Martin Daniel Kinabo kukaimu nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka hiyo.

Mabadiliko haya yamefanyika kwa mujibu wa sheria ya huduma za Maji na Usafi wa mazingira ambapo Mhandisi Kinabo kabla ya uteuzi huu alikuwa Meneja Ufundi wa Kampuni ya Kiliwater, sasa baada ya hayo ni Waziri kuteua bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Rombo.

Kwa upande mwingine pia leo Waziri Aweso amemsimamisha kazi Meneja wa Wilaya (RUWASA) Rombo kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake ya usimamizi wa mradi wa maji ambao ilishindikana kuzinduliwa na Mkimbiza mwenge kutaifa mwaka huu.
20210714_194141.jpg
20210714_194336.jpg
20210714_194359.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu alikuwa Mgeni rasmi leo Dar es salaam kwenye kongamano la mwaka mmoja toka kifo cha Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa lililoandaliwa na mkapa foundation

Pamoja na mambo mengine haya ndio aliyoyaongea Rais Samia kuhusu Hayati Benjamin Mkapa————“Mzee Mkapa wakati wa Uongozi wake alisimamia mageuzi ya kiuchumi, alitoa fursa kwa sekta binafsi na kukaribisha uwekezaji, hatua hizi zilisaidia kuongeza Pato la Serikali kutoka Tsh. Bilioni 331.2 mwaka 1995 hadi kufikia Tsh. Trilioni 2 mwaka 2005”

“Mzee Mkapa alifanikiwa kupunguza Deni la Taifa kutoka 143.7 % ya pato la Taifa tulilokuwa tukidaiwa mwaka 1995 hadi 60.7% mwaka 2005 na hii ni baada ya Mzee Mkapa kuzishawishi Nchi Wahisani na Taasisi za Kifedha za Kimataifa kutusamehe madeni”

“Mzee Mkapa alianzisha Taasisi nyingi wale waliokuwepo wakati huo tunakumbuka slogan yake ya kodi kwanza, kwenye mikutano tulikuwa tunaitana ‘Haloo Haloo, Haloo ya Mkapa kodi kwanza’ alianzisha TRA, PCCB, TASAF, TANROADS, MKURABITA, MKUKUTA n.k”———-Rais SamiaView attachment 1853748View attachment 1853749
20210714_194703.jpg
 
Ni kauli ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu leo Dar es salaam kwenye kongamano la mwaka mmoja toka kifo cha Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa lililoandaliwa na

Pamoja na mambo mengine aliyoyaongea Rais Samia kuhusu Hayati Benjamin Mkapa, ametilia mkazo umuhimu wa Watu kuendelea kujikinga dhidi ya corona na kusisitiza pia kwamba chanjo Nchini Tanzania halitokua swala la lazima.

“Serikali inaendelea kumtaka kila Mwananchi kuchukua tahadhari dhidi ya Corona, tunaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na ugonjwa huu ambapo kwa sasa tunakamilisha taratibu za kuagiza chanjo kwa ajili ya kinga, mwelekeo ni kwamba kila atakayehitaji huduma ya chanjo iwe inapatikana na chanjo hiyo ni ya hiari” ——— Rais Samia.View attachment 1853675
OK Mama
 
UNAAMBIWA

Wale Watu ambao hutumia nguvu kubwa kuangalia nyota zao wakitafuta Watu wenye nyota zinazoendana na wao wanapoteza muda tu.

Utafiti wa Chuo Kikuu cha Manchester unaeleza kuwa mambo ya nyota hayana uhusiano na mambo ya Mapenzi, ndoa au kudumu kwenye ndoa.

“Tumetafiti Birthday za Maharusi Milioni 20 England, Wales na sehemu nyingine na tumejiridhisha hakuna uhusiano wowote kati ya makundi ya nyota na Watu kupendana, wale wanaosema Mimi nyota yangu hii nastahili kuolewa au kuwa kwenye Mapenzi na mwenye nyota fulani ni kujidanganya tu”
20210714_194907.jpg
 
UNAAMBIWA

Utafiti wa ONS unaeleza kuwa jina analopewa Mtoto wa kike la ‘Karen’ linakaribia kutoweka na huenda lisisikike tena miaka ya mbele kwasababu kadri siku zinavyosogea ni Watoto wachache huitwa Karen.

Mwaka 2018 nchini Uingereza ni Watoto 21 pekee waliitwa Karen…. kibongobongo ni majina gani yanapotea?
20210714_195034.jpg
 
UNAAMBIWA

Waigizaji wa Filamu nchini Misri katika miaka ya nyuma hawakuwa wanaruhusiwa kuwa Mashahidi Mahakamani kwasababu walichukuliwa ni Watu wenye utaalamu wa kudanganya na kwamba wana uwezo wa kusema uongo na Watu wakaamini ni kweli.
20210714_195139.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom